Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuko Siku Hatutakosa Mambo ya Lazima?

Kuko Siku Hatutakosa Mambo ya Lazima?

 Mu inchi za mingi, watu wanafanya maandamano mu barabara juu wanakosa mambo ya lazima. Mambo ilikuwa mubaya tena zaidi wakati ya ugonjwa wa Coronavirus wenye ulifanya watu wakose furaha juu ya kubakia tu ku nyumba, kukosa chakula, na kukosa matunzo. Na ile ilifanya tofauti kati ya matajiri na maskini ikuwe wazi zaidi.

 Kuko siku hatutakosa mambo ya lazima? Ndiyo. Biblia inaonyesha mambo yenye Mungu atafanya juu ya kumaliza magumu yetu.

Magumu yenye Mungu atamaliza

 Magumu: Serikali zimeshindwa kutimizia kila mutu mambo ya lazima.

 Mambo yenye Mungu atafanya: Mungu atatosha serikali zote za wanadamu na kutia serikali yake yenye inaitwa Ufalme wa Mungu. Itakuwa mbinguni na itatawala dunia yote.—Danieli 2:44; Matayo 6:10.

 Matokeo: Juu Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote, utasimamia muzuri mambo yote ku dunia. Hakutakuwa tena watu maskini, na watu hawatakosa mambo ya lazima. (Zaburi 9:7-9, 18) Watafurahia matokeo ya kazi yao, na kuishi maisha yenye kutosheka pamoya na familia zao. Biblia inasema hivi: “Watajenga nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani, wala hawatapanda ili wengine wakule.”—Isaya 65:21, 22.

 Magumu: Watu hawawezi kuepuka hali zenye zinafanya wateseke na wakose mambo ya lazima.

 Mambo yenye Mungu atafanya: Kupitia Ufalme wake, Mungu atamaliza mambo yote yenye inafanya watu waogope na wakose usalama.

 Matokeo: Wakati Ufalme wa Mungu utatawala, watu na familia zao hazitakosa tena mambo ya lazima. Kwa mufano, vita, kukosa chakula, na magonjwa haitakuwa tena. (Zaburi 46:9; 72:16; Isaya 33:24) Mungu anasema hivi: “Watu wangu watakaa katika makao yenye amani, katika makao salama na katika mahali pa kupumuzikia penye utulivu.”—Isaya 32:18.

 Magumu: Mara nyingi watu wenye kutafuta tu faida zao na wenye pupa wanatesaka wanadamu wenzao.

 Mambo yenye Mungu atafanya: Watu wenye watatawaliwa na Ufalme wa Mungu watajifunza kupenda wengine zaidi ya vile wanajipenda wenyewe.—Matayo 22:37-39.

 Matokeo: Wakati Ufalme wa Mungu utatawala, kila mutu ataiga upendo wa Mungu wenye “hautafute faida zake wenyewe.” (1 Wakorinto 13:4, 5) Biblia inasema hivi: “Hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza wala uharibifu wowote katika mulima wangu wote mutakatifu, kwa maana dunia hakika itajaa ujuzi juu ya Yehova a kama vile maji yanafunika bahari.”—Isaya 11:9.

 Biblia inaonyesha kama tunaishi siku za mwisho za hii dunia na kama karibuni Mungu atatimiza ahadi yake ya kumaliza magumu yote yenye inafanya watu wakose mambo ya lazima. b (Zaburi 12:5) Mbele ile wakati ifike, kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia wakati tunakosa mambo ya lazima. Kwa mufano, ona habari “Jinsi ya Kuishi Ukiwa na Pesa Kidogo” na “Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza.”

a Biblia inaonyesha kama Yehova njo jina ya Mungu.—Zaburi 83:18.

b Juu ya kujifunza sababu gani unaweza kutegemea Biblia, ona habari “Biblia Ni Kitabu Chenye Kinatusaidia Kupata Kweli.”