Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ninapaswa Kukopa Feza?

Ninapaswa Kukopa Feza?

“Kukopa arusi; kulipa matanga.”—Mezali ya Kiswahili.

WATU wa Afrika ya Mashariki wanajua sana maneno hayo, na yanaonyesha namna watu wa inchi nyingi katika dunia wanaona kukopa (kukongola). Wewe pia unaona vile juu ya kukopa feza kwa rafiki ao nafasi zingine? Hata ikiwa kukopa kunaweza kuwa jambo lenye kufaa wakati fulani, je, ni wazo la muzuri? Kukopa kunaleta hatari na mitego gani?

Mezali ingine ya Kiswahili inaeleza tatizo kubwa la kukopa linaweza kuwa gani. Inasema hivi: ‘Kinachoharibisha urafiki ni kukopa na kuazima.’ Kwa kweli, madeni yanaweza kuharibisha urafiki na uhusiano kati ya watu. Hata ikiwa mutu anakopa akiwa na mipango na makusudi ya muzuri, mambo hayaendeke siku zote kama vile alitumainia. Kwa mufano, ikiwa wakati unapita na deni halijalipwa, mutu aliyekopesha (aliyekongwesha) anaweza kukasirika. Hasira inaweza kuanza, na uhusiano unaweza kuharibika kati ya mutu aliyekopesha na mutu aliyekopa, na hata kati ya familia zao. Kwa kuwa mikopo inaleta kutoelewana, tunaweza kuiona kuwa njia ya mwisho ya kutusaidia wakati tuko na matatizo ya feza; hatupaswe kuiona kuwa njia nyepesi ya kutusaidia.

Kukopa feza kunaweza kuharibisha uhusiano wa mutu na Mungu. Namna gani? Kwanza, Biblia inasema kuwa ni mutu muovu ndiye anakataa kimakusudi kulipa madeni yake. (Zaburi 37:21) Tena inasema waziwazi kuwa ‘mukopaji ni mutumwa wa mukopeshaji.’ (Methali 22:7, Biblia Habari Njema) Mutu anayekopa anapaswa kujua kuwa anakuwa mutumwa wa mutu aliyemukopesha mupaka wakati atalipa deni. Mezali hii ingine ya Afrika ni ya kweli: “Ikiwa unakopa miguu ya mutu, utaenda mahali anakuongoza.” Wazo ni hili: mutu mwenye kuwa na deni nyingi hana uhuru wa kufanya mambo anapenda.

Kwa hiyo, kulipa deni kunapaswa kuonwa kuwa jambo la maana sana. Ikiwa mutu halipe deni, magumu yanaweza kutokea. Madeni mengi yanaweza kuleta huzuni nyingi, kumufanya mutu akose usingizi usiku, atumike kupita kiasi, yanaweza kuleta mabishano kati ya bibi na bwana, na hata kuvunja familia, yanaweza pia kufanya mutu ashitakiwe kisheria ao kufungwa. Kuna hekima katika maneno ya andiko la Waroma 13:8 linalosema hivi: ‘Musiwe na deni la hata jambo moja la mutu yeyote, isipokuwa kupendana.’

 NI LAZIMA KUKOPA?

Kulingana na mambo hayo, ni jambo la muzuri kuwa muangalifu wakati inaomba kukopa feza. Ni jambo la hekima kujiuliza hivi: Kuna lazima kabisa ya kukopa? Ni ili upate feza za kukusaidia uhangaikie mahitaji ya familia yako? Ao, kuna aina fulani ya pupa, pengine tamaa ya kuishi zaidi ya mapato yako? Katika hali nyingi, inaweza kuwa muzuri kutosheka na kidogo uliyo nayo kuliko kulazimika kukopa.

Bila shaka, kunaweza kuwa hali zingine zinazoweza kumulazimisha mutu akope feza, kama vile wakati kuna mambo yanayoomba kutenda haraka na inaonekana hakuna jambo lingine la kufanya. Hata hivyo, ikiwa mutu anaamua kukopa, anapaswa kujionyesha kuwa mutu mwenye kuaminika. Namna gani?

