Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Namna gani watoto wanaweza kujifunza kumupenda Mungu?

Tumikisha habari za uumbaji ili kusaidia watoto wako wamujue Mungu na kumupenda

Watoto wako wanaweza kujifunza kumupenda Mungu ikiwa tu wako hakika kuwa Mungu iko na kuwa anawapenda. Ili kumupenda Mungu, wana lazima ya kumujua. (1 Yohana 4:8) Kwa mufano, wana lazima ya kujua: Mungu alikuwa na kusudi gani alipoumba mutu? Sababu gani Mungu anaacha watu wateseke? Mungu atafanyia watu nini wakati unaokuja?—Soma Wafilipi 1:9.

Ili kusaidia watoto wako wamupende Mungu, unapaswa kuwaonyesha kuwa wewe mwenyewe unamupenda. Wakati wanaona hivyo, labda watafuata mufano wako.—Soma Kumbukumbu la Torati 6:5-7; Methali 22:6.

Namna gani unaweza kugusa mioyo ya watoto wako?

Neno la Mungu liko na nguvu. (Waebrania 4:12) Kwa hiyo, saidia watoto wako wajue mafundisho ya musingi ya Neno la Mungu. Ili kugusa mioyo ya watu, Yesu aliuliza maulizo, alisikiliza, na kufasiria Maandiko. Ili kugusa mioyo ya watoto wako, unaweza kuiga njia ya Yesu ya kufundisha.—Soma Luka 24:15-19, 27, 32.

Tena, habari za Biblia juu ya namna Mungu alitendea watu zinaweza kusaidia watoto wamujue Mungu na kumupenda. Vitabu vinavyoweza kusaidia kufanya hivyo vinapatikana kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com.—Soma 2 Timotheo 3:16.