Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

“Mwanamuke” mwenye kuzungumuziwa mu Isaya 60:1 ni nani, na namna gani ‘anasimama’ na ‘kutoa mwangaza’?

Isaya 60:1 inasema hivi: “Simama, Ee mwanamuke, toa mwangaza, kwa maana mwangaza wako umekuja. Utukufu wa Yehova unakuangazia.” Mu mistari yenye inafuata ile andiko, ule “mwanamuke” ni Sayuni ao Yerusalemu, yenye ilikuwa muji mukubwa wa Yuda ile wakati. (Isa. 60:14; 62:1, 2) Ule muji uliwakilisha taifa yote. Maneno ya Isaya inatokeza hii maulizo mbili: Kwanza, ni wakati gani na namna gani Yerusalemu ‘ilisimama’ na kutoa mwangaza wa kiroho? Pili, maneno ya Isaya iko na utimizo mukubwa wakati wetu?

Ni wakati gani na namna gani Yerusalemu ‘ilisimama’ na kutoa mwangaza wa kiroho? Yerusalemu na hekalu yake vilibakia mabomoko kwa miaka 70 yenye Wayahudi walikuwa mu uhamisho Babiloni. Lakini kisha Wamedi na Waajemi kushinda Wababiloni, Waisraeli wote wenye walikuwa mu utawala wote wa Babiloni walikuwa huru kurudia kwao na kurudisha ibada safi. (Ezr. 1:1-4) Kuanzia mwaka wa 537 M.K.Y., mabaki waaminifu kutoka makabila yote 12 walirudia. (Isa. 60:4) Walianza kumutolea Yehova zabihu, kufanya sikukuu mbalimbali, na kujenga tena hekalu. (Ezr. 3:1-4, 7-11; 6:16-22) Kwa mara ingine tena, utukufu wa Yehova ulianza kuangaza Yerusalemu, ni kusema utukufu wa Mungu ulianza kuangazia tena watu wake. Kisha, wao pia wakakuwa mwangaza kwa ajili ya mataifa yenye ilikuwa mu giza ya kiroho.

Lakini, maunabii mbalimbali yenye Isaya alitoa ilitimia kwa sehemu tu ile wakati. Kwa ujumla, Waisraeli hawakuendelea kumutii Mungu. (Ne. 13:27; Mal. 1:6-8; 2:13, 14; Mt. 15:7-9) Kisha wakati, walifikia hata kumukataa Masiya, Yesu Kristo. (Mt. 27:1, 2) Mu mwaka wa 70 K.K.Y., Yerusalemu na hekalu yake viliharibiwa kwa mara ya pili.

Yehova alikuwa alishatabiri kama ile mambo itatokea. (Da. 9:24-27) Ni wazi kama haikuwa kusudi yake Yerusalemu ya ku dunia itimize sehemu zote za unabii kuhusu kurudishwa, zenye kuwa mu Isaya sura ya 60.

Maneno ya Isaya iko na utimizo mukubwa wakati wetu? Ndiyo, lakini iko inatimia juu ya mwanamuke mwingine wa mufano, ni kusema, “Yerusalemu la juu.” Mutume Paulo aliandika hivi juu yake: “Hilo ni mama yetu.” (Gal. 4:26) Yerusalemu la juu ni sehemu ya mbinguni ya tengenezo ya Mungu, yenye kufanyizwa na viumbe wake waaminifu wa roho. Watoto wake ni Yesu na Wakristo watiwa-mafuta 144000 wenye, kama Paulo, wako na tumaini ya kuishi mbinguni. Watiwa-mafuta wanafanyiza “taifa takatifu,” ni kusema “Israeli wa Mungu.”—1 Pe. 2:9; Gal. 6:16.

Namna gani ule mwanamuke, ao Yerusalemu la juu, ‘alisimama’ na ‘kutoa mwangaza’? Alifanya vile kupitia watoto wake watiwa-mafuta wa ku dunia. Linganisha mambo yenye iliwafikia na mambo yenye kuzungumuziwa mu Isaya 60.

Wakristo watiwa-mafuta walipaswa ‘kusimama’ juu walikuwa wameingia mu giza ya kiroho wakati uasi-imani ulienea mu kutaniko ya Kikristo mu karne ya 2, sawa vile ilikuwa imetabiriwa. (Mt. 13:37-43) Ile wakati walifikia kuwa watumwa wa Babiloni mukubwa, ni kusema dini ya uongo. Watiwa-mafuta walibakia mu utumwa mupaka “umalizio wa mupangilio wa mambo,” wenye ulianza mwaka wa 1914. (Mt. 13:39, 40) Muda mufupi kisha pale, mu mwaka wa 1919 waliachiliwa huru, na bila kukawia wakaanza kutoa mwangaza wa kiroho kwa kufanya kwa bidii kazi ya kuhubiri. a Kwa miaka mingi watu kutoka mataifa yote wamepata ule mwangaza, kutia ndani mabaki wa Israeli ya Mungu, “wafalme” wenye kuzungumuziwa mu Isaya 60:3.—Ufu. 5:9, 10.

Wakati wenye kuya, Wakristo watiwa-mafuta watatoa mwangaza wa Mungu mu njia yenye kuwa kubwa zaidi. Namna gani? Wakati wanafikia mwisho wa maisha yao ku dunia, wanakuwa sehemu ya “Yerusalemu Mupya,” ao bibi-arusi wa Kristo, ni kusema wale 144000 wenye watatawala naye wakiwa wafalme na makuhani.—Ufu. 14:1; 21:1, 2, 24; 22:3-5.

Yerusalemu mupya itahusika sana mu utimizo wa Isaya 60:1. (Linganisha Isaya 60:1, 3, 5, 11, 19, 20 na Ufunuo 21:2, 9-11, 22-26.) Sawa vile Yerusalemu ya zamani njo kulikuwa serikali ya Israeli ya zamani, Yerusalemu mupya na Kristo njo itakuwa serikali ya mupangilio mupya wa mambo. Namna gani Yerusalemu mupya inashuka “kutoka mbinguni kwa Mungu”? Kwa kutenda kwa ajili ya dunia. Watu wenye kumuogopa Mungu kutoka mataifa yote ‘watatembea kupitia mwangaza wake.’ Na hata watawekwa huru kutoka katika zambi na kifo. (Ufu. 21:3, 4, 24) Matokeo itakuwa “kurudishwa kwa mambo yote,” sawa vile Isaya na manabii wengine walitabiri. (Mdo. 3:21) Ile kazi kubwa ya kurudisha mambo yote ilianza wakati Kristo aliwekwa kuwa Mufalme na itaisha ku mwisho wa Utawala wake wa Miaka Elfu.

a Kurudishwa kwa ibada safi yenye ilifanyika mu 1919 inazungumuziwa pia mu Ezekieli 37:1-14 na mu Ufunuo 11:7-12. Ezekieli alitabiri kama Wakristo wote watiwa-mafuta wangerudishwa kisha kufanya muda murefu mu utumwa. Unabii wenye kuwa mu Ufunuo ulitabiri kama kikundi kidogo ya ndugu watiwa-mafuta wenye waliongoza wangezaliwa upya mu njia ya mufano kisha kulazimishwa kwa muda mufupi kuacha kazi, juu walikuwa wamefungwa bila sababu. Mu 1919, waliwekwa kuwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.”— Mt. 24:45; ona kitabu Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!, uku. 118.