Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Pornografia? Ni Mubaya Kutumiana Mambo ya Ngono ku Enternete?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Pornografia? Ni Mubaya Kutumiana Mambo ya Ngono ku Enternete?

Jibu ya Biblia

 Biblia haizungumuzie waziwazi pornografia, mambo ya ngono ku Enternete, ao mambo ingine sawa ile. Lakini, Biblia inaonyesha waziwazi maoni ya Mungu kuhusu matendo yenye inatia watu moyo kufanya ngono mbele ya ndoa ao kuwafanya wakuwe na maoni ya mubaya juu ya ngono. Fikiria hii maandiko ya Biblia:

  •   “Muue viungo vya mwili wenu vyenye kuwa katika dunia kuhusiana na uasherati, uchafu, tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe.” (Wakolosai 3:5) Kuliko kuua tamaa ya mubaya, kuangalia pornografia kunaichochea. Na kunamufanya mutu akuwe muchafu mbele ya Mungu.

  •   “Kila mutu mwenye anaendelea kumuangalia mwanamuke kwa njia ya kumutamani amekwisha kufanya uzinifu pamoja naye katika moyo wake.” (Matayo 5:​28) Picha zenye kuonyesha matendo machafu ya ngono zinatokeza mawazo ya mubaya yenye inachochea mutu kufanya matendo ya mubaya.

  •   “Uasherati na kila namna ya ukosefu wa usafi ao pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu.” (Waefeso 5:3) Hatupaswe hata kufurahia kuzungumuzia mambo ya uasherati, na kuangalia ao kusoma habari za uasherati.

  •   “Matendo ya mwili yanaonekana wazi, nayo ni uasherati, uchafu, . . . na mambo kama hayo. Ninawaonya mbele ya wakati juu ya mambo hayo, kama vile nimekwisha kuwaonya, kwamba wale wenye wanazoea kufanya mambo kama hayo hawatariti Ufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:​19-​21) Wale wenye wanaangalia video, picha ao kusoma habari za ngono, wale wenye wanatumia wengine ujumbe ao kuzungumuzia ngono ku Enternete ili kuamusha tamaa ya ngono, wale wenye wanatumia telefone yao ili kuzungumuzia ao kutumia wengine picha ao ujumbe wa ngono ni wachafu mbele ya Mungu. Ikiwa tunazoea kufanya ile mambo, Mungu hawezi kutukubali.