Kulingana na Mathayo 23:1-39

  • Msiwaige waandishi na Mafarisayo (1-12)

  • Ole kwa waandishi na Mafarisayo (13-36)

  • Yesu aombolezea Yerusalemu (37-39)

23  Ndipo Yesu akauambia umati pamoja na wanafunzi wake:  “Waandishi na Mafarisayo wamejiketisha kwenye kiti cha Musa.  Kwa hiyo, fanyeni mambo yote wanayowaambia, lakini msitende kama wao, kwa maana wao husema lakini hawatendi mambo wanayosema.+  Wao hufunga mizigo mizito na kuiweka kwenye mabega ya watu,+ lakini wao wenyewe hawataki kuisogeza hata kwa kidole chao.+  Kazi zote wanazofanya, wanazifanya ili waonwe na watu,+ kwa maana wanapanua visanduku vyenye maandiko wanavyovaa kama ulinzi,*+ na kurefusha pindo zenye nyuzi za mavazi yao.+  Wao hupenda mahali penye heshima zaidi kwenye milo ya jioni na viti vya mbele* katika masinagogi+  na kusalimiwa sokoni na kuitwa Rabi* na watu.  Lakini ninyi, msiitwe Rabi, kwa maana Mwalimu+ wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.  Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu+ ni mmoja, Yule aliye mbinguni. 10  Wala msiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo. 11  Lakini aliye mkuu zaidi kati yenu lazima awe mhudumu wenu.+ 12  Yeyote anayejiinua atanyenyekezwa,+ na yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.+ 13  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu mnawafungia watu Ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi wenyewe hamwingii, na mnawazuia wale wanaotaka kuingia.+ 14 * —— 15  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki!+ kwa sababu mnasafiri baharini na kwenye nchi kavu ili kumgeuza imani mtu mmoja, na anapogeuka, mnamfanya astahili Gehena* mara mbili zaidi yenu. 16  “Ole wenu, viongozi vipofu+ mnaosema, ‘Yeyote akiapa kwa hekalu, si kitu; lakini yeyote akiapa kwa dhahabu ya hekalu, yuko chini ya wajibu.’+ 17  Wapumbavu na vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, dhahabu au hekalu linaloitakasa dhahabu hiyo? 18  Isitoshe, ‘Yeyote akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini yeyote akiapa kwa zawadi iliyo kwenye madhabahu, yuko chini ya wajibu.’ 19  Ninyi vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, zawadi au madhabahu ambayo huitakasa zawadi hiyo? 20  Kwa hiyo yeyote anayeapa kwa madhabahu anaapa kwa madhabahu na kwa kila kitu kilicho juu yake; 21  na yeyote anayeapa kwa hekalu anaapa kwa hekalu na kwa Yule anayekaa ndani yake;+ 22  na yeyote anayeapa kwa mbingu anaapa kwa kiti cha ufalme cha Mungu na kwa Yule anayeketi juu yake. 23  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki! kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na dili na bizari,+ lakini mmepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, yaani, haki,+ rehema,+ na uaminifu. Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine.+ 24  Viongozi vipofu,+ ambao huchuja mbu+ lakini hummeza ngamia!+ 25  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki! kwa sababu mnasafisha upande wa nje wa kikombe na wa sahani,+ lakini ndani vimejaa pupa*+ na kutojizuia.+ 26  Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe na sahani ili upande wa nje uwe safi pia. 27  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki!+ kwa sababu mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa,+ ambayo kwa nje yanapendeza lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila namna ya uchafu. 28  Vivyo hivyo, kwa nje mnaonekana waadilifu kwa watu, lakini ndani mmejaa unafiki na uasi sheria.+ 29  “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo wanafiki!+ kwa sababu mnajenga makaburi ya manabii na kuyarembesha makaburi* ya waadilifu,+ 30  nanyi mnasema, ‘Kama tungeishi katika siku za mababu zetu, hatungeshirikiana nao kumwaga damu ya manabii.’ 31  Kwa hiyo, mnashuhudia dhidi yenu wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.+ 32  Basi, kijazeni kipimo cha mababu zenu. 33  “Ninyi nyoka, wana wa nyoka,*+ mtaikimbiaje hukumu ya Gehena?*+ 34  Kwa sababu hiyo, ninawatuma kwenu manabii+ na watu wenye hekima na walimu wa watu wote.+ Baadhi yao mtawaua+ na kuwatundika kwenye miti, na baadhi yao mtawapiga mijeledi+ katika masinagogi yenu na kuwatesa+ katika jiji baada ya jiji, 35  ili damu yote ya waadilifu iliyomwagwa duniani ije juu yenu, kuanzia damu ya Abeli+ mwadilifu mpaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, ambaye mlimuua kati ya patakatifu na madhabahu.+ 36  Kwa kweli ninawaambia, mambo yote haya yatakipata kizazi hiki. 37  “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na aliyewapiga mawe wale waliotumwa kwake+—nilijaribu mara ngapi kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga wake chini ya mabawa yake! Lakini hamkutaka.+ 38  Tazama! Mmeachiwa nyumba yenu.*+ 39  Kwa maana ninawaambia, tangu sasa hamtaniona tena mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!’”*+

Maelezo ya Chini

Au “wanapanua vibweta vyao.”
Au “bora.”
Au “Mwalimu.”
Angalia Kamusi.
Au “vitu vilivyoporwa.”
Au “makaburi ya ukumbusho.”
Au “nyoka-vipiri.”
Angalia Kamusi.
Au labda, “Mmeachiwa nyumba yenu ukiwa.”