Ufunuo kwa Yohana 20:1-15

  • Shetani afungwa kwa miaka 1,000 (1-3)

  • Wale watakaotawala pamoja na Kristo kwa miaka 1,000 (4-6)

  • Shetani afunguliwa, kisha aangamizwa (7-10)

  • Wafu wahukumiwa mbele ya kiti cheupe cha ufalme (11-15)

20  Nami nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa shimo refu lisilo na mwisho*+ na mnyororo mkubwa mkononi mwake.  Akamkamata yule joka,+ yule nyoka wa zamani,+ ambaye ni Ibilisi+ na Shetani,+ na kumfunga kwa miaka 1,000.  Naye akamtupa katika shimo refu lisilo na mwisho*+ akalifunga na kulitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka 1,000 itakapokwisha. Baada ya hapo atafunguliwa kwa muda mfupi.+  Nami nikaona viti vya ufalme, na wale walioketi kwenye viti hivyo wakapewa mamlaka ya kuhukumu. Ndiyo, niliona nafsi* za wale waliouawa* kwa sababu ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa sababu ya kusema kumhusu Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama wa mwituni au sanamu yake na ambao hawakupokea ile alama kwenye paji la uso wao na kwenye mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo+ kwa miaka 1,000.  (Wale wafu+ wengine hawakuwa hai mpaka ile miaka 1,000 ilipokwisha.) Huo ndio ufufuo wa kwanza.+  Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza;+ kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka 1,000.+  Sasa mara tu ile miaka 1,000 itakapokwisha, Shetani atafunguliwa kutoka katika gereza lake,  naye ataenda kuyapotosha yale mataifa yaliyo katika pembe nne za dunia, Gogu na Magogu, ili kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita. Idadi yao ni kama mchanga wa bahari.  Nao wakaenda katika dunia yote na kuizunguka kambi ya watakatifu na lile jiji linalopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.+ 10  Na Ibilisi aliyekuwa akiwapotosha alitupwa ndani ya lile ziwa la moto na kiberiti, ambamo wote wawili, yule mnyama wa mwituni+ na yule nabii wa uwongo, tayari walikuwa;+ nao watateswa* mchana na usiku milele na milele. 11  Nami nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na Yule aliyeketi juu yake.+ Dunia na mbingu zikatoweka kutoka mbele zake,+ na hazikupatikana tena. 12  Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Wafu wakahukumiwa kutokana na yale mambo yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+ 13  Na bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, nao wakahukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+ 14  Na kifo na Kaburi* vikatupwa ndani ya lile ziwa la moto.+ Hilo linamaanisha kifo cha pili,+ lile ziwa la moto.+ 15  Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kile kitabu cha uzima+ alitupwa ndani ya lile ziwa la moto.+

Maelezo ya Chini

Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Tnn.,” waliouawa kwa shoka.”
Angalia Kamusi na Maelezo ya chini ya Ufu 6:9.
Au “watazuiliwa; watafungwa gerezani.”
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.