Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Wakati Uchumba Unaisha

Wakati Uchumba Unaisha

TATIZO

“Niliwaza nilikuwa nimepata mutu mwenye kunistahili. Nilifikiri kuwa ningeishi maisha yangu yote pamoja na kijana huyo. Lakini kisha kufanya uchumba kwa miezi mbili, nililazimika kuachana naye. Sikuamini kuwa uchumba huo wenye ulianza muzuri ungeisha haraka sana!”—Anna. *

“Ilionekana kuwa tulipatana katika mambo mengi. Katika akili yangu, nilikuwa ninaona sawa vile tumekwisha kuoana. Lakini kisha wakati kupita, nilianza kuona kama hatupatane kabisa. Wakati niliona kuwa nilikuwa ninafanya kosa kubwa, niliachana naye.”—Elaine.

Jambo kama hilo limekwisha kukufikia? Ikiwa ni hivyo, habari hii inaweza kukusaidia.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Wakati uchumba unaisha, hilo linaweza kuumiza sana moyoni, hata mutu mwenye alipenda uishe. Kijana mwanamuke anayeitwa Sarah, ambaye aliachana na muchumba wake kisha miezi sita, anasema hivi: “Nilijisikia mubaya sana! Mutu huyo alikuwa katika maisha yangu ya leo na ya wakati unaokuja; kisha alitoka mara moja. Nilikuwa ninasikia nyimbo zenye mimi na yeye tulikuwa tunapenda, na hilo lilikuwa linanikumbusha wakati muzuri tulikuwa tunapitisha pamoja. Nilikuwa ninaenda nafasi zenye mimi na yeye tulifurahia, na nilikuwa ninaumia moyoni kwa sababu sikukuwa tena naye. Mambo hayo yaliniumiza moyoni hata kama ni mimi nilipenda uchumba uishe!”

Kumaliza uchumba kunaumiza moyoni, lakini hilo linaweza kuwa jambo la muzuri. Elaine anasema hivi: “Haupendi kuumiza mwengine moyoni. Lakini unaona kuwa, mwishowe nyinyi wawili mutaumia moyoni ikiwa munaendelea na uchumba wenye kuwa na magumu.” Sarah anakubaliana na maneno hayo. Anasema hivi: “Ninawaza kama ikiwa haufurahie mutu wakati mungali katika uchumba, inawezekana hautamufurahia wakati mutaoana; kwa hiyo, ni muzuri kumaliza uchumba huo.”

Ikiwa uchumba unaisha, haimaanishe kama wewe umeshindwa. Kwa kweli, uchumba muzuri unaongoza kwenye uamuzi fulani, hauongoze kila mara kwenye ndoa. Ikiwa mumoja kati yenu iko na mashaka makubwa, uamuzi muzuri unaweza kuwa kumaliza uchumba. Jambo hilo likitokea, ni uchumba wenu ndio umeshindwa, lakini haimaanishe kama wewe umeshindwa. Unaweza kuendelea na maisha! Namna gani?

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Uitike maumivu yako. Elaine mwenye alitajwa kwenye mwanzo wa habari hii anasema hivi: “Sikupoteza tu rafiki, nilipoteza rafiki yangu wa sana.” Wakati unaachana na rafiki wa namna hiyo, ni kawaida kuwa na huzuni kwa wakati fulani. Kijana mumoja mwenye kuitwa Adam anasema hivi: “Urafiki umeisha, na sikuzote hilo linaleta huzuni fulani, hata kama unajua kuwa huo ulikuwa uamuzi muzuri.” Unaweza kujisikia kama Mufalme Daudi mwenye kuzungumuziwa katika Biblia. Wakati alikuwa katika kipindi cha huzuni, aliandika hivi: “Usiku kucha nafanya kitanda changu kilowane; kwa machozi yangu.” (Zaburi 6:6) Wakati fulani, ni muzuri kuitika maumivu kuliko kujaribu kuyaepuka. Kuitika kuwa unaumia moyoni inaweza kuwa hatua ya kwanza ya kukusaidia ujisikie muzuri.—Kanuni ya Biblia: Zaburi 4:4.

Ufanye urafiki na watu wenye kukuhangaikia. Kwa kweli, inaweza kuwa vigumu kufanya hivyo. Anna, mwenye tumekwisha kutaja anasema hivi: “Mwanzoni sikupenda hata kuona watu. Nilikuwa na lazima ya wakati ili niweze kupona, kufikiri juu ya jambo lenye lilitokea, na kulielewa.” Lakini kisha wakati fulani, Anna aliona kuwa ni jambo la hekima kupitisha wakati pamoja na marafiki wa sana wenye wangeweza kumutia moyo. Anasema tena hivi: “Sasa niko na amani ya akili, na leo sivunjike tena moyo sana kama vile zamani.”—Kanuni ya Biblia: Methali 17:17.

Upate somo kupitia jambo lenye lilitokea. Ujiulize hivi: ‘Jambo lenye lilitokea, linaonyesha kama kuna mambo fulani yenye ninapaswa kufanyia maendeleo? Kuna jambo fulani ninapaswa kuepuka wakati nitapata muchumba mwengine?’ Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Marcia anasema hivi: “Kisha wakati fulani, niliweza kuchunguza muzuri jambo lenye lilitokea. Lakini, nilipaswa kungojea tena mupaka wakati nitaweza kufikiri muzuri bila kuongozwa na mawazo ya moyo wangu.” Adam, mwenye tumekwisha kutaja, anakubaliana na mawazo hayo. Anasema hivi: “Kisha uchumba wetu kuisha, iliomba mwaka muzima ili nijisikie muzuri. Iliomba wakati murefu zaidi ili nipate somo kupitia jambo lenye lilitokea. Jambo lenye lilitokea lilinifundisha mambo mengi juu yangu mwenyewe, juu ya wanawake, na juu ya urafiki. Leo siumie tena sana moyoni juu ya uchumba wetu kuisha.”

Usali juu ya mahangaiko yako. Biblia inasema kama Mungu “anawaponya wenye mioyo iliyovunjika, naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.” (Zaburi 147:3) Yehova hawezi kukuchagulia mutu wa kuoa ao wa kuolewa naye, na hatuwezi kusema ni kosa lake wakati uchumba unaisha, lakini anapenda ukuwe na maisha ya muzuri. Umuelezee waziwazi katika sala namna unajisikia moyoni. —Kanuni ya Biblia: 1 Petro 5:7.

^ fu. 4 Majina yamebadilishwa katika habari hii.