Hamia kwenye habari

Walithamini Barua Zake

Walithamini Barua Zake

 Brooke ni Shahidi wa Yehova na anaishi Marekani. Katika kipindi cha COVID-19 alihubiri kwa kuandika barua. Brooke aliandika barua nyingi kila juma. Hata hivyo, baada ya mwaka mmoja na nusu alikata tamaa. Kufikia wakati huo, ni mtu mmoja tu aliyekuwa amejibu barua zake na mtu huyo alimwonya Brooke asijaribu kumwandikia tena. Brooke alihisi jitihada zake zinaambulia patupu.

 Hata hivyo, baada ya muda, dada anayeitwa Kim alimwambia Brooke kwamba alikuwa amezungumza na mteja fulani kwenye benki anayofanya kazi. Mteja huyo alimwambia Kim kwamba alikuwa amepata barua iliyoandikwa kwa mkono kutoka kwa Shahidi wa Yehova. Kumbe barua hiyo ilikuwa imeandikwa na Brooke! Mteja huyo alirudi benki juma linalofuata. Katika mazungumzo yao alimwambia Kim kwamba angependa kuhudhuria mikutano yetu. Kipindi hicho tulikuwa tukifanya mikutano kupitia mtandao.

 Baada ya muda, Shahidi mwingine anayeitwa David, alimwambia Brooke kwamba mfanyakazi mwenzake alikuwa amepokea barua kutoka kwa Brooke. Mfanyakazi huyo aliguswa moyo sana alipoona kwamba barua hiyo ilikuwa imeandikwa kwa mkono. Alimwambia David: “Laiti watu wengi zaidi wangewajali wenzao kiasi hiki.” David alitumia fursa hiyo kumweleza mwanamume huyo habari zaidi kuhusu Biblia na akaahidi kumletea machapisho. Mwanamume huyo alisikiliza na akasema kwamba anatazamia kwa hamu kupata machapisho.

 Ukweli ni kwamba, huenda Mashahidi wa Yehova wasijue mbegu wanayopanda katika huduma inapochipuka. (Mhubiri 11:5, 6) Hata hivyo, mambo hayo yaliyoonwa yalimsaidia Brooke kuona fungu muhimu analotimiza katika kazi ya kuhubiri.​—1 Wakorintho 3:6.