Mhubiri 8:1-17

  • Mwanadamu asiye mkamilifu anapotawala (1-17)

    • Tii amri za mfalme (2-4)

    • Madhara ya utawala wa mwanadamu (9)

    • Hukumu isipotekelezwa upesi (11)

    • Ule, unywe, na kufurahia (15)

8  Ni nani aliye kama mwenye hekima? Ni nani anayejua suluhisho la tatizo?* Hekima ya mtu huutia nuru uso wake na kuilainisha sura yake ngumu.  Nasema: “Tii maagizo ya mfalme+ kwa sababu ya kiapo chako kwa Mungu.+  Usifanye haraka kuondoka mbele ya mfalme.+ Usitetee jambo lolote baya;+ kwa kuwa anaweza kufanya jambo lolote apendalo,  kwa sababu neno la mfalme ni uamuzi wa mwisho;+ ni nani anayeweza kumuuliza: ‘Unafanya nini?’”  Mtu anayeshika amri hatapata madhara,+ na moyo wenye hekima utajua wakati unaofaa na utaratibu unaofaa.*+  Kwa maana kila jambo lina wakati wake na utaratibu wake,*+ kwa sababu matatizo ya wanadamu ni mengi sana.  Kwa kuwa hakuna mtu anayejua litakalotukia, ni nani anayeweza kumwambia jinsi litakavyotukia?  Kama vile ambavyo hakuna mtu aliye na nguvu juu ya roho* au anayeweza kuizuia roho, vivyo hivyo hakuna yeyote aliye na nguvu juu ya siku ya kufa.+ Kama vile ambavyo hakuna yeyote anayeruhusiwa kurudi nyumbani wakati wa vita, vivyo hivyo uovu hautawaruhusu wale wanaozoea kuutenda waponyoke.*  Hayo yote nimeyaona, nami nimetafakari moyoni mwangu kila kazi ambayo imefanywa chini ya jua, wakati ambapo mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake kwa kumuumiza.*+ 10  Nami nikaona waovu wakizikwa, wale waliokuwa wakiingia na kutoka mahali patakatifu, lakini walisahauliwa upesi katika jiji ambalo walitenda hivyo.+ Hili pia ni ubatili. 11  Kwa sababu hukumu dhidi ya tendo ovu haijatekelezwa upesi,+ moyo wa wanadamu hupata ujasiri wa kutenda uovu.+ 12  Ingawa huenda mwovu akatenda uovu mara mia moja na bado aishi kwa muda mrefu, hata hivyo ninajua kwamba mambo yatawaendea vyema wale wanaomwogopa Mungu wa kweli, kwa sababu wanamwogopa.+ 13  Lakini mambo hayatamwendea vyema mwovu,+ wala hatarefusha siku zake zilizo kama kivuli,+ kwa sababu hamwogopi Mungu. 14  Kuna jambo la ubatili* ambalo hutukia duniani: Kuna watu waadilifu wanaotendewa kana kwamba walikuwa wametenda uovu,+ na kuna watu waovu wanaotendewa kana kwamba walikuwa wametenda uadilifu.+ Nasema kwamba hili pia ni ubatili. 15  Basi nikapendekeza kushangilia,+ kwa sababu hakuna jambo bora kwa mwanadamu chini ya jua kuliko kula na kunywa na kushangilia; mambo hayo yanapaswa kufuatana naye anapofanya kazi kwa bidii sikuzote za maisha yake,+ ambazo Mungu wa kweli anampa chini ya jua. 16  Nilijitahidi sana ili moyo wangu upate hekima na ili nione shughuli* zote zinazofanywa duniani,+ hata nilikosa usingizi usiku na mchana.* 17  Kisha nikatafakari kazi yote ya Mungu wa kweli, nikatambua kwamba wanadamu hawawezi kufahamu kinachotukia chini ya jua.+ Hata wanadamu wakijitahidi kadiri gani, hawawezi kuifahamu. Hata wakidai kwamba wana hekima ya kutosha kujua, kwa kweli hawawezi kuifahamu.+

Maelezo ya Chini

Au “maana ya jambo.”
Au “hukumu inayofaa.”
Au “hukumu yake.”
Au “pumzi, upepo.”
Au labda, “uovu hauwezi kuwaokoa waovu.”
Au “kumdhuru; kumletea hasara.”
Au “linalovunja moyo.”
Au “kazi.”
Au labda, “kwamba watu hawalali mchana wala usiku.”