Hamia kwenye habari

“Ninafanya Ninachoweza”

“Ninafanya Ninachoweza”

Irma, anayeishi nchini Ujerumani anakaribia umri wa miaka 90. Amepatwa na aksidenti mbili mbaya na akafanyiwa upasuaji mara kadhaa, kwa hiyo, hawezi kuhubiri nyumba kwa nyumba kama zamani. Sasa Irma anahubiri kwa kuwaandikia barua watu wa ukoo na marafiki. Barua za kuwatia moyo na kuwafariji waliofiwa hupokelewa vizuri sana hivi kwamba mara nyingi watu humpigia simu kumuuliza atawaandikia barua nyingine lini. Pia, yeye hupokea barua nyingi za shukrani zikimwomba aandike barua nyingine. Irma anasema, “Hayo yote hunifanya niwe na furaha na kunifanya niendelee kuhubiri.”

Pia, Irma huwatumia barua watu wengine waliozeeka. Anasema hivi: “Mwanamke fulani mzee alinipigia simu na kusema kwamba barua yangu ilikuwa imemfariji sana baada ya kifo cha mume wake. Ameiweka barua hiyo ndani ya Biblia yake na mara nyingi anaisoma jioni. Mwanamke mwingine ambaye mume wake alikufa hivi karibuni, alisema kwamba barua yangu ilimsaidia zaidi kuliko kuhutubiwa na kasisi wake. Alikuwa na maswali mengi yaliyohitaji majibu na akaomba ikiwa anaweza kunitembelea.”

Rafiki ya Irma ambaye si Shahidi alihamia mbali na akamwomba Irma awe akimwandikia barua. Irma anasema hivi: “Mwanamke huyo alihifadhi barua zangu zote. Alipokufa, binti yake alinipigia simu. Aliniambia kwamba alikuwa amesoma barua zote nilizomwandikia mama yake na akaniomba ikiwa ninaweza kumwandikia yeye pia barua zenye ujumbe wa Biblia.”

Irma anafurahia sana huduma yake. Anasema: “Ninamwomba Yehova aendelee kunipa nguvu za kumtumikia. Ingawa siwezi kwenda nyumba kwa nyumba tena, ninafanya ninachoweza.”