Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MRADI WA KUJIFUNZA

Jifunze kwa Bidii Ili Uendelee Kukaa Macho

Jifunze kwa Bidii Ili Uendelee Kukaa Macho

Soma Danieli 9:​1-19 ili ujifunze umuhimu wa kujifunza kwa bidii.

Chunguza muktadha. Ni mambo gani yaliyokuwa yametukia, na yalikuwa na matokeo gani kwa Danieli? (Dan. 5:29–6:5) Ungehisije ikiwa wewe ungekuwa Danieli?

Chimba zaidi. Huenda Danieli alitumia ‘vitabu gani vitakatifu’? (Dan. 9:​2, maelezo ya chini; w11 1/1 22 ¶2) Kwa nini Danieli aliungama dhambi zake na za taifa la Israeli? (Law. 26:​39-42; 1 Fal. 8:​46-50; dp 182-184) Sala ya Danieli inaonyeshaje kwamba alikuwa mwanafunzi mwenye bidii wa Neno la Mungu?—Dan. 9:​11-13.

Nimejifunza nini? Jiulize hivi:

  • ‘Ninaweza kuepukaje kukengeushwa na matukio ya ulimwengu?’ (Mika 7:7)

  • ‘Nitanufaikaje kwa kusoma kwa bidii Neno la Mungu kama alivyofanya Danieli?’ (w04 8/1 12 ¶17)

  • ‘Ninaweza kujifunza habari gani katika funzo langu la kibinafsi zitakazonisaidia “kuendelea kukesha”?’ (Mt. 24:​42, 44; w12 8/15 5 ¶7-8)