Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Walitumia Biblia ili Kujibu Kila Ulizo!

Walitumia Biblia ili Kujibu Kila Ulizo!
  • ALIZALIWA MWAKA WA 1950

  • INCHI HISPANIA

  • ALIKUWA MUTAWA MWANAMUKE (MAMA) MUKATOLIKI

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Wakati nilizaliwa, wazazi wangu walikuwa na shamba ndogo katika kijiji cha mashambani cha Galicia, kaskazini​-mangaribi mwa Hispania. Nilikuwa mutoto wa ine katika familia ya watoto munane. Familia yetu ilikuwa yenye furaha. Wakati huo katika Hispania, ilikuwa kawaida mutoto mumoja katika familia aingie kwenye seminari ao kwenye makao ya watawa. Katika familia yetu, watoto tatu kati yetu walienda huko.

Nilipokuwa na miaka 13, nilienda kwenye makao ya watawa katika muji wa Madrid ambako dada yangu alikuwa. Katika makao hayo ya watawa, watu hawakuwa wanahangaikiana. Watu hawakufanya urafiki, kulikuwa tu sheria, sala, na hatukuwa na uhuru. Asubuhi mapema, tulikusanyika katika kanisa ndogo ili kutafakari ao kufikiri sana, lakini mara nyingi sikuwa na mambo ya kufikiri. Kisha hapo, tuliimba nyimbo za kidini na kuhuzuria Misa, tulifanya mambo yote hayo katika luga ya Kilatini. Sikusikia karibu jambo lolote na nilijisikia kuwa Mungu alikuwa mbali na mimi. Siku zangu zilipita kimyakimya katika makao ya watawa. Hata wakati tulikutana na dada yangu, tulikuwa tunasema tu, “Maria mutakatifu atukuzwe.” Watawa walituruhusu tuzungumuze kati yetu kwa dakika makumi tatu tu kisha kula. Maisha hayo yalikuwa tofauti kabisa na maisha ya furaha ya nyumbani kwetu! Nilijisikia kuwa mwenye kutengwa kabisa na mara nyingi nililia.

Hata ikiwa sikujisikia kuwa karibu na Mungu hata siku moja, nilipokuwa na miaka 17, nilifanya viapo vyangu na nikakuwa mutawa. Kwa kweli, nilifanya tu mambo niliyoombwa, lakini bila kukawia nilianza kuwa na mashaka ikiwa Mungu alinichagua kabisa ili kuwa mutawa. Watawa walizoea kusema kuwa wale walio na mashaka kama hayo wataingia katika moto wa mateso! Lakini, niliendelea tu kuwa na mashaka. Nilijua kwamba Yesu Kristo hakujitenga; lakini, aliendelea kufundisha kwa bidii na kusaidia watu. (Mathayo 4:23-25) Nilipokuwa na miaka 20, sikuona tena sababu nzuri za kunifanya niendelee kuwa mutawa. Jambo la kushangaza, mutawa mwanamuke aliyesimamia makao yetu aliniambia kwamba ikiwa sina uhakika kuwa nitabaki mutawa, ni vizuri nitoke haraka. Ninawaza alisema hivyo kwa sababu aliogopa kuwa nitachochea wengine. Kwa hiyo, nilitoka kwenye makao ya watawa.

Niliporudia nyumbani, wazazi wangu walinielewa. Lakini kwa sababu sikupata kazi katika kijiji chetu, nilihamia katika inchi ya Ujerumani, ambako kaka yangu mumoja alikuwa anaishi. Alikuwa mutu wa kikundi cha Wakomunisti kilichoundwa na Wahispania waliohamia Ujerumani. Nilijisikia huru kati ya watu hao waliotetea haki za wafanyakazi na kutokubagua wanawake. Kwa hiyo, nikajiunga na kikundi cha Wakomunisti na kisha nikaolewa na mwanaume wa kikundi hicho. Niliwaza kuwa nilikuwa ninafanya jambo fulani la maana, niligawanya vitabu vya Wakomunisti na kushiriki katika maandamano ya kupinga serikali.

