Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA KUULIZA MAULIZO | GENE HWANG

Mwanasayansi wa Hesabu Anaeleza Imani Yake

Mwanasayansi wa Hesabu Anaeleza Imani Yake

Gene Hwang, mwenye alizaliwa katika mwaka wa 1950 katika muji wa Tainan, inchi ya Taiwan, alikuwa profesa wa hesabu kwenye Masomo ya Juu ya Taifa ya Chung Cheng katika Taiwan. Alikuwa pia profesa kwenye Masomo ya Juu ya Cornell, inchi ya Amerika, kwenye alifundisha na kufanya uchunguzi katika mambo ya uwezekano na takwimu (maelezo ya hesabu ya kufafanua na kulinganisha ukweli wa matukio ao jambo fulani). Kwa miaka mingi, alikuwa kati ya watu wenye waliandikwa sana katika maandishi kuhusu mambo ya takwimu, anaendelea katika mambo hayo mupaka sasa. Wakati alikuwa kijana, aliamini kama uzima ulianza kupitia hatua za mageuzi. Lakini kisha alibadilisha mawazo yake. Gazeti Amuka! lilimuuliza juu ya kazi yake na imani yake ya dini.

Ni mafundisho gani ulifundishwa wakati ulikuwa kijana?

Kwenye masomo, tulifundishwa mageuzi, lakini hakuna mutu alieleza namna uzima ulianza. Wakati wazazi wangu waliamini katika dini ya Tao, nilizoea kusikiliza walimu wao wa dini na niliwauliza maulizo mengi. Lakini sikupata majibu mengi ya kunifurahisha.

Sababu gani uliamua kusoma hesabu?

Wakati nilikuwa kwenye masomo ya musingi, nilipendezwa sana na hesabu. Wakati nilienda kwenye masomo ya juu, niliendelea kupendezwa zaidi na somo za hesabu na uwezekano. Ninaona kuwa uhakikisho mufupi wa hesabu unaweza kuwa wazi na wenye kupendeza.

Namna gani ulifikia kupendezwa na Biblia?

Katika mwaka wa 1978, Jinghuei, bibi yangu, alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, na mara kwa mara nilijiunga nao katika mazungumuzo. Wakati huo, tulikuwa tunaishi katika inchi ya Amerika. Jinghuei alikuwa ametoka tu kupata diploma ya doktora katika fizikia, na nilikuwa ninajifunza mambo ya takwimu kwenye Masomo ya Juu ya Purdue, katika jimbo la Indiana.

Ulikuwa na mawazo gani juu ya Biblia?

Nilipendezwa sana na habari za Biblia juu ya namna dunia ilitayarishwa ili watu waishi juu yake. Tofauti na hadisi za zamani za kutunga, vipindi sita vya uumbaji vyenye kuelezwa katika kitabu cha Mwanzo, hata kama ni katika luga nyepesi, vilionekana kuwa vinapatana na mambo ya kweli. * Lakini, kwa miaka mingi sikupenda kuamini kama kuko Muumbaji.

Sababu gani ilikuwa vigumu kwako kuamini kama kuko Muumbaji?

Kukubali kama kuko Muumbaji kulimaanisha kukataa dini yangu ya kuanzia utoto

Kwa sababu ya mambo yenye yalikuwa katika moyo wangu. Kukubali kama kuko Muumbaji kulimaanisha kukataa dini yangu ya kuanzia utoto, kwa sababu dini ya Tao haifundishe kama kuko Mungu mwenye kuwa mutu wa kweli kabisa, ao Muumbaji.

Lakini mawazo yako yalibadilika. Sababu gani?

