Ona video zinazopatikana

Maneno “Jicho kwa Jicho” Iko na Maana Gani?

Maneno “Jicho kwa Jicho” Iko na Maana Gani?

Jibu ya Biblia

 Sheria yenye ilisema “jicho kwa jicho” ilikuwa moja ya sheria zenye Mungu alipatia taifa la Israeli kupitia Musa. Yesu naye alirudilia ile maneno mu Mahubiri yake Kwenye Mulima. (Matayo 5:38; Kutoka 21:24, 25; Kumbukumbu la Torati 19:21) Ile maneno ilimaanisha kama wakati wa kupatia mukosaji malipizi, ile malipizi ilipaswa kulingana na kosa yenye alifanya. *

 Ile Sheria ilitumiwa wakati mutu fulani alitendea mwingine mubaya kimakusudi. Sheria ya Musa ilisema hivi juu ya ule mutu: “Mufupa wenye ulivunjika kwa mufupa wenye ulivunjika, jicho kwa jicho, jino kwa jino, tendo lilelile la kuumiza lenye alitendea mwenzake ndilo atatendewa.”​—Mambo ya Walawi 24:20

 Ile sheria ya “jicho kwa jicho” ilikuwa na kusudi gani?

 Ile sheria ya “jicho kwa jicho” haikuruhusu mutu ajilipilizie kisasi. Lakini, ilisaidia waamuzi wenye walichaguliwa, watoe malipizi yenye ililingana na kosa, ni kusema, isipite mipaka ao isikuwe ya chini sana.

 Ile sheria ilisaidia pia mutu mwenye alipanga kufanya mwingine mubaya asifanye vile. Sheria ilieleza hivi: “Wale wenye kubakia [ni kusema, wale wenye walikuwa wanaona vile haki ya Mungu ilitumiwa] watasikia na kuogopa, na hawatafanyaka tena jambo la mubaya kama hilo kati yako.”​—Kumbukumbu la Torati 19:20.

 Wakristo wanaweza pia kufuata ile sheria ya “jicho kwa jicho”?

 Hapana. Ilikuwa kati ya Sheria ya Musa, na iliondolewa na zabihu yenye Yesu alitoa kupitia kifo chake.​—Waroma 10:4.

 Lakini ile sheria inatusaidia tujue muzuri mawazo ya Mungu. Kwa mufano, inaonyesha kama Mungu anapendaka haki. (Zaburi 89:14) Inaonyesha pia kama, kulingana na Mungu, mukosaji alipaswa kupewa malipizi “kwa kiasi chenye kufaa.”​—Yeremia 30:11.

 Mawazo ya uongo kuhusu ile sheria ya “jicho kwa jicho”

 Mawazo ya uongo: Ile sheria ya “jicho kwa jicho” ilipitisha mipaka.

 Mawazo ya kweli: Ile sheria haikuruhusu waamuzi watumikishe haki kupita mipaka, kwa njia ya makali sana. Lakini, waliitumia muzuri, kwa kupatia mutu malipizi ao kusema kama iko na kosa kisha kuchunguza kwanza muzuri kila jambo, na kujua ni kwa kiasi gani ule mukosaji alitenda kosa kimakusudi. (Kutoka 21:28-​30; Hesabu 35:22-​25) Sheria ya “jicho kwa jicho” ilisaidia kuepuka kutoa malipizi ya makali sana.

 Mawazo ya uongo: Ile sheria ya “jicho kwa jicho” ilifanya watu waendelee kulipiza kisasi kila wakati.

 Mawazo ya kweli: Sheria ya Musa ilikuwa inasema hivi: “Haupaswe kulipiza kisasi wala kuwekea kinyongo wana wa watu wako.” (Mambo ya Walawi 19:18) Sheria haikutia moyo Waisraeli wakuwe wanalipiza kisasi, lakini watumainie Mungu na mipango ya sheria yenye iliwekwa ili kushugulikia makosa.​—Kumbukumbu la Torati 32:35.

^ Ile kanuni ya haki, yenye wakati fulani inaitwa pia lex talionis mu Kilatini, ilitumiwa pia mu sheria ya watu mbalimbali wa zamani.