Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Kazi

Kazi

Hata kama Biblia iliandikwa zamani, kanuni zake zinatumika mupaka leo. Mambo yenye Biblia inasema juu ya kazi ni ya maana leo kama vile yalikuwa wakati iliandikwa.

Unapaswa kuwa na mawazo gani juu ya kazi?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

Ili kuchunga kazi yako, ni lazima uitie pa nafasi ya kwanza katika maisha. Mawazo hayo yamefanya watu fulani wajitoe sana juu ya kazi yao na hilo limefanya wakose kuhangaikia familia na afya yao.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inafundisha kama tunapaswa kuwa na usawaziko juu ya kazi. Inatutia moyo tufanye kazi kwa bidii na inakataza uvivu. (Methali 6:6-11; 13:4) Lakini Biblia haituambie tutumie wakati na nguvu yetu yote katika kazi. Inatutia moyo tutumie wakati wa kadiri ili kujifurahisha. Andiko la Mhubiri 4:6 linasema hivi: ‘Konzi moja ya pumuziko [kupumuzika kidogo] ni afazali kuliko konzi mbili za kazi [kazi nyingi] ngumu na kufuatilia upepo.’ Kwa hiyo, hatupaswe kujitoa sana katika kazi yetu mupaka itufanye tukose kuhangaikia familia yetu ao afya yetu. Hakuna faida yoyote ya kujitesa sana kwa sababu ya kazi!

‘Kwa mwanadamu hakuna jambo bora [la muzuri] kuliko kwamba akule, akunywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.’Mhubiri 2:24.

Kila kazi ni ya muzuri?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

Ikiwa kazi iko na mushahara muzuri, kazi hiyo ni ya muzuri. Mawazo hayo, pamoja na tamaa ya kupata feza kwa vyepesi, yamechochea watu fulani wajiingize katika biashara za udanganyifu na hata kukubali kazi isiyopatana na sheria ya inchi.

Wengine wanachochewa na mawazo ya kusema kama mutu anapaswa kufanya kazi yenye alipanga kufanya katika maisha ao yenye anapenda. Hilo linafanya wakubali tu kazi yenye inawafanya waendelee kuchangamuka. Ikiwa wanafanya kazi yenye hawakupanga kufanya katika maisha, ao yenye haiwafanye wachangamuke, wanaiona kuwa ni ya kuchokesha. Kwa hiyo, wanakuwa na mawazo mabaya juu ya kazi yao na hawaifanye kwa bidii. Wanaweza hata kukataa kazi ya muzuri kwa sababu wanaona kama haiwastahili.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inakataza kazi yenye kufanya mutu atumie udanganyifu ao atendee wengine mubaya kwa njia yoyote. (Walawi 19:11, 13; Waroma 13:10) Kazi ya muzuri inaletea wengine faida na inasaidia mwenye kuifanya ‘akuwe na zamiri njema.’—1 Petro 3:16.

Tena, Biblia inafundisha kuwa kazi inatimiza mambo ya maana, haiko tu kutimizia mutu kile anapenda, lakini inasaidia mutu kupata mambo yenye iko nayo lazima kabisa, na kutegemeza familia. Hata kama haiko mubaya kufurahia kazi yetu, hatupaswe kuitia pa nafasi ya kwanza katika maisha.

“Baba yangu iko na mambo mengi ya kufanya. Iko na kazi ya kimwili, na iko na mambo mengi ya kufanya katika kutaniko letu la Mashahidi wa Yehova. Lakini baba yangu ni mufanyakazi muzuri. Kila jambo lenye iko na lazima ya kufanya, analifanya, lakini hakose wakati kwa ajili ya mama yangu, dada yangu na mimi. Sikuzote baba yangu iko na mambo ya kufanya, lakini ni mwenye usawaziko.”—Alannah.

Kwa kweli, wakati bei ya vitu inapanda, tunaweza kuwa na mahangaiko juu ya namna tutapata mambo yenye tuko nayo lazima, lakini Biblia inasema kama tunapaswa kuwa na kiasi. Inasema hivi: ‘Tukiwa na chakula na kitu cha kujifunika, tutarizika na vitu hivyo.’ (1 Timotheo 6:8) Maneno hayo hayamaanishe kama tunapaswa kujinyima vitu vingine vya maisha. Lakini tunapaswa kujua ni vitu gani tuko na uwezo wa kununua, na hatupaswe kutafuta vitu vingi kupita mipaka.—Luka 12:15.

NAMNA YA KUTUMIKISHA HABARI HII

Ufanye kazi yako kwa bidii. Uifurahie kabisa. Hata kama kazi yako inaonekana kuwa ya hali ya chini, ao haiko kazi yenye ulipanga kufanya katika maisha, ujikaze kuifanya muzuri. Wakati unafanya kazi kwa bidii, unajisikia kuwa unatimiza jambo fulani, na wakati unaifanya muzuri zaidi, hilo linafanya ikuletee furaha zaidi.

Lakini, ukuwe pia na usawaziko. Mara kwa mara, ukuwe na wakati wa kupumuzika na kujifurahisha. Wakati huo unaleta furaha sana kisha kufanya kazi kwa bidii. Tena, wakati tunapata mambo yenye tuko nayo lazima, hilo linafanya tujiheshimie, na watu wengine watuheshimie, hata watu wa familia yetu.—2 Wathesalonike 3:12.

‘Musihangaike kamwe na kusema, Tutakula nini? ao, Tutakunywa nini? ao, Tutavaa nini? . . . Baba yenu wa mbinguni anajua munahitaji vitu hivi vyote.’Mathayo 6:31, 32.