Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inasema Nini juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Wakati Wetu Wenye Kuya?

Biblia Inasema Nini juu ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Wakati Wetu Wenye Kuya?

 “Hali ya hewa inakuwa ya mubaya sana, na ile inafanya dunia isikuwe tena fasi ya muzuri kuishi.”—The Guardian.

 Wanadamu wako na magumu yenye wamejiletea wao wenyewe. Wanasayansi wengi wanasema kama mambo yenye wanadamu wako nafanya njo inafanya kukuwe kifukutu sana ku dunia. Kuongezeka kwa kifukutu kumefanya kukuwe mabadiliko ya hali ya hewa na kumeleta matokeo mingi ya mubaya. Ona tu mifano fulani:

  •   Kunakuwa hali mingi za hewa zenye kuwa za mubaya zaidi na zenye kutokea mara mingi, ile inatia ndani kifukutu mingi sana, ukame ao sècheresse, upepo mukali, yenye nayo inaleta mvua mingi sana yenye inafanya maji iyale, na pia moto wa pori.

  •   Kuyeyuka kwa miamba ya barafu na barafu ya Aktiki.

  •   Kuongezeka sana kwa maji mu bahari.

 Magumu ya hali ya hewa imekuwa na matokeo mu dunia yote. Kisha kuzungumuzia hali zenye kuwa mu inchi 193, ripoti moya ya gazeti New York Times ilisema hivi: “Dunia iko inatuomba musaada.” Juu mabadiliko ya hali ya hewa imefanya kukuwe vifo na mateso, Shirika ya Afya Ulimwenguni ilisema kama ile mabadiliko ya hewa njo “hatari kubwa zaidi ya afya yenye wanadamu wako wanapambana nayo.”

 Lakini, hatuna sababu ya kuogopa juu ya wakati wetu wenye kuya. Biblia ilitabiri mambo yenye iko inatokea leo, na pia inaonyesha sababu yenye inafanya tutumainie kama Mungu atabadilisha hali yetu, na pia mambo yenye atafanya ili kulinda wakati wetu wenye kuya.

Mabadiliko ya hali ya hewa iko inatimiza unabii wa Biblia?

 Ndiyo. Mabadiliko ya hali ya hewa yenye inaleta kuongezeka kwa kifukutu inapatana kabisa na mambo yenye Biblia ilitabiri juu ya wakati wetu.

 Unabii: Mungu ‘ataharibu wale wenye kuharibu dunia.’—Ufunuo 11:18.

 Biblia ilitabiri kama kungekuwa wakati wenye matendo ya wanadamu ingekaribia kuharibu kabisa dunia. Na juu kifukutu inaongezeka sana, tunaona kama leo watu wanaharibu dunia.

 Ile unabii inatusaidia kuelewa sababu moya yenye kuonyesha juu ya nini hatupaswe kutumainia kama wanadamu watalinda dunia. Mungu atafanya jambo fulani wakati watu watakuwa “wanaharibu dunia.” Kuko watu wenye kufanya yao yote juu ya kulinda hali yetu ya hewa. Lakini hata vile, ile haitatosha ili kuzuia wanadamu wasiharibu dunia.

 Unabii: “Kutakuwa mambo yenye kuogopesha.”—Luka 21:11.

 Biblia ilitabiri kama “kutakuwa mambo yenye kuogopesha,” ni kusema, matukio fulani yenye kuogopesha ingetokea mu wakati wetu. Mabadiliko ya hali ya hewa imeleta mambo yenye kuogopesha mu dunia yote. Leo, watu fulani wako wanaogopa kama siku moya wanaweza kufa kwa sababu ya hali ya mubaya ya hewa.

 Unabii: “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, . . . wenye hawana ushikamanifu, . . . wenye hawataki makubaliano yoyote, . . . wasaliti, wenye vichwa vigumu.”—2 Timoteo 3:1-4.

