Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA CHA GAZETI: JE, UNAPASWA KUOGOPA MWISHO WA DUNIA?

Mwisho wa Dunia​—Je, Ni Jambo Lenye Kuogopesha, Kuvutia, ao Kuvunja Moyo?

Mwisho wa Dunia​—Je, Ni Jambo Lenye Kuogopesha, Kuvutia, ao Kuvunja Moyo?

Unajisikia namna gani juu ya tarehe 21 Mwezi wa 12, 2012, tarehe ya kalendari ya Wamaya ambayo watu wengi wanasema kwamba kutakuwa badiliko duniani pote? Iwe ulitazamia jambo gani juu ya tarehe hiyo, unaweza kutulizwa, kuvunjika moyo, ao kutojali. Je, huo utakuwa uongo mwengine wa kutabiri mwisho wa dunia?

Tuseme nini juu ya “mwisho wa dunia” unaozungumuziwa katika Biblia? (Mathayo 24:3La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo) Watu fulani wanaogopa kuwa dunia itaunguzwa. Wengine wanavutiwa na yale yatakayotokea wakati mwisho wa dunia utafika. Wengine wengi wamechoshwa na wazo la kusema mwisho umekaribia. Lakini je, mwisho wa dunia ni habari ya kweli ao ya kuwazia tu?

Labda utashangaa kujua mambo ambayo Biblia inafundisha kabisa juu ya mwisho wa dunia. Biblia haionyeshe tu sababu za kutazamia mwisho wa dunia lakini pia inaeleza kwamba watu fulani wanaweza kuvunjika moyo kwa kuona kwamba mwisho unakawia sana. Tunakutia moyo uchunguze majibu ya Biblia kwa maulizo ambayo watu wengi wanajiuliza juu ya mwisho wa dunia.

Je, dunia itaunguzwa kwa moto?

JIBU LA BIBLIA: ‘Mungu ameiwekea dunia musingi juu ya mahali pake palipofanywa imara; haitatikiswa mupaka wakati usio na kipimo, ao milele.’​—ZABURI 104:5.

Dunia haitaharibiwa kwa moto wala kwa njia nyingine yoyote. Lakini Biblia inafundisha kama watu watakaa katika dunia hii milele. Andiko la Zaburi 37:29 linasema hivi: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”​—Zaburi 115:16; Isaya 45:18.

Kisha Mungu kuumba dunia, alisema kwamba ‘ilikuwa njema,’ na anaendelea kuiona hivyo. (Mwanzo 1:31) Mungu hakusudie kuiharibu dunia, lakini anaahidi “kuwaharibu wale wanaoiharibu dunia,” na kuilinda ili isiharibiwe milele.​—Ufunuo 11:18.

Hata hivyo, unaweza kujiuliza juu ya andiko la 2 Petro 3:7. Andiko hilo linasema hivi: “Mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto.” Je, andiko hilo linaonyesha kuwa dunia itaunguzwa kwa moto? Kwa kweli, nyakati fulani Biblia inatumia maneno “mbingu,” “dunia,” na “moto” kwa njia ya mufano. Kwa mufano, wakati andiko la Mwanzo 11:1 linaposema kama ‘dunia yote iliendelea kuwa na luga moja,’ inatumia neno “dunia” ili kumaanisha watu.

Mistari inayozunguka andiko la 2 Petro 3:7 inaonyesha kama maneno mbingu, dunia, na moto yanayotajwa katika andiko hilo yanatumiwa pia kwa njia ya mufano. Mustari wa 5 na wa 6 unalinganisha uharibifu unaokuja wa dunia hii na Garika ya siku za Noa. Wakati huo, dunia ya zamani iliharibiwa, lakini dunia yetu, ni kusema udongo, haikuharibiwa. Hata hivyo, Garika ilifagilia mbali “dunia,” ni kusema, watu waovu. (Mwanzo 6:11) Garika iliharibu pia “mbingu,” ni kusema, viongozi waliotawala watu hao waovu. Vivyo hivyo, andiko la 2 Petro 3:7 linatabiri uharibifu wa milele, kama vile kwa moto, wa watu waovu na serikali zao mbaya.

Mwisho wa dunia ni nini?

JIBU LA BIBLIA: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”​—1 YOHANA 2:17.

“Ulimwengu” unaozungumuziwa katika andiko hilo ambao utapitilia mbali si dunia, lakini ni watu wote wa ulimwengu ambao hawaishi kupatana na mapenzi ya Mungu. Kama vile tu muganga anayepasua watu anaweza kuondoa kivimba cha kansere ili kuokoa uzima wa mugonjwa, Mungu pia atawaharibu watu waovu ili watu wazuri wafurahie kabisa maisha duniani. (Zaburi 37:9) Katika maana hiyo, tunaweza kusema kama “mwisho wa dunia” ni jambo nzuri.

Tafsiri za Biblia ambazo zinatumia maneno kama vile ‘umalizio wa mufumo wa mambo’ ao “mwisho wa nyakati” zinatoa wazo nzuri juu ya “mwisho wa dunia.” (Mathayo 24:3; Biblia Habari Njema) Kwa sababu ni watu waovu tu ndio wataharibiwa, kutakuwa watu wazuri ambao wataendelea kuishi duniani na kuwa na maisha tofauti kabisa, sivyo? Jibu la Biblia ni ndiyo, kwa sababu inatumia maneno ‘mufumo wa mambo unaokuja.’​—Luka 18:30.