Kwanza, usitafute kufaidika na mutu fulani kwa sababu tu anaonekana kuwa na feza nyingi kupita wengine. Hatupaswe kuwaza kama wakati tunamuona mutu fulani kuwa ana feza nyingi maana yake analazimika kutusaidia kwa kutupatia feza. Wala hatupaswe kujisikia kuwa hatuna daraka la kutendea mutu kama huyo kwa uaminifu. Usitamani watu wanaoonekana kuwa na feza nyingi.—Methali 28:22.

Kisha, ujikaze kulipa deni, na ufanye hivyo bila kukawia. Ikiwa mutu anayekukopesha hakuwekee tarehe ya kulipa deni, unapaswa wewe mwenyewe kuweka tarehe na kuiheshimu. Ni vizuri muandike mapatano yenu ili kuepuka kutoelewana. (Yeremia 32:9, 10) Ikiwa inawezekana, urudishe wewe mwenyewe kitu ulichokopa kwa mutu aliyekukopesha ili umushukuru wewe mwenyewe. Kuonyesha uaminifu kwa kurudisha feza ulizokopa kutafanya ukuwe na uhusiano muzuri na mutu aliyekukopesha. Katika Mahubiri yake ya Mulimani Yesu alisema hivi: ‘Muache tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo.’ (Mathayo 5:37) Tena, kumbuka kila wakati Kanuni Bora: ‘Kwa hiyo, mambo yote munayotaka watu wawatendee ninyi, lazima muwatendee wao pia vivyo hivyo.’—Mathayo 7:12.

KANUNI ZA BIBLIA ZENYE KUSAIDIA

Biblia inatoa dawa nyepesi inayoweza kukusaidia ushinde tamaa ya kukopa feza. Inasema hivi: “Kwa hakika, huo ni njia ya kupata faida kubwa, huu ujitoaji-kimungu pamoja na ujitoshelevu [ao kutosheka].” (1 Timotheo 6:6) Kwa maneno mengine, kutosheka na vitu vyenye mutu iko navyo ni njia ya muzuri ya kuepuka matokeo mabaya ya kukopa. Hata hivyo, kwa kweli, haiko vyepesi kutosheka katika dunia ya leo inayochochea watu watimize tamaa zao palepale. Katika hali hiyo, ni jambo la maana kuwa na “ujitoaji-kimungu.” Namna gani?

Kwa mufano, fikiria bibi na bwana fulani Wakristo katika Asia. Katika ndoa yao walipokuwa wangali vijana, walikuwa wanatamani watu waliokuwa na uwezo wa kununua nyumba yao wenyewe. Kwa hiyo, waliamua kununua nyumba kwa feza walizokuwa wanaweka na feza walizokopa kwenye benki na kwa watu wa familia. Hata hivyo, bila kukawia, walianza kujisikia kuwa na muzigo muzito kwa sababu ya kulipa feza nyingi kila mwezi. Walichukua kazi ya zaidi na kuanza kutumika siku nzima, na hilo lilifanya wakose wakati wa kupitisha pamoja na watoto wao. Bwana alisema hivi: “Mahangaiko ya akili, maumivu, na kukosa usingizi vilinifanya nijisikie kuwa mwenye kubeba jiwe kubwa kwenye kichwa. Tulikosa amani.”

“Kuona vitu vya kimwili kwa njia ya kiroho ni ulinzi”

Kisha wakati kupita, walikumbuka maneno ya andiko la 1 Timotheo 6:6 na wakaamua kuwa njia moja ya kumaliza tatizo hilo ilikuwa kuuzisha nyumba hiyo. Iliwachukua miaka mbili mbele washushe muzigo huo. Bibi na bwana hao walijifunza nini kutokana na jambo hilo? Walisema kuwa “kuona vitu vya kimwili kwa njia ya kiroho ni ulinzi.”

Watu wengi wanajua mezali ya Kiswahili tuliyotaja kwenye mwanzo wa habari hii. Lakini kujua mezali hiyo hakuzuie watu kukopa. Kupitia kanuni za Biblia tulizozungumuzia, hauone kuwa inaweza kuwa jambo la hekima kufikiri kwa uangalifu juu ya ulizo hili: Ninapaswa kukopa feza?