Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuacha Kuweka Kinyongo

Namna ya Kuacha Kuweka Kinyongo

TATIZO

Hauwezi kusahau mambo mabaya ambayo bibi ao bwana yako alisema ao kufanya; utaendelea kukumbuka maneno yake makali na matendo aliyofanya bila kufikiri. Kwa hiyo, kuliko kuendelea kumupenda, unaweza kuanza kumuwekea kinyongo. Labda hauna jambo lingine la kufanya, ila tu kuendelea kuishi na mutu ambaye hakupendi. Kwa hiyo, unamuwekea kinyongo bibi ao bwana yako.

Uwe hakika kwamba mambo yanaweza kubadilika. Kwanza, tuchunguze mambo fulani unayopaswa kujua juu ya kuweka kinyongo.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Kuendelea kuweka kinyongo kunafanya ndoa yako isiendelee mbele vizuri

Kuweka kinyongo kunaweza kuharibu ndoa. Sababu gani? Kwa sababu kunaharibu sifa ambazo zinapaswa kujenga ndoa, kama vile upendo, kutumainiana, na uaminifu. Katika maana fulani, kuweka kinyongo hakutokane na tatizo fulani la ndoa, lakini kuweka kinyongo ni tatizo la ndoa. Ndiyo sababu, Biblia inatoa shauri hili: ‘Uchungu wote wenye uovu na uondolewe mbali kutoka kwenu.’—Waefeso 4:31.

Ikiwa unaweka kinyongo, unajiumiza mwenyewe. Kuweka kinyongo ni sawa na kujipiga kofi na kisha kutazamia mutu mwengine asikie maumivu. Katika kitabu chake, Mark Sichel aliandika hivi: “Pengine mushiriki wa familia ambaye unawekea kinyongo anajisikia muzuri kabisa, anafurahia maisha, na hasumbuliwe hata kidogo na jambo lolote.” (Healing From Family Rifts) Tunajifunza nini? Sichel anasema: “Kuweka kinyongo kunakuumiza sana kuliko mutu ambaye unawekea kinyongo.”

Kuweka kinyongo ni sawa na kujipiga kofi na kisha kutazamia mutu mwengine asikie maumivu

Mutu anaweza kuamua kutoweka kinyongo. Watu fulani wanaweza kushakia jambo hilo. Wanaweza kusema, ‘Bibi ao bwana yangu alinikasirisha.’ Tatizo ni kwamba, mawazo kama hayo yanakufanya ufikirie tu jambo ambalo hauwezi kuzuia, ni kusema, matendo ya mutu mwengine. Biblia inatoa shauri linaloweza kukusaidia. Inasema: ‘Kila mumoja na asibitishe [achunguze] kazi [matendo] yake mwenyewe ni nini.’ (Wagalatia 6:4) Hatuwezi kuzuia mutu fulani kusema ao kutenda mambo fulani, lakini tunaweza kuona ikiwa sisi tutafanya nini kama anasema ao kutenda kwa njia fulani. Haulazimishwe tu kuweka kinyongo.

 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Jizuie. Kwa kweli, ni vyepesi kumulaumu bibi ao bwana yako. Lakini, kumbuka kwamba kuweka kinyongo ao kusamehe ni kupenda kwako. Unaweza kuamua kufuata shauri hili la Biblia: ‘Jua lisitue mukiwa katika hali ya kuchokozeka.’ (Waefeso 4:26) Roho ya kusamehe inakutolea nafasi ya kutatua matatizo ya ndoa ukiwa mwenye kutulizana.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.

Jichunguze muzuri. Biblia inaonyesha kwamba watu fulani ni ‘wenye hasira na wenye muelekeo wa gazabu.’ (Methali 29:22) Je, ni vile uko? Jiulize: ‘Nina muelekeo wa kukasirika? Ninakasirika kwa vyepesi? Kila mara ninatafuta kubishana juu ya mambo madogomadogo?’ Biblia inasema kwamba mutu “anayeendelea kuongea juu ya jambo anawatenganisha watu wanaofahamiana.” (Methali 17:9; Mhubiri 7:9) Inaweza kuwa hivyo pia katika ndoa. Kwa hiyo, ikiwa una muelekeo wa kuweka kinyongo, jiulize, ‘Ninaweza kujikaza ili niwe muvumilivu zaidi kwa bibi ao bwana yangu?’—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.

Chagua jambo la maana. Biblia inasema kwamba kuna “wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:7) Si lazima kuzungumuzia kila jambo linalokuumiza; wakati fulani unaweza tu ‘kusema moyoni mwako, kitandani mwako, na kunyamaza.’ (Zaburi 4:4) Wakati unataka kuzungumuzia jambo fulani lililokuumiza, ngoja mupaka hasira yako ipite. Bibi mumoja anayeitwa Beatriz anasema hivi: “Wakati ninajisikia mwenye kukasirika, ninangoja nitulizane kwanza. Wakati fulani ninatambua baadaye kwamba kosa ambalo walinitendea haliko nzito sana, na hilo linanisaidia nizungumuze kwa heshima.”—Kanuni ya Biblia: Methali 19:11.

Tambua maana ya “kusamehe.” Katika Biblia, neno “kusamehe” linatafsiriwa wakati fulani kutokana na neno la luga ya zamani linalomaanisha kuachilia kitu fulani. Kwa hiyo, kusamehe hakumaanishe kupunguza uzito wa jambo lililokuumiza ao kufanya kama vile halikutendeka, lakini kunamaanisha kuachilia jambo hilo, kwa sababu unatambua kwamba kuweka kinyongo kunaweza kuharibu zaidi afya na ndoa yako kuliko kosa lenyewe.