Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini juu ya Kujipodoa na Kuvaa Vitu vya Kujipamba?

Biblia Inasema Nini juu ya Kujipodoa na Kuvaa Vitu vya Kujipamba?

Jibu la Biblia

 Hata kama haitoe maelezo mengi juu ya habari hiyo, Biblia haikataze kujipodoa, kuvaa vitu vya kujipamba ao aina ingine ya kujipamba. Lakini, kuliko kukazia sura ya inje, Biblia inakazia zaidi “vazi lisiloharibika la roho ya utulivu na ya upole.”​—1 Petro 3:​3, 4.

Haiko mubaya kujipamba

  •   Wanawake waaminifu wenye kuzungumuziwa katika Biblia walijipamba. Rebeka, mwenye aliolewa na Isaka mutoto wa Abrahamu, alivaa pete ya zahabu kwenye pua, vikomo vya zahabu, na vitu vingine vya kujipamba vya bei vyenye alipewa kama zawadi kutoka kwa ule mwenye angekuwa baba mukwe wake. (Mwanzo 24:22, 30, 53) Vilevile, Esta alikubali vitu vya kumufanya akuwe na sura na umbo la muzuri zaidi ili kujitayarisha kwa ajili ya daraka kubwa la kuwa malkia ao bibi ya mufalme wa Utawala wa Perse. (Esta 2:​7, 9, 12) Pengine hilo lilitia ndani kutumia “vitu mbalimbali vya kujipodoa.”​—New International Version; Easy-to-Read Version.

  •   Mifano ya Biblia inatumia vitu vya kujipamba ili kulinganisha mambo fulani ya muzuri. Kwa mufano, mutu mwenye kutoa mashauri ya muzuri analinganishwa na ‘pete ya pambo la zahabu . . . kwenye sikio linalosikia.’ (Methali 25:12) Vilevile, Mungu mwenyewe alijilinganisha namna alikuwa anatendea taifa la Israeli na bwana mwenye kupamba bibi yake na vikomo, vitu vya kuvaa kwenye shingo, na vitu vya kuvaa kwenye masikio. Mapambo hayo yalifanya taifa hilo likuwe ‘murembo [ao lenye kupendeza] sana.’​—Ezekieli 16:11-​13.

Mawazo ya uwongo juu ya kujipodoa na kuvaa vitu vya kujipamba

 Mawazo ya uwongo: Kwenye 1 Petro 3:3, Biblia inakataza “kusuka nywele kwa nje na kule kujivika mapambo ya zahabu.”

 Kweli: Maneno yenye kuwa juu na chini ya andiko hilo yanaonyesha kama Biblia inakazia faida ya uzuri wa ndani wenye kuwa tofauti na sura ya muzuri ao mapambo. (1 Petro 3:​3-6) Tofauti hiyo inazungumuziwa pia mahali pengine katika Biblia.​—1 Samweli 16:7; Methali 11:22; 31:30; 1 Timotheo 2:​9, 10.

 Mawazo ya uwongo: Kwa sababu Yezebeli, malkia mubaya sana alikuwa anatia rangi kwenye macho yake, hilo linaonyesha kama kutia rangi kwenye macho ni mubaya.​—2 Wafalme 9:​30.

 Kweli: Yezebeli mwenye alikuwa anafanya ulozi na kuua watu, alihukumiwa kwa sababu ya matendo yake ya mubaya, haiko kwa sababu ya sura yake.​—2 Wafalme 9:​7, 22, 36, 37.