Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Faida ya Kazi za Nyumbani

Faida ya Kazi za Nyumbani

MAGUMU

Katika familia fulani, wazazi wanatazamia watoto wafanye kazi za nyumbani, na watoto hao wanafanya kazi hizo bila kunungunika. Katika familia zingine, wazazi wamepunguza matazamio yao kuelekea watoto wao. Kufanya hivyo, kunafurahisha watoto. Lakini hilo linafanya uwezo wa watoto wao upunguke pia.

Wachunguzi wanaona kama jambo hilo linaanza kutokea katika inchi za Mangaribi. Katika inchi hizo watoto wanaelekea kuwa watumiaji kuliko kuwa wachangaji. Muzazi mumoja mwenye kuitwa Steven anasema hivi: “Leo, watoto wanaachwa peke yao ili kucheza michezo za video, kupitisha wakati kwenye Internete, na kuangalia televizyo. Ni mambo madogo sana ndio wanatazamiwa kufanya.”

Wewe, unawaza namna gani? Kazi za nyumbani ni za maana kabisa kwa ajili ya kutunza nyumba tu, ao zinasaidia pia mutoto akomae muzuri?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Wazazi fulani wanajizuia kupatia watoto wao kazi za nyumbani, zaidi sana wakati watoto wao wako na mambo mengi ya masomo ya kufanya kisha saa za masomo. Lakini, tufikirie faida ya kazi za nyumbani.

Kazi za nyumbani zinasaidia mutoto akomalishe sifa nzuri. Watoto wenye kufanya kazi za nyumbani wako na uwezekano mukubwa wa kutumika muzuri kwenye masomo, na hilo halishangaze. Kuunga mukono kazi za nyumbani kunafanya mutoto akomalishe sifa nzuri kama vile uhakika na kujizuia; sifa hizo ni za maana ili kujifunza.

Kazi za nyumbani zinatayarisha watoto ili watumikie watu wengine. Watu fulani wametambua kwamba watoto wenye wanatazamiwa kufanya kazi za nyumbani wako na uwezekano mukubwa wa kujitolea kwa ajili ya wengine wakati watakuwa wakubwa. Jambo hilo halitushangaze, kwa sababu kazi za nyumbani zinazoeza watoto watie pa nafasi ya kwanza mahitaji ya wengine kuliko mahitaji yao. Kwa upande mwingine, Steven, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Wakati hakuna kitu chenye kutazamiwa kutoka kwao, watoto wanafikiri kama wanapaswa kutumikiwa, na wanakomaa wakiwa na mawazo yenye hayafae kuhusu mambo yenye watakuwa nayo lazima katika maisha ili kutimiza madaraka na kufanya kazi kwa bidii.”

Kazi za nyumbani zinaunganisha watu wa familia. Kupitia kazi zenye wanafanya nyumbani, watoto wanafikia kutambua kwamba wao ni washiriki wa maana katika familia na pia kwamba wako na daraka la kutimiza kwa ajili ya familia. Watoto wanaweza kukosa kutambua jambo hilo kama wazazi wao wanaona kazi za masomo kuwa za maana sana kuliko kazi za nyumbani. Ujiulize, ‘Kuko faida gani kama mutoto wangu anakuwa na uhusiano na timu la kabumbu lakini anapoteza uhusiano wake pamoja na familia?’

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Anza wakati wangali wadogo. Watu fulani wanasema kwamba wazazi wanapaswa kuanza kupatia watoto wao kazi za nyumbani wakati wanakuwa na miaka tatu. Wengine wanashauria miaka mbili ao hata chini. Wazo ni hili: Watoto wadogo wanapenda kufanya kazi pamoja na wazazi wao na kuwaiga.​—Kanuni ya Biblia: Methali 22:6.

Uwapatie kazi kulingana na uwezo wao. Kwa mufano, mutoto wa miaka tatu anaweza kuokota vitu vya kuchezea, kusafisha kwenye maji yalimwangikia, ao kupanga nguo za kufua. Watoto wakubwa wanaweza kuondoa vumbi, kusafisha motokari, ao hata kupika chakula. Patia mutoto wako kazi kulingana na uwezo wake. Unaweza kushangaa kuona namna mutoto wako anaweza kufurahia kufanya kazi za nyumbani kwa bidii.

Tia kazi za nyumbani pa nafasi ya kwanza. Inaweza kuwa vigumu kufanya hivyo kama kila siku mutoto wako iko na kazi nyingi za masomo. Lakini, kitabu The Price of Privilege kinasema kwamba kuondoa kazi ili mutu aweze kwenye masomo “ni alama ya kutia pa nafasi ya kwanza mambo yenye hayafae.” Kama vile tumekwisha kuonyesha, kazi za nyumbani zinasaidia watoto wakuwe wanafunzi wazuri zaidi. Na mambo yenye wanajifunza yanawatayarisha kwa ajili ya wakati wenye watakuwa na familia yao wenyewe.​—Kanuni ya Biblia: Wafilipi 1:10.

Uhangaikie zaidi kusudi lenye unafuatilia. Mutoto wako anaweza kuchukua wakati murefu ili amalize kazi kuliko namna uliwazia. Unaweza pia kufikiri kwamba kazi hiyo ingekuwa muzuri zaidi kama uliifanya wewe mwenyewe. Wakati jambo kama hilo linatokea, epuka kujitwika wewe mwenyewe kazi hiyo. Kusudi lako haiko kumufanya mutoto wako atimize kazi muzuri kama vile mutu mukubwa, lakini ni kumusaidia ajifunze kutimiza madaraka na kutambua furaha yenye mutu anapata wakati anafanya kazi.​—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 3:22.

Tambua wakati wenye kufaa ili kumupatia feza. Watu fulani wanafikiri kwamba kulipa watoto kwa ajili ya kazi yenye wanafanya kunawafundisha kutimiza madaraka. Wengine wanasema kwamba hilo linafanya watoto wakaze akili yao juu ya jambo lenye wanapokea katika familia kuliko jambo lenye wanachangia katika familia. Wanasema pia kwamba watoto wanaweza kukataa kufanya kazi wakati wako na feza za kutosha; hilo linaonyesha kwamba watoto hao wameanza kupoteza faida ya kazi za nyumbani. Tunajifunza nini? Ni jambo la muzuri sana kama feza zenye unapatia mutoto wako haiko kwa ajili ya kazi fulani yenye alifanya nyumbani.