Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 5

Utaona Mambo Gani Katika Mikutano Yetu ya Kikristo?

Utaona Mambo Gani Katika Mikutano Yetu ya Kikristo?

Argentina

Sierra Leone

Ubelgiji

Malasia

Watu wengi wameacha kwenda katika dini zao kwa sababu hawapati mwongozo au faraja ya kiroho. Kwa nini basi uhudhurie mikutano ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova? Utaona mambo gani huko?

Shangwe ya kuwa miongoni mwa watu wenye upendo na wanaojali. Katika karne ya kwanza, Wakristo walipangwa katika makutaniko, nao walikutanika ili kumwabudu Mungu, kujifunza Maandiko, na kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) Wakiwa wamekusanyika pamoja na watu wenye upendo, walihisi kwamba wako miongoni mwa marafiki wa kweli, ndugu zao wa kiroho. (2 Wathesalonike 1:3; 3 Yohana 14) Tunafanya vivyo hivyo leo, nasi tunapata shangwe kama yao.

Faida ya kujifunza jinsi ya kutumia kanuni za Biblia. Kama ilivyokuwa katika nyakati za Biblia, leo pia, wanaume, wanawake, na watoto hukutanika pamoja. Walimu wanaostahili huitumia Biblia kutusaidia kuelewa jinsi ya kutumia kanuni za Biblia maishani. (Kumbukumbu la Torati 31:12; Nehemia 8:8) Wote wanaweza kushiriki katika mazungumzo na kuimba. Kufanya hivyo hutupa nafasi ya kutangaza tumaini letu la Kikristo.—Waebrania 10:23.

Imani yako katika Mungu itaimarishwa. Mtume Paulo aliliambia hivi kutaniko moja: “Ninatamani kuwaona ninyi ili . . . tutiane moyo, kila mmoja kupitia imani ya mwenzake, yenu na yangu pia.” (Waroma 1:11, 12) Tunaposhirikiana kwa ukawaida na waamini wenzetu katika mikutano, imani yetu na azimio letu la kuendelea kuishi kulingana na kanuni za Kikristo huimarika.

Tunakualika uhudhurie mikutano yetu ili ujionee mwenyewe mambo hayo. Utakaribishwa kwa uchangamfu. Hakuna kiingilio katika mikutano yetu wala sadaka hazitolewi.

  • Mikutano yetu inafuata mfano gani?

  • Tunawezaje kufaidika kwa kuhudhuria mikutano ya Kikristo?