Kutoka 32:1-35

  • Ibada ya ndama wa dhahabu (1-35)

    • Musa asikia uimbaji usio wa kawaida (17, 18)

    • Musa ayavunjavunja mabamba ya sheria (19)

    • Walawi wabaki washikamanifu kwa Yehova (26-29)

32  Basi, watu wakaona kwamba Musa amekawia sana kushuka kutoka mlimani.+ Kwa hiyo wakakusanyika kumzunguka Haruni na kumwambia: “Haya, tutengenezee mungu atakayetuongoza+ kwa sababu hatujui lililompata huyu Musa, mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri.”  Ndipo Haruni akawaambia: “Chukueni vipuli vya dhahabu+ ambavyo wake zenu, wana wenu, na binti zenu wamevaa masikioni mniletee.”  Basi watu wote wakaanza kutoa vipuli vya dhahabu walivyokuwa wamevaa masikioni wakamletea Haruni.  Kisha akachukua dhahabu iliyokuwa kwenye vipuli hivyo, akatengeneza sanamu* ya ndama kwa kifaa cha kuchongea.+ Watu wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wenu, enyi Waisraeli, aliyewaongoza kutoka katika nchi ya Misri.”+  Haruni alipoona hilo, akajenga madhabahu mbele ya sanamu hiyo na kutangaza hivi: “Kesho kutakuwa na sherehe kwa ajili ya Yehova.”  Basi wakaamka mapema siku iliyofuata na kuanza kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika. Baada ya hayo watu wakaketi ili wale na kunywa. Kisha wakasimama ili wajitumbuize.+  Sasa Yehova akamwambia Musa: “Nenda, shuka, kwa sababu watu wako uliowaongoza kutoka katika nchi ya Misri wametenda uovu.*+  Wamegeuka haraka na kuacha njia niliyowaamuru wafuate.+ Wamejitengenezea sanamu* ya ndama, nao wanaendelea kuiinamia na kuitolea dhabihu wakisema, ‘Huyu ndiye Mungu wenu, enyi Waisraeli, aliyewaongoza kutoka katika nchi ya Misri.’”  Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nimeona kwamba watu hawa ni wakaidi.*+ 10  Basi sasa, niache niwaangamize kabisa kwa hasira yangu inayowaka, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa.”+ 11  Ndipo Musa akamsihi* Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, kwa nini uwaelekezee watu wako hasira yako inayowaka, baada ya kuwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu?+ 12  Kwa nini Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia ovu alipowatoa Misri. Alitaka kuwaua milimani na kuwaangamiza kabisa kutoka duniani’?+ Acha hasira yako inayowaka na ufikirie upya* uamuzi wako wa kuwaletea watu wako msiba huu. 13  Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Israeli, uliowaapia kwa jina lako mwenyewe na kusema, ‘Nitaufanya uzao wenu uwe mwingi kama nyota za mbinguni,+ nami nitaupa uzao* wenu nchi yote hii niliyowaahidi, ili iwe miliki yao ya kudumu.’”+ 14  Basi Yehova akaanza kufikiria upya* msiba ambao alikuwa amesema atawaletea watu wake.+ 15  Kisha Musa akageuka na kushuka kutoka mlimani akiwa amebeba yale mabamba mawili ya Ushahidi+ mikononi mwake.+ Mabamba hayo yalikuwa yameandikwa pande zote mbili; upande wa mbele na wa nyuma. 16  Mabamba hayo yalitengenezwa na Mungu, na maandishi yake yalikuwa maandishi ya Mungu yalichongwa kwenye mabamba hayo.+ 17  Yoshua alipoanza kusikia sauti za watu wakipiga kelele, akamwambia Musa: “Kuna kelele za vita kambini.” 18  Lakini Musa akasema: “Si sauti za watu wanaoimba kwa sababu ya ushindi,*Wala si sauti za watu wanaolia kwa sababu ya kushindwa;Ninasikia sauti za uimbaji wa aina nyingine.” 19  Mara tu Musa alipoikaribia kambi na kuona ile sanamu ya ndama+ na watu wakicheza dansi, akaanza kuwaka hasira, naye akayatupa chini yale mabamba mawili yaliyokuwa mikononi mwake, yakavunjika-vunjika chini ya mlima.+ 20  Akaichukua sanamu ya ndama waliyokuwa wametengeneza, akaiteketeza na kuipondaponda ikawa ungaunga;+ kisha akaunyunyiza juu ya maji na kuwalazimisha Waisraeli wayanywe.+ 21  Musa akamuuliza Haruni: “Watu hawa walikufanya nini hivi kwamba ukasababisha watende dhambi kubwa hivi?” 22  Haruni akajibu: “Usikasirike, bwana wangu. Unajua vizuri kwamba watu hawa wana mwelekeo wa kutenda maovu.+ 23  Basi waliniambia, ‘Tutengenezee mungu atakayetuongoza, kwa sababu hatujui lililompata huyu Musa, mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri.’+ 24  Basi nikawaambia, ‘Mtu yeyote aliye na dhahabu aitoe na kunipa.’ Kisha nikaitupa motoni na ndama huyu akatokea.” 25  Musa akaona kwamba watu wanafanya watakavyo, kwa sababu Haruni aliwaacha wafanye watakavyo, hivi kwamba wakajiletea aibu mbele ya wapinzani wao. 26  Kisha Musa akasimama kwenye lango la kambi na kusema: “Ni nani aliye upande wa Yehova? Njooni kwangu!”+ Ndipo Walawi wote wakakusanyika kumzunguka. 27  Basi Musa akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mmoja wenu na ajifunge upanga wake na kupita kotekote kambini, kutoka lango mpaka lango, amuue ndugu yake, jirani yake, na rafiki yake wa karibu.’”+ 28  Walawi wakafanya kama Musa alivyowaambia. Kwa hiyo wanaume 3,000 hivi waliuawa siku hiyo. 29  Kisha Musa akawaambia: “Jitakaseni* leo kwa ajili ya Yehova, kwa maana kila mmoja wenu amemshambulia mwana wake mwenyewe na ndugu yake mwenyewe;+ atawabariki leo.”+ 30  Siku iliyofuata, Musa akawaambia watu: “Mlitenda dhambi kubwa sana, na sasa nitapanda kwenda kwa Yehova ili nione ikiwa ninaweza kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi yenu.”+ 31  Kwa hiyo Musa akarudi kwa Yehova na kumwambia: “Watu hawa wametenda dhambi kubwa sana! Walijitengenezea mungu wa dhahabu!+ 32  Lakini sasa ukipenda, wasamehe dhambi yao;+ la sivyo, tafadhali nifute katika kitabu chako ulichoandika.”+ 33  Hata hivyo, Yehova akamwambia Musa: “Yeyote aliyenitendea dhambi, nitamfuta katika kitabu changu. 34  Nenda sasa, waongