Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia ya Bedell—Ilisaidia Watu Kuelewa Biblia Muzuri

Biblia ya Bedell—Ilisaidia Watu Kuelewa Biblia Muzuri

WAKATI William Bedell, padri Muingereza, alienda Irelandi katika mwaka wa 1627, alikuta hali yenye kushangaza sana. Inchi ya Irelandi yenye kuwa na Wakatoliki wengi, ilikuwa inatawaliwa na inchi ya Uingereza ya Kiprotestanti. Waprotestanti wa Marekebisho Makubwa walikuwa wametafsiri Biblia katika luga za wenyeji katika Ulaya yote. Lakini, hakuna mutu alionekana kuwa anapendezwa kuitafsiri katika luga ya Kiirelandi.

Bedell aliona kabisa kuwa watu wa Irelandi, “hawapaswe kupuuzwa mupaka wajifunze Kiingereza.” Aliamua kutafsiri Biblia katika luga ya Kiirelandi. Lakini alipingwa vikali, zaidi sana na Kanisa la Waprotestanti. Sababu gani?

UPINZANI JUU YA KUTUMIKISHA LUGA YA KIIRELANDI

Bedell aliamua kujifunza luga ya Kiirelandi. Wakati alikuwa mukuu wa masomo ya Trinity ya Dublin na wakati alikuwa askofu wa Kilmore, alitia wanafunzi moyo kutumikisha luga ya Kiirelandi. Jambo la hakika ni kwamba, wakati Malkia Elizabeth wa 1 wa Uingereza alianzisha masomo hayo ya Trinity, alikuwa na kusudi la kuzoeza mapadri wenye wangeweza kufundisha watu habari ya Biblia katika luga yao. Bedell alipima kutimiza jambo hilo.

Katika Diocèse ya Kilmore, watu wengi walikuwa wanasema Kiirelandi. Kwa hiyo, Bedell alikazia kuwe na mapadri wenye kujua kusema Kiirelandi. Jambo aliomba lilipatana na maneno ya mutume Paulo kwenye 1 Wakorintho 14:19, yenye kusema hivi: ‘Katika kutaniko ingekuwa afazali niseme maneno matano kwa akili yangu, ili pia niwafundishe wengine kwa mudomo, kuliko maneno elfu kumi kwa luga,’ ni kusema, luga yenye haieleweke muzuri.

Lakini watu wenye mamlaka walifanya yao yote ili kumuzuia. Kulingana na wanahistoria, watu fulani wenye mamlaka waliona kama kutumia luga ya Kiirelandi kulikuwa “hatari juu ya Taifa” na wengine waliona kama “haingekuwa kwa faida ya Serikali.” Watu fulani waliona kama ilikuwa kwa faida ya Uingereza watu wasitumie luga ya Kiirelandi. Kwa kweli, sheria zilitungwa zenye ziliomba Wairelandi waache luga yao na desturi zao na wajifunze Kiingereza na kufuata njia na tabia za Waingereza.

KAZI YA BEDELL YA KUTAFSIRI BIBLIA

Bedell hakuvunjwa moyo na mawazo kama hayo ya madikteta. Mwanzoni mwa miaka kati ya 1631 na 1640, alianza kutafsiri Biblia katika Kiirelandi kwa kutumia Biblia ya Kiingereza yenye ilikuwa ya mwisho kuchapishwa wakati huo (King James Version ya mwaka wa 1611). Alitaka kutafsiri Biblia yenye watu wengi wangeelewa. Alisadiki kabisa kama watu masikini hawangechunguza Maandiko ili wapate njia ya uzima wa milele ikiwa hawana Biblia katika luga yao.—Yohana 17:3.

Bedell hakukuwa mutu wa kwanza kuwaza hivyo. Miaka karibu 30 mbele ya hapo, askofu mwengine, William Daniel, alikuwa ameona kama ilikuwa vigumu sana kwa watu kujifunza mambo Biblia inafundisha “katika luga yenye haijulikane.” Daniel alikuwa ametafsiri Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiirelandi. Sasa Bedell alianza kutafsiri Maandiko ya Kiebrania. Biblia ya Bedell inatia ndani sehemu yenye Bedell alitafsiri na sehemu yenye William Daniel alitafsiri mbele yake. Kwa kweli, Biblia ya Bedell, ni kusema Biblia ya kwanza yenye ilitafsiriwa yote nzima katika Kiirelandi, ndiyo tu ilikuwa Biblia nzima ya Kiirelandi kwa miaka 300 iliyofuata.

Bedell, mwenye alikuwa anajua sana Kiebrania, aliomba watu wawili wenye Kiirelandi ilikuwa luga yao ya kizalikio wamusaidie kutafsiri Biblia ya Kiingereza katika Kiirelandi. Wakati kazi ilikuwa inaendelea, Bedell pamoja na musaidizi mumoja ao wawili wenye kutumainika, walichunguza na kurudilia kila mustari kwa uangalifu. Ili kufanya hivyo, walichunguza tafsiri ya mwanateolojia Muswisi, Giovanni Diodati, walichunguza pia tafsiri ya Biblia ya Kigiriki inayoitwa Septante, na maandishi fulani ya zamani ya Biblia katika Kiebrania yenye yalikuwa ya maana sana.

Kikundi hicho cha watafsiri kilifuata mufano wa watafsiri wa King James Version (inawezekana Bedell alijuana na wengi kati yao) na wakatia jina la pekee la Mungu nafasi mbalimbali katika Biblia yao. Kwa mufano, kwenye Kutoka 6:3, walitafsiri jina la Mungu kuwa “Iehovah.” Biblia ya kwanza kabisa ya Bedell inapatikana katika Jumba la Kuchungia Vitabu la Marsh, Dublin, Irelandi.—Soma kisanduku “Bedell Anakumbukwa na Kazi Yake Inatambuliwa.”

INAFIKIA KUCHAPISHWA

Bedell alimaliza kazi yake ya kutafsiri Biblia katika mwaka wa 1640 hivi. Lakini hangeweza kuichapisha mara moja. Sababu gani? Sababu moja ni kwamba aliendelea kupingwa sana. Wachambuzi waliharibishia sifa mutafsiri mukubwa wa Bedell, wakitumaini kuwa hilo litafanya watu wazarau kazi yake. Kwa ujanja, walifikia hata kumukamata na kumufunga katika gereza. Zaidi ya hilo, Bedell alijikuta katikati ya wauaji wenye hasira ambao waliasi utawala wa Uingereza; uasi huo ulitokea katika mwaka wa 1641. Hata kama Bedell alikuwa Muingereza, Wairelandi wa eneo lake walimulinda kwa muda fulani kwa sababu walijua kuwa alikuwa anapendezwa nao kweli kweli. Lakini, mwishowe maaskari waasi walimufunga katika hali mbaya sana. Kwa kweli, hilo lilifanya akufe haraka katika mwaka wa 1642. Alikufa bila kuona Biblia yake inachapishwa.

Ukurasa wa kwanza wa maandishi ya kwanza-kwanza ya Bedell, mwaka wa 1640 hivi, na Biblia yenye ilichapishwa mwaka wa 1685

Ilionekana kuwa kazi ya Bedell ilipotea kabisa wakati walinyanganya kila kitu katika nyumba yake na wakaiharibisha. Jambo la kufurahisha ni hili: rafiki yake mumoja wa sana aliokoa maandishi yote yenye alikuwa ametafsiri. Kisha, Narcissus Marsh mwenye alifikia kuwa askofu mukubwa wa muji wa Armagh na mukubwa wa Kanisa la Irelandi, alipata maandishi hayo. Mwanasayansi Robert Boyle alimupatia musaada wa feza na bila woga akachapisha Biblia ya Bedell katika mwaka wa 1685.

HATUA NDOGO LAKINI YA MAANA

Biblia ya Bedell haikukubaliwa na watu wote katika dunia. Ilikuwa hatua ndogo lakini ya maana yenye ilisaidia watu kuelewa Biblia muzuri, zaidi sana watu wenye kusema Kiirelandi. Haikusaidia watu katika inchi ya Irelandi tu lakini pia katika inchi ya Écosse, na katika maeneo mengine mengi. Sasa wangeweza kutimiza uhitaji wao wa kiroho kwa kusoma Neno la Mungu katika luga yao ya kizalikio.—Mathayo 5:3, 6.

“Wakati tulisoma Biblia ya Bedell, tulisikia maneno ya Biblia katika luga yetu ya kizalikio. Hiyo ilikuwa hatua ya maana sana yenye ilinisaidia mimi na familia yangu kujifunza mafundisho ya muzuri yenye kuwa katika Maandiko”

Biblia ya Bedell imeendelea kusaidia watu wenye kupenda kweli kufanya hivyo mupaka leo. Mwanaume mumoja mwenye kusema Kiirelandi, ambaye hivi karibuni alijifunza mambo Biblia inafundisha kabisa, anasema hivi: “Wakati tulisoma Biblia ya Bedell, tulisikia maneno ya Biblia katika luga yetu ya kizalikio. Hiyo ilikuwa hatua ya maana sana yenye ilinisaidia mimi na familia yangu kujifunza mafundisho ya muzuri yenye kuwa katika Maandiko.”