Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuonyesha Shukrani

Namna ya Kuonyesha Shukrani

MAGUMU

Ni jambo la lazima kuonyesha shukrani ili kuwa na ndoa yenye furaha. Lakini, watu wengi wenye kufunga ndoa wameacha kutambua sifa za muzuri za bibi ao bwana yao, wanawaonyesha shukrani kidogo tu. Mushauri mumoja mwenye anatajwa katika kitabu fulani, anatambua kwamba bibi na bwana wengi wenye wanakuja kumuona “wanahangaikia sana jambo lenye halifanyike [katika ndoa yao] kuliko kuhangaikia jambo lenye kufanyika. Wanakuja katika biro yangu ili kuniambia kuhusu jambo lenye linapaswa kubadilika, kuliko kuniambia kuhusu jambo lenye linapaswa kubaki namna liko. Kosa lenye bibi na bwana hao wote wanafanya ni kushindwa kuonyesha upendo kupitia shukrani.”—Emotional Infidelity.

Namna gani wewe na bibi ao bwana yako munaweza kuepuka mutego huo?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Kuonyesha shukrani kunaweza kupunguza magumu ya ndoa. Wakati bibi ao bwana anajikaza kuona sifa za muzuri za mwenzake na kumuonyesha shukrani, uhusiano wao unakuwa muzuri zaidi. Hata matatizo makubwa yanaweza kupunguka kama bibi ao bwana anajisikia kwamba mwenzake anamuona kuwa wa maana.

Kwa bibi. Kitabu Emotional Infidelity, chenye tumekwisha kutaja, kinasema hivi: “Mara nyingi, wanawake wengi hawakamate kwa uzito kazi kubwa yenye wanaume wanafanya ili kutimiza mambo yenye watu wa familia zao wako nayo lazima.” Katika maeneo fulani, hilo linaweza kutokea hata katika familia yenye bibi na bwana wanafanya kazi.

Kwa bwana. Mara nyingi, wanaume hawakamate kwa uzito mambo yenye bibi anafanya ili kutegemeza familia, ikuwe kufanya hivyo kupitia kazi, kuchunga watoto, ao kutunza nyumba. Fiona, * mwenye amefanya karibu miaka tatu katika ndoa, anasema hivi: “Sisi wote tunafanya makosa, na wakati ninafanya kosa, ninajisikia mubaya. Kwa hiyo, wakati bwana yangu ananiambia kwamba nilifanya muzuri jambo fulani katika nyumba, ninatambua kwamba anaendelea kunipenda hata kama ninafanya makosa. Tena, ninajisikia kwamba ananitegemeza na hilo linaniletea furaha zaidi!”

Lakini, ikiwa bibi ao bwana anajiona kuwa wa bure, hilo linaweza kufanya ikuwe vigumu kuwa muaminifu katika ndoa. Bibi mumoja mwenye kuitwa Valerie anasema hivi: “Wakati unajisikia kwamba bibi ao bwana yako hakuone kuwa wa maana, ni mwepesi kukaribia mutu mwengine mwenye anakufanya ujisikie kuwa wa maana.”

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ukuwe muangalifu. Katika juma lenye kuja, uangalie sifa nzuri zenye bibi ao bwana yako anaonyesha. Tena, uangalie nini anatimiza ili kufanya mambo yaendeke muzuri katika nyumba, pengine mambo yenye mupaka sasa uliona kuwa ya kawaida. Kwenye mwisho wa juma, ufanye liste ya (1) sifa yenye unafurahia kwa bibi ao bwana yako na (2) mambo yenye alifanya kwa faida ya familia.​—Kanuni ya Biblia: Wafilipi 4:8.

Sababu gani ni jambo la maana kuwa muangalifu? Bibi mumoja mwenye kuitwa Erika anasema hivi: “Miaka fulani kisha kufunga ndoa, unaweza kuanza kuona bibi ao bwana yako kuwa mutu wa kawaida tu. Unaweza kuacha kutambua mambo mazuri yenye bwana yako anafanya na kuanza kukazia akili zaidi mambo yenye hatimize.”

Ujiulize hivi: ‘Ninaona kazi ngumu ya bibi ao bwana yangu kuwa ya kawaida tu?’ Kwa mufano, kama bwana yako anafanya kazi fulani nyumbani, unajizuia kumushukuru kwa sababu unaona kwamba ni daraka lake kutimiza kazi hiyo? Kama uko bwana, unaona kama haistahili kupongeza bibi yako wakati anajikaza kutunza watoto kwa sababu tu hilo ni jambo lenye anatazamiwa kufanya? Ujiwekee mupango wa kutambua na kuonyesha shukrani kwa mambo yote yenye bibi ao bwana yako anafanya, ikuwe makubwa ao madogo, kwa faida ya familia yenu.​—Kanuni ya Biblia: Waroma 12:10.

Uonyeshe shukrani kila mara. Biblia haiseme tu kwamba tunapaswa kuwa wenye shukrani, lakini inasema hivi: ‘Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.’ (Wakolosai 3:15) Kwa hiyo, ujikaze kuwa na tabia ya kushukuru bibi ao bwana yako. Bwana mumoja mwenye kuitwa James anasema hivi: “Wakati bibi yangu anaonyesha shukrani kwa ajili ya mambo yenye ninafanya, hilo linanichochea kutumika zaidi ili kuwa bwana muzuri na kuongeza bidii yangu ya kufanya mengi katika ndoa.”—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 4:6.

Bibi na bwana wenye wanaonyeshana shukrani wanafanya uhusiano wao ukuwe nguvu. Bwana mumoja mwenye kuitwa Michael anasema hivi: “Ninaamini kwamba ndoa nyingi zinaweza kuokoka ikiwa bibi ao bwana anajikaza kukazia akili mambo mazuri yenye mwenzake anafanya. Wakati magumu yanatokea, hawawezi kuamua mara moja kuvunja ndoa yao kwa sababu wanaendelea kukumbuka mambo mazuri yenye wanafanya.”

^ fu. 9 Majina fulani yamebadilishwa.