Wakati niliendelea kufikiri zaidi juu ya namna uzima ulianza, niliendelea kusadiki kama kiumbe cha kwanza chenye uzima kilipaswa kuwa kigumu sana kueleweka. Kwa mufano, kilipaswa kuwa na uwezo wa kuzaana, jambo lenye kuomba habari za chembe za uriti na uwezo wa kufanya kopi za habari hizo bila kukosea. Tena, hata chembe nyepesi zaidi yenye uzima iko na lazima ya mashini za molekuli ili kujenga sehemu zote za chembe mupya, na pia namna ya kutumia na kuongoza nguvu. Namna gani utendaji huo mbalimbali wenye kuwa mugumu kueleweka ungeweza kutokea bila mupango kutokana na vitu vyenye havina uzima? Kwa sababu niko mwanasayansi wa hesabu, singeitika wazo hilo. Hilo halingewezekana kabisa kupitia hatua zenye hazina mupango.

Ni nini kilikuchochea uchunguze kwa uangalifu mafundisho ya Mashahidi wa Yehova?

Nilikuwa nimejifunza na Mashahidi wa Yehova mara kwa mara. Kisha, katika mwaka wa 1995, wakati nilitembelea Taiwan, niligonjwa na nikakuwa na lazima ya musaada. Bibi yangu mwenye alibakia katika inchi ya Amerika, aliita Mashahidi wa Yehova wa Taiwan. Walinikuta mwenye kuchoka sana inje ya hospitali moja kwenye sikupata kitanda. Shahidi mumoja alinibeba kwenye hoteli ili nipumuzike. Aliendelea kunihangaikia na kisha akanibeba kwenye hospitali ingine ili nipate matunzo.

Kunihangaikia hivyo kulinigusa moyo sana, na nilifikiria namna Mashahidi wa Yehova walikuwa wameonyesha familia yangu wema mara nyingi. Imani ya Mashahidi wa Yehova iliwafanya wakuwe tofauti na watu wengine. Kwa hiyo, nilianza tena kujifunza nao Biblia. Nilibatizwa mwaka wenye ulifuata.

Imani yako inapingana na mambo ulijifunza kwenye masomo?

Hapana kabisa! Katika miaka ya hivi karibuni nimetoa musaada wa hesabu kwa wanasayansi wenye kujifunza namna chembe za uriti zinafanya kazi. Kujifunza chembe za uriti kunasaidia kuelewa uzima, na ujuzi huo unanifanya nishangazwe sana na hekima ya Muumbaji.

Toa mufano wa hekima hiyo.

Wazia uwezo wa kuzaana wa viumbe. Viumbe fulani, kama vile amiba, havina amiba wa kiume na wa kike. Mikrobe hiyo yenye chembe moja inafanya tu kopi ya habari zenye kuwa katika chembe za uriti na inajigawanya, njia hiyo ya kuzaa inafanywa bila viungo vya uzazi. Lakini, mimea mingi na wanyama wengi wanazaana kwa kutumia viungo vya uzazi, kwa kuchanga habari zenye kuwa katika chembe za uriti za muzazi wa kiume na muzazi wa kike. Sababu gani kuzaana kwa kutumia viungo vya uzazi kunashangaza?

Sababu gani njia ya kuzaana ambamo kiumbe anajigawanya tu katika sehemu mbili na amefanya hivyo muzuri sana, hatujue kwa muda gani, inaweza kugeuka kuwa njia ambamo vitu viwili vinaungana ili kufanyiza kitu kimoja? Utendaji huo wenye kuomba kuchukua nusu ya habari za chembe za uriti kutoka kwa kiumbe wa kiume, na nusu ingine kutoka kwa kiumbe wa kike na kuunganisha habari hizo, uko mugumu sana kueleweka, na hilo linaleta tatizo kubwa sana kwa wanabiolojia wa mageuzi. Mimi ninaona kama njia ya kuzaana kwa kutumia viungo vya uzazi vya kiume na vya kike inaonyesha waziwazi akili ya Mungu.

^ fu. 11 Ili kupata habari zingine juu ya vipindi vya uumbaji, soma broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza kupata broshua hiyo kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com/sw.