Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Kwa nini Yesu alishutumu zoea la Wayahudi la kuapa?

VIAPO fulani vilikubalika katika Sheria ya Musa. Hata hivyo, lilikuwa jambo la kawaida sana kwa watu wa siku za Yesu kuapa hivi kwamba waliapa ili kuthibitisha ukweli wa kila jambo walilosema. Ingawa zoea hilo lilikusudiwa kuthibitisha ukweli wa mambo ambayo mtu alisema, Yesu alishutumu zoea hilo katika pindi mbili tofauti. Alifundisha hivi: “Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo.”—Mt. 5:33-37; 23:16-22.

Kamusi Theological Dictionary of the New Testament, inasema kwamba “zoea la Wayahudi la kuthibitisha kila jambo kwa kuapa” lilikuwa limekita mizizi sana; jambo hilo linaonekana wazi katika mistari ya Talmud ambayo inataja kihususa viapo ambavyo vingeweza kukubalika na ambavyo vingeweza kuvunjwa.

Si Yesu peke yake aliyeshutumu mazoea hayo mabaya. Kwa mfano, mwanahistoria Myahudi Flavius Josephus alisema hivi kuhusu dhehebu fulani la Kiyahudi: “Waliepuka kuapa, kwa kuwa waliona kufanya hivyo kuwa jambo baya zaidi kuliko kusema uwongo, na walisema kwamba ikiwa mtu haaminiki bila kuapa kwa Mungu, tayari yeye ni mwenye hatia.” Pia, maandishi ya Kiyahudi ya apokrifa yanayoitwa Wisdom of Sirach, au Ecclesiasticus, (23:11) yanaeleza hivi: “Mwanamume mwenye zoea la kuapa ameasi sheria kabisa.” Hivyo, Yesu alishutumu zoea la kuapa kivivihivi. Ikiwa tunazungumza kweli wakati wote, hatuhitaji kuapa ili maneno yetu yaaminike.