Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Manyoya ya Fisi-Maji wa Bahari

Manyoya ya Fisi-Maji wa Bahari

WANYAMA wengi wenye kunyonyesha ambao wanaishi katika maji ya baridi wako na mafuta mengi kwenye ngozi yao yenye yanawasaidia kuendelea kuwa na joto katika mwili wao. Fisi-maji wa bahari anategemea njia ingine ya kuchunga joto: Anafunikwa na manyoya mengi.

Fikiria jambo hili: Manyoya ya fisi-maji wa bahari ni yenye kubanana sana kuliko manyoya ya munyama mwingine mwenye kunyonyesha. Kwenye kila sentimetre moja ya muraba (cm2) kuna karibu manyoya 155 000. Wakati fisi-maji anaogelea, manyoya yake yanachukua hewa yenye kuwa karibu na mwili wake. Hewa hiyo inazuia maji ya baridi yasiguse ngozi ya munyama huyo na kufanya mwili wake usipoteze joto.

Wanasayansi wanaamini kwamba kuna jambo lenye wanaweza kujifunza kupitia manyoya ya fisi-maji wa bahari. Wamejaribu kutengeneza nguo nyingi za manyoya, kwa kutegemea urefu na kubanana kwa manyoya. Wanasayansi wametambua kwamba “kadiri manyoya ni mengi na marefu, sehemu yenye kuwa na manyoya inabaki yenye kukauka ao inazuia maji yasifike kwenye ngozi.” Kwa maneno mengine, fisi-maji wa bahari anaweza kujivunia kabisa manyoya yake.

Wanasayansi wanatumaini kwamba kujifunza manyoya hayo kutawaongoza kutengeneza nguo zenye haziingize maji. Hilo linaweza kufanya watu fulani wajiulize kama haingekuwa muzuri zaidi kwa wale wenye kuogelea katika maji ya baridi kuvaa nguo zenye kuwa na manyoya kama ya fisi-maji wa bahari!

Unawaza namna gani? Manyoya yenye kuchunga joto ya fisi-maji wa bahari yalijitokeza yenyewe? Ao yaliumbwa?