Lakini, baada ya muda, nilivunjika moyo. Niliona kuwa Wakomunisti walishindwa mara nyingi kutimiza mambo waliyokuwa wanatetea. Mashaka yangu yaliongezeka katika mwaka wa 1971 wakati vijana fulani wa kikundi chetu waliunguza biro ya balozi ao muakilishi wa inchi ya Hispania, biro hiyo ilikuwa katika muji wa Frankfurt. Walifanya hivyo ili kupinga ukosefu wa haki wa inchi ya Hispania iliyokuwa na utawala wa udikteta. Lakini niliamini kuwa hiyo haikuwa njia nzuri ya kuonyesha hasira.

Wakati nilizaa mutoto wangu wa kwanza, nilimuambia bwana yangu kwamba sitaendelea kushiriki mikutano ya Wakomunisti. Nilijisikia kabisa kuwa peke yangu kwa sababu hakuna hata mumoja wa marafiki wangu wa zamani aliyekuja kuniona mimi na mutoto wangu. Nilijiuliza maisha yana kusudi gani. Je, lilikuwa jambo la maana kabisa kujikaza ili kuleta mabadiliko katika maisha ya watu?

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Katika mwaka wa 1976, Mashahidi wa Yehova wawili wa inchi ya Hispania walitutembelea nyumbani na wakatutolea vichapo fulani vinavyotegemea Biblia. Nilikubali vichapo hivyo. Walipotutembelea mara ya pili, nilianza kuwauliza maulizo mengi moja baada ya lingine juu ya mateso, kukosa kuona watu kuwa sawasawa, na ukosefu wa haki. Nilishangaa kuona kwamba walitumia Biblia ili kujibu kila ulizo! Mara moja nilikubali funzo la Biblia.

Kwanza, nilikuwa ninapenda tu kujua mambo mengi. Lakini mambo yalibadilika wakati mimi na bwana yangu tulianza kuenda kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova katika Jumba la Ufalme. Wakati huo, tulikuwa na watoto wawili. Mashahidi wa Yehova walituonyesha upendo, walikuwa wanakuja kutuchukua ili tuende pamoja kwenye mikutano na walikuwa wanatusaidia kuhangaikia watoto wakati wa mikutano. Nilifikia kufurahia Mashahidi wa Yehova.

Hata hivyo, niliendelea kuwa na mashaka fulani. Niliamua kutembelea familia yangu katika inchi ya Hispania. Baba yangu mudogo, aliyekuwa padri, alijaribu kunivunja moyo niache kujifunza Biblia. Lakini Mashahidi wa Yehova wa huko walinisaidia sana. Walijibu maulizo yangu kwa kutumia Biblia, kama tu Mashahidi wa Yehova wa Ujerumani walivyofanya. Niliamua kwamba nitaanza tena kujifunza Biblia wakati nitarudia Ujerumani. Hata ikiwa bwana yangu aliacha kujifunza Biblia, mimi nilianza tena kujifunza na nikaendelea. Katika mwaka wa 1978, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA:

Ujuzi wa kweli wa Biblia umenisaidia kujua waziwazi kusudi la maisha na kupata muongozo muzuri katika maisha. Kwa mufano, andiko la 1 Petro 3:1-4 linatia wanawake moyo ‘wajitiishe’ kwa bwana zao “pamoja na heshima kubwa” na waonyeshe ‘roho ya utulivu na ya upole, ambayo ni ya samani kubwa machoni pa Mungu.’ Kanuni kama hizo zimenisaidia kuwa bibi na mama muzuri.

Miaka 35 hivi imepita tangu nimekuwa Shahidi wa Yehova. Ninafurahi kumutumikia Mungu nikiwa katika familia ya duniani pote ya ndugu na dada, na ninafurahi sana sababu watoto ine kati ya watoto wangu tano wanamutumikia pia Mungu.