Yesu aliita wakati huo unaokuja “kutengenezwa upya [kwa] ulimwengu.” Wakati huo, Yesu atarudishia wanadamu hali ambazo Mungu alikusudia wawe nazo hapo mwanzoni. (Mathayo 19:28Verbum Bible) Tutafurahia mambo yanayofuata:

  •  

  •  

  •  

  •  

  •  

Ikiwa tunafanya “mapenzi ya Mungu,” ni kusema, yale ambayo anatuomba tufanye, hatutaogopa mwisho wa dunia. Lakini tunaweza kuungojea kwa hamu.

Je, kweli mwisho wa dunia unakaribia?

JIBU LA BIBLIA: ‘Wakati munapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba ufalme wa Mungu uko karibu.’​—LUKA 21:31.

Katika kitabu chake (The Last Days Are Here Again), Profesere Richard Kyle anaandika kwamba “mabadiliko ya pasipo kutazamia na muvurugo katika jamii, yote hayo yanatokeza hali nzuri za kutabiri mambo mbalimbali juu ya mwisho wa dunia.” Inakuwa hivyo zaidi sana wakati ni vigumu kueleza sababu ya muvurugo na mabadiliko hayo.

Hata hivyo, manabii wa Biblia ambao walisema juu ya mwisho wa dunia, hawakufanya hivyo ili kueleza hali mbaya ambazo zilikuwa wakati wao. Lakini waliongozwa na roho ya Mungu ili kueleza hali ambazo zingeonyesha kwamba mwisho wa dunia unakaribia sana. Ona unabii fulani kati ya unabii huo na uamue ikiwa unatimizwa wakati wetu.

  •  

  •  

  •  

  •  

  •  

  •  

Kama Yesu alivyosema, tunapoona “mambo yote hayo” tunajua kwamba mwisho wa dunia unakaribia. (Mathayo 24:33) Mashahidi wa Yehova wanaamini kama alama hizo ni zenye kusadikisha, na katika inchi 236, wanahubiria watu wengine mambo wanayoamini.

Je, matazamio yasiyo ya kweli juu ya mwisho wa dunia yanaonyesha kama mwisho huo hautakuja tena?

JIBU LA BIBLIA: ‘Wakati watakapokuwa wakisema: Amani na usalama! ndipo uharibifu wa gafula utakapokuwa juu yao mara moja kama vile maumivu ya taabu juu ya mwanamuke mwenye mimba; nao hawataponyoka hata kidogo.’​—1 WATHESALONIKE 5:3.

Biblia inafananisha uharibifu wa dunia na mwanzo wa maumivu ya kuzaa; mama mwenye mimba hawezi kuepuka maumivu hayo na yanakuja bila kutazamiwa. Wakati unaoongoza kwenye mwisho wa dunia unafananishwa pia na mimba, kwa sababu mama anayetazamia kuzaa anajua kwamba maumivu yanapoongezeka ni alama ya kuwa anakaribia kuzaa. Muganga wa mama huyo anaweza kukadiria tarehe ya kuzaa; lakini hata ikiwa anakawia kuzaa, mama huyo ataendelea kuwa na uhakika kama mutoto atazaliwa karibuni. Vivyo hivyo, matazamio yoyote yasiyo ya kweli juu ya mwisho wa dunia hayabadilishe alama zinazoonyesha kuwa hizi ni “siku za mwisho.”​—2 Timotheo 3:1.

Unaweza kujiuliza, ‘Ikiwa alama zinazoonyesha kwamba mwisho unakaribia ziko wazi, sababu gani watu wengi sana hawazitambue?’ Biblia inaonyesha kwamba wakati mwisho utakaribia, watu wengi watapuuza alama zilizo wazi. Watu hao hawangeamini kama hali za ulimwengu zinaharibika na kama tunaishi katika siku za mwisho. Lakini wangewazihaki wale wanaoamini hivyo kwa kusema: “Tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji.” (2 Petro 3:3, 4) Kwa maneno mengine, alama za siku za mwisho zinaonekana wazi, lakini watu wengi wanazipuuza.​—Mathayo 24:38, 39.

Habari hii imezungumuzia tu maandiko fulani yanayoonyesha kwamba mwisho wa dunia unakaribia. * Je, ungependa kujua mambo mengi zaidi juu ya mwisho wa dunia? Ikiwa jibu ni ndiyo, tunakutia moyo uwatafute Mashahidi wa Yehova na ukubali kujifunza nao Biblia bila malipo. Unaweza kujifunza nyumbani kwako, mahali pengine panapokufaa, ao hata kupitia telefone. Jambo moja tu ambalo unaombwa kutoa ni wakati wako, na faida ambazo utapata haziwezi kulinganishwa na kitu chochote.

^ Ili kupata habari zingine, soma sura ya 9 yenye kichwa, “Tunaishi Kweli Katika ‘Siku za Mwisho’?,” ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.