Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Ni Wakristo?

Je, Mashahidi wa Yehova Ni Wakristo?

 Ndiyo. Sisi ni Wakristo kwa sababu zifuatazo:

  •   Tunajitahidi kufuata mafundisho na mwenendo wa Yesu Kristo.—1 Petro 2:21.

  •   Tunaamini kwamba Yesu ndiye njia ya kupata wokovu, kwamba “hakuna jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo lazima sisi tupate kuokolewa.”—Matendo 4:12.

  •   Watu wanapokuwa Mashahidi wa Yehova, wanabatizwa katika jina la Yesu.—Mathayo 28:18, 19.

  •   Tunaomba katika jina la Yesu.—Yohana 15:16.

  •   Tunaamini kwamba Yesu ndiye Kichwa, au yule aliyewekwa rasmi kuwa na mamlaka, juu ya wanaume wote.—1 Wakorintho 11:3.

 Hata hivyo, kuna tofauti mbalimbali kati yetu na vikundi vingine vya kidini vya Kikristo. Kwa mfano, tunaamini kwamba Biblia inafundisha kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, si sehemu ya Utatu. (Marko 12:29) Tunaamini kwamba nafsi inaweza kufa, na kwamba hakuna msingi wowote wa Kimaandiko wa kusema kwamba Mungu huwatesa watu milele katika moto wa mateso. Pia, tunaamini kwamba wale wanaoongoza katika mambo ya kidini hawapaswi kuwa na majina ya cheo yanayowainua juu ya watu wengine.—Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4; Mathayo 23:8-10.