Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kuzoea Kutaniko ya Mupya

Namna ya Kuzoea Kutaniko ya Mupya

ULISHAKAHAMIA mu kutaniko ya mupya? Kama ni vile, pengine unakubaliana na hii maneno ya Jean-Charles: “Ni nguvu kujipatanisha na kutaniko ya mupya na wakati uleule kuendelea kusaidia kila mutu mu familia aendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho.” Zaidi ya kutafuta kazi, fasi ya kuishi, na pengine masomo, wale wenye wanahamia fasi ingine wanapambana na magumu ya kujipatanisha na hali ya hewa, desturi ya mupya, na eneo ya mupya ya kuhubiria.

Nicolas na Céline walipambana na tatizo ingine. Walikubali mugao wenye tawi ya Ufaransa iliwapatia wa kuhamia mu kutaniko ingine. Wanasema hivi: “Ku mwanzo tulifurahi sana, kisha hali ikakuwa nguvu juu tulikumbuka sana marafiki wetu. Tulikuwa hatuyazoeana sana na ndugu na dada wa mu kutaniko yetu ya mupya.” a Kisha kufikiria ile magumu yote, unaweza kufanya nini ili uzoee kutaniko ya mupya? Wengine wanaweza kusaidia namna gani? Utapata baraka gani? Na namna gani weye pia utasaidia kutaniko yako ya mupya?

KANUNI INE ZENYE ZINAWEZA KUKUSAIDIA

Umutegemee Yehova

1. Umutegemee Yehova. (Zb. 37:5) Kazumi, dada fulani wa Japani, alikuwa mu kutaniko fulani kwa miaka 20. Alilazimika kuhama kutaniko wakati kazi iliomba bwana yake atumikie fasi ingine. Namna gani ‘alitia njia yake katika mukono wa Yehova’? Anasema hivi: “Nilimufungulia Yehova moyo wangu kuhusu mambo yenye ilikuwa naniogopesha, nilimuambia namna nilikuwa najisikia kuwa peke yangu, na mahangaiko yote yenye nilikuwa nayo. Kila wakati yenye nilifanya vile, alinipatia nguvu yenye nilikuwa nayo lazima.”

Unaweza kufanya nini juu umutegemee Yehova zaidi? Sawa vile muti unakuwaka na lazima ya maji na udongo wenye mboleo ili kuota, imani yetu iko na lazima ya kulishwa ili ikomae. Nicolas, mwenye tulizungumuzia, aliona kama kutafakari juu ya mifano ya wanaume wenye walijitoa sana ili kufanya mapenzi ya Mungu sawa vile Abrahamu, Yesu, na Paulo, kulimusaidia akuwe hakika zaidi kama Yehova atamutegemeza. Kujifunza Biblia kwa ukawaida kutakusaidia upambane na mabadiliko yoyote, na kutakusaidia pia ujue namna ya kutia wengine moyo mu kutaniko yako ya mupya.

Epuka kulinganisha

2. Epuka kulinganisha. (Muh. 7:10) Wakati Jules alitoka Benin na kuhamia Amerika, aliona kama kulikuwa tofauti kubwa sana kati ya desturi ya zile inchi. Anasema hivi: “Nilisikia sawa vile nilipaswa kuelezea kila mutu mwenye nilikutana naye maisha yangu.” Kwa sababu mambo ilikuwa tofauti na mambo yenye alizoea, alianza kujitenga na kutaniko. Lakini kisha kujua ndugu na dada muzuri, alibadilisha mawazo yake. Anasema hivi: “Ninaamini kama ikuwe tunaishi wapi ku dunia, siye wote tuko sawa. Namna yetu ya kutenda na kuzungumuza njo tu iko tofauti. Ni jambo ya lazima kukubali watu vile wako.” Kwa hiyo epuka kulinganisha kutaniko yako ya zamani na kutaniko yako ya mupya. Anne-Lise, dada fulani painia anasema hivi: “Sikuhama juu nikutane tena na mambo yenye niliacha nyuma. Nilihama juu nivumbue mambo ya mupya.”

Wazee pia wanapaswa kujikaza kuepuka kulinganisha kutaniko yao ya zamani na kutaniko yao ya mupya. Juu watu wanafanya mambo mu namna tofauti, ile haimaanishe kama namna yao ya kufanya mambo haiko muzuri. Ni jambo ya hekima kujua kwanza hali ya eneo mbele ya kuleta mapendekezo. (Muh. 3:1, 7b) Ni muzuri zaidi kuongoza kupitia mufano wetu kuliko kulazimisha wengine mu kutaniko wafuate mawazo yetu.—2 Ko. 1:24.

Ukuwe na mambo mingi ya kufanya

3. Ukuwe na mambo mingi ya kufanya. (Flp. 1:27) Kuhama kunaombaka wakati mingi na nguvu mingi. Lakini ni jambo ya maana tuanze kuhuzuria mikutano ku Jumba ya Ufalme wakati tu tunafika. Kama ndugu na dada wa mu kutaniko yako ya mupya hawayakuonaka ao wanakuonaka tu mara moya-moya, namna gani wanaweza kukutegemeza? Lucinda na watoto wake wanamuke wawili walihamia mu muji mukubwa katika Afrika ya Kusini. Lucinda anasema hivi: “Walinishauria nikuwe na bidii mu kutaniko, nihubiri pamoya na wengine, na kujibia wakati wa mikutano. Tulitoa pia nyumba yetu itumiwe kwa ajili ya mukutano wa mahubiri.”

“Kukazana pamoja” ao kufanya mambo ya kiroho pamoya na ndugu na dada wa mu kutaniko yako ya mupya ni njia ya muzuri ya kuchangia “imani ya habari njema.” Wazee walimutia moyo Anne-Lise, mwenye tulizungumuzia, ajikaze kuhubiri na kila mutu. Matokeo ilikuwa nini? Anne-Lise anasema hivi: “Bila kukawia nilitambua kama kufanya vile njo kunasadia mutu azoee kabisa kutaniko.” Pia, kujitoa ili kusaidia katika mambo mbalimbali sawa vile kusafisha Jumba ya Ufalme, kunaonyesha kama unaona ile kutaniko ya mupya kuwa kutaniko yako. Kama unajikaza kufanya mambo mingi, bila kukawia ndugu na dada watakuzoea na utajisikia kuwa mu familia ya kiroho.

Tafuta marafiki wapya

4. Tafuta marafiki wa mupya. (2 Ko. 6:11-13) Kuhangaikia wengine ni njia ya muzuri zaidi ya kupata marafiki. Kwa hiyo mbele na kisha mikutano, ukuwe nazungumuza na ndugu na dada ili uwajue muzuri. Ujikaze kujua majina yao. Kukumbuka majina yao na kuwa muchangamufu kutafanya wengine wakukaribie na kutakusaidia kupata marafiki wapya.

Kuliko kuwa na wasiwasi ikiwa wengine watakukubali, acha ndugu na dada wakujue vile uko kabisa. Fanya sawa vile dada Lucinda alifanya, anasema hivi: “Leo tuko na marafiki wa karibu kwa sababu tulikamata hatua ya kualika wengine kwetu.”

“MUKARIBISHANE”

Haikuwake mwepesi kwa watu fulani kuingia mu Jumba ya Ufalme yenye kujaa watu wenye hawajue. Sasa tunaweza kufanya nini ili kusaidia wapya? Mutume Paulo anatutia moyo hivi: “Mukaribishane, kama vile Kristo pia aliwakaribisha ninyi.” (Ro. 15:7) Wazee wanaweza kuiga mufano wa Kristo kwa kusaidia wapya wajisikie kuwa wamekaribishwa. (Ona kisanduku “ Mambo Yenye Inaweza Kusaidia Wakati Mutu Anahama Kutaniko.”) Lakini, watu wote mu kutaniko, hata watoto, wanaweza kusaidia kukaribisha wapya.

Njia moya ya kukaribisha wengine ni kuwaonyesha ukarimu lakini pia kuwatolea musaada wenye wako nao lazima. Kwa mufano, dada fulani alijitoa ili kuonyesha dada wa mupya fasi mbalimbali mu muji na namna ya kukamata bisi ao train. Jambo yenye ule dada alifanya iligusa sana ule dada wa mupya na ilimusaidia azoee eneo ya mupya.

NAFASI YA KUKOMAA KIROHO

Wakati nzige iko nakomala, inatoshaka ngozi yake mara mingi mbele mabawa yake ikuwe na uwezo wa kuruka. Vilevile, wakati unahamia mu kutaniko ya mupya, unapaswa kuachana na mambo yote yenye inaweza kukuzuia kuendelea mbele mu kazi ya Yehova. Nicolas na Céline wanasema hivi: “Kuhama ni njia ya muzuri ya kujizoeza. Juu ya kuzoea watu wapya na fasi yenye kuwa tofauti, inaombaka tukomalishe sifa za mupya zenye hatukukuwa nazo.” Jean-Charles, mwenye tulizungumuzia, anaonyesha faida yenye familia yake ilipata. Anasema hivi: “Mabadiliko ilisaidia watoto wetu wafanye maendeleo mu kutaniko ya mupya. Kisha tu miezi fulani, mutoto wetu mwanamuke alipitisha kipindi ku mukutano wa katikati ya juma na mutoto wetu mwanaume akakuwa muhubiri mwenye hayabatizwa.”

Kama hali yako haikuruhusu kuhamia fasi ingine, pengine fasi kwenye kuwa na lazima ya wahubiri, unaweza kufanya nini? Fanya sawa vile kutaniko yako ni ya mupya kwa kutumikisha mapendekezo yenye tumezungumuzia. Umutegemee Yehova, ukuwe na mambo mingi ya kufanya mu kutaniko yako, kwa mufano ufanye mipango ili kuhubiri pamoya na wengine, ujifanyie marafiki wapya, ao utie nguvu uhusiano wako na marafiki wako wa zamani. Unaweza kusaidia wapya ao wenye wako mu uhitaji kwa kuwatolea musaada fulani wenye wako nao lazima? Juu upendo njo unatambulisha Wakristo wa kweli, kufanya vile kutakusaidia uendelee kukomaa kiroho. (Yoh. 13:35) Unaweza kuwa hakika kama “Mungu anapendezwa na zabihu za namna hiyo.”—Ebr. 13:16.

Hata kama kuhamia mu kutaniko ya mupya iko na magumu yake, Wakristo wengi wamepata matokeo ya muzuri; weye pia unaweza kupata matokeo ya muzuri! Anne-Lise anasema hivi: “Kubadilisha kutaniko kulinisaidia kupanuka.” Sasa Kazumi iko hakika kama wakati unahamia mu kutaniko ingine “unaweza kujionea namna Yehova iko nakutegemeza mu njia yenye haukuwazia.” Tuseme nini juu ya Jules? Anasema hivi: “Marafiki wenye nimepata wamenisaidia nijisikie kuwa nyumbani. Sasa naona kuwa kutaniko yangu ya mupya ni familia yangu, na inaweza kuwa nguvu kuiacha.”

a Juu ya kupata mashauri kuhusu “Kukabiliana na Tatizo la Kutamani Nyumbani Katika Utumishi wa Mungu,” ona ile habari mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 1994.