 Biblia ilitabiri tabia za wanadamu zenye zimeleta hali ya mubaya ya hewa. Serikali na mambo ya biashara zinatafuta kwanza faida zao bila kufikiria hata kama hali ya kesho ya watu itakuwa namna gani. Wanajikaza wakati fulani kutumika pamoya, lakini wapi! Wanashindwa kupatana kuhusu mambo yenye inaomba kufanya ili kuzuia kifukutu isiendelee kuwa mingi.

 Ile unabii inaonyesha kama hatupaswe kutazamia kama watu kwa ujumla watabadilisha matendo yao na kulinda dunia. Lakini, Biblia inasema kama watu wenye kujifirikia tu wao wenyewe “wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.”—2 Timoteo 3:13.

Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Mungu atabadilisha mambo?

 Biblia inaonyesha kama Yehova a Mungu, Muumbaji wetu, anahangaikia sana dunia na wenye kuishi ndani. Ona tu maandiko tatu yenye kuonyesha kama Mungu atabadilisha mambo.

  1.  1. Mungu ‘hakuumba [dunia] tu bila sababu, lakini aliifanya ili ikaliwe na watu.’—Isaya 45:18.

     Mungu atatimiza kusudi yake kuhusu dunia. (Isaya 55:11) Hataruhusu iharibiwe ao ibakie bila kuikaliwa.

  2.  2. “Wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani. Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”—Zaburi 37:11, 29.

     Mungu anaahidi kama wanadamu wataishi hapa ku dunia milele na kwa amani.

  3.  3. “Waovu, wataondolewa katika dunia, na wadanganyifu watangolewa kutoka ndani yake.”—Mezali 2:22.

     Mungu anaahidi kama ataondoa ao kuharibu wale wenye kuendelea kufanya mambo ya mubaya, kutia ndani wale wenye kuharibu dunia.

Mambo yenye Mungu atatufanyia mu wakati wenye kuya

 Namna gani Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu dunia? Atatumia guvernema yenye itatawala dunia yote, ndiyo, Ufalme wa Mungu. (Matayo 6:10) Ile Ufalme itatawala na iko mbinguni. Haitafanya mapatano na serikali za wanadamu juu ya mambo yenye kuhusu dunia na hali ya hewa. Lakini, ile Ufalme itakamata fasi ya ma guvernema ya wanadamu.—Danieli 2:44.

 Ufalme wa Mungu ni habari njema kwa wanadamu wote na pia kwa planete yetu. (Zaburi 96:10-13) Ona mambo yenye Yehova Mungu atafanya kupitia Ufalme wake.

  •   Kufanya planete ikuwe ya muzuri

     Mambo yenye Biblia inasema: “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”—Isaya 35:1.

     Ile iko na maana gani juu ya wakati wetu wenye kuya? Yehova ataponyesha planete yetu, hata fasi zenye wanadamu waliharibisha.

  •   Yehova atafanya kusikuwe tena hali ya mubaya ya hewa

     Mambo yenye Biblia inasema: “[Yehova] anatuliza zoruba yenye upepo mukali; mawimbi ya bahari yananyamaza.”—Zaburi 107:29.

     Ile iko na maana gani juu ya wakati wetu wenye kuja? Yehova iko na uwezo wa kuongoza nguvu za asili. Hakuna siku watu watateseka tena kwa sababu ya hali ya mubaya ya hewa.

  •   Kufundisha wanadamu namna ya kutunza dunia

     Mambo yenye Biblia inasema: “Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata.”—Zaburi 32:8.

     Ile iko na maana gani juu ya wakati wetu wenye kuja? Yehova alipatia wanadamu daraka ya kutunza dunia. (Mwanzo 1:28; 2:15) Atatufundisha njia ya muzuri zaidi ya kutimiza ile daraka ya kutunza uumbaji wake, na kuishi mu njia yenye haitaharibisha planete yetu.

a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Ona habari “Yehova Ni Nani?