Ona video zinazopatikana

Namba 666 Maana Yake Nini?

Namba 666 Maana Yake Nini?

Jibu ya Biblia

 Kulingana na kitabu cha mwisho cha Biblia, 666 ni namba, ao jina, ya ule munyama wa pori mwenye kuwa na vichwa saba na pembe kumi mwenye anapanda kutoka katika bahari. (Ufunuo 13:1, 17, 18) Huyu munyama anafananisha viongozi wa serikali (guvernema) za ulimwengu, wenye wanatawala juu ya “kila kabila na watu na luga na taifa.” (Ufunuo 13:7) Jina 666 inaonyesha kama kulingana na Mungu, viongozi wa serikali za ulimwengu wameshindwa kabisa. Namna gani?

  Haiko kibandiko tu. Kwa kawaida, wakati Mungu anapatia mutu ao kitu jina fulani, ile jina iko na maana. Kwa mufano, Mungu alibadilisha jina ya Abramu, yenye kuwa na maana ya “Baba Iko Juu (Ametukuzwa),” kuwa Abrahamu, jina yenye kuwa na maana ya “Baba ya Watu Wengi; Baba ya Wengi),” wakati alitoa ahadi ya kumufanya Abrahamu “kuwa baba ya umati wa mataifa.” (Mwanzo 17:5 maelezo ya chini) Vilevile, Mungu alipatia ule munyama jina 666 kuwa alama ya sifa zenye kumutambulisha.

  Namba 6 inamaanisha kukosa kukamilika. Mara mingi, namba ziko na maana fulani mu Biblia. Namba 7 inamaanisha hali ya kuwa kamili ao ukamilifu. Kwa sababu namba 6 ni namba 7 kupunguza namba moja, inaweza kumaanisha kitu chenye hakiko kamili ao chenye kuwa na makosa mbele ya Mungu, na inaweza kuhusu maadui wa Mungu.​—1 Mambo ya Nyakati 20:6; Danieli 3:1.

  Mara tatu ili kukazia. Wakati fulani Biblia inakazia jambo kwa kuitaja mara tatu. (Ufunuo 4:8; 8:13) Kwa hiyo, jina 666 inakazia kama Mungu anaona serekali za leo zenye wanadamu wanaongoza kuwa zimeshindwa kabisa. Wanadamu wameshindwa kuleta amani na usalama wa kweli, mambo yenye ni Ufalme wa Mungu tu utaleta.

Alama ya ule munyama

 Biblia inasema kama watu wanapata “alama ya ule munyama wa pori” kwa sababu wanamufuata “kwa mushangao,” kufikia hata kumuabudu. (Ufunuo 13:3, 4; 16:2) Wanamuabudu wakati wanatukuza inchi yao, alama za inchi yao, ao uwezo wa jeshi ya inchi yao. Kitabu The Encyclopedia of Religion kinasema hivi: “Kupenda sana inchi imekuwa dini kubwa mu ulimwengu wa leo.” *

 Namna gani mutu anatiwa alama ya ule munyama kwenye mukono na paji la uso wake? (Ufunuo 13:16) Wakati Mungu alipatia taifa ya Israeli amri, alisema hivi: ‘Muzifunge kama kikumbusho kwenye mukono wenu, na zinapaswa kuwa kama utepe wa kichwa kwenye paji la uso wenu.’ (Kumbukumbu la Torati 11:18) Hii maneno haikumaanisha kama Waisraeli walipaswa kutia alama juu ya mikono na paji za uso zao, lakini ilimaanisha kama walipaswa kuacha maneno ya Mungu iongoze matendo na mawazo yao. Vile vile, hata kama namba 666 haipaswe kuonwa kuwa kama alama yenye mutu amejichanja ao kuchorwa, kwa njia ya mufano wale wenye wanaitika serekali za ulimwengu zitawale maisha yao wanatambulishwa kwa alama ya ule munyama. Wale wenye wako na alama ya ule munyama wanamupinga Mungu​—Ufunuo 14:​9, 10; 19:19-​21.

^ Ona pia kitabu Nationalism in a Global Era, ukurasa wa 134, na kitabu Nationalism and the Mind: Essays on Modern Culture, ukurasa wa 94.