Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Sababu gani Yesu alihukumu tabia ya Wayahudi ya kufanya viapo?

KULINGANA na Sheria ya Musa, kulikuwa wakati wenye ilifaa kuapa. Lakini, watu wa wakati wa Yesu walizoea sana kuapa katika maisha yao ya kila siku, walikuwa wanaapa ili kukazia jambo lolote lenye wanasema. Tendo hilo la kuapa juu ya mambo madogo-madogo, lilikuwa na kusudi la kuonyesha kuwa mutu anasema kweli; lakini Yesu alihukumu mara mbili jambo hilo. Alifundisha hivi: “Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo.”​—Mt. 5:33-37; 23:16-22.

Kitabu Theological Dictionary of the New Testament, kinasema kuwa “zoea la Wayahudi la kupenda kuapa ili kuonyesha kuwa mambo yenye wanasema ni ya kweli,” lilikuwa lenye nguvu sana kama vile inaweza kuonekana katika maandishi ya Talmud, yenye kuonyesha waziwazi ni viapo gani vyenye vilipaswa kuheshimiwa na vyenye vingeweza kuvunjwa.

Haiko Yesu tu ndiye alihukumu tabia hiyo ya mubaya. Kwa mufano, mwanahistoria Muyahudi Flavius Josèphe, alisema kuwa watu wa dini fulani ndogo ya Wayahudi waliepuka kufanya kiapo kwa sababu kufanya hivyo ilikuwa mubaya zaidi kuliko kusema uwongo, kwa sababu walisema kuwa ikiwa mutu anapaswa kufanya kiapo ili kuonyesha kwa wengine kuwa anasema kweli, mutu huyo alipaswa kuwa muongo. Kitabu kimoja cha Wayahudi chenye kuitwa Busara ya Sira, (23:11) kinasema pia hivi: “Mutu mwenye anapaswa kuapa hajue kabisa sheria katika moyo wake.” Kwa hiyo, Yesu alihukumu tabia ya kufanya kiapo juu ya mambo yenye haiko ya maana. Ikiwa tunasema kweli kila wakati, hatutakuwa na lazima ya kufanya kiapo ili kuonyesha kuwa mambo yenye tunasema ni kweli.