Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

AspctStyle/stock.adobe.com

KAMPENI YA UKUMBUSHO

Yesu Atakomesha Vita

Yesu Atakomesha Vita

 Yesu alipokuwa duniani, alionyesha anawapenda watu sana, kufikia hatua ya kudhabihu uhai wake kwa ajili yao. (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni ataonyesha tena kwamba anawapenda watu kwa kutumia mamlaka yake akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu ‘kukomesha vita katika dunia yote.’​—Zaburi 46:9.

 Ona jinsi Biblia inavyofafanua kile ambacho Yesu atafanya:

  •    “Atamwokoa maskini anayelilia msaada, pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi. Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini, naye ataokoa uhai wa maskini. Atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”​—Zaburi 72:12-14.

 Tunaweza kuonyeshaje uthamini kwa ajili ya mambo yote ambayo Yesu amefanya na atakayotufanyia? Kwenye Luka 22:19, Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake. Hiyo ndiyo sababu kila mwaka Mashahidi wa Yehova hukutana ili kuadhimisha kifo chake. Tunakualika ujiunge nasi kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu Jumapili, Machi 24, 2024.

Tafuta Mahali Ukumbusho Utakapofanyika