Ona video zinazopatikana

Mupinga-Kristo Ni Nani?

Mupinga-Kristo Ni Nani?

Jibu la Biblia

 Mupinga-Kristo haiko mutu mumoja, shirika ao kikundi fulani cha pekee, kwa sababu Biblia inasema kwamba kuna “wapinga-Kristo wengi.” (1 Yohana 2:​18) Neno ‘mupinga-kristo,’ lenye kutoka katika neno la Kigiriki ambalo linamaanisha “zidi (ao badala) ya Kristo,” linahusu watu wote wenye:

 Biblia inaita wapinga-Kristo watu wote wenye kufanya matendo hayo, lakini pia inawaita wote kwa ujumla ‘mupinga-Kristo.’ (2 Yohana 7) Mupinga-Kristo alitokea mara ya kwanza wakati wa mitume na tangu wakati huo anaendelea kufanya kazi. Unabii wa Biblia ulitabiri jambo hilo.​—1 Yohana 4:3.

Namna ya kutambua wapinga-Kristo

  •   Wanaeneza mawazo ya uongo kuhusu Yesu. (Mathayo 24:​9, 11) Kwa mufano, watu wenye wanafundisha Utatu ao wenye kufundisha kwamba Yesu ndiye Mungu Mweza-Yote wanapinga kabisa mafundisho ya Yesu. Yesu alisema hivi: ‘Baba ni mukuu kuliko mimi.’​—Yohana 14:28.

  •   Wapinga-Kristo wanakataa mambo Yesu alisema kuhusu kazi ya Ufalme wa Mungu. Kwa mufano, viongozi fulani wa dini wanasema kwamba Kristo anatenda kupitia serikali ao guvernema za wanadamu. Lakini, hilo linapingana na maneno haya ya Yesu: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”​—Yohana 18:36.

  •   Wanasema kwamba Yesu ni Bwana wao, lakini hawatii amri zake, kutia ndani amri ya kuhubiri habari njema ya Ufalme.​—Mathayo 28:19, 20; Luka 6:​46; Matendo 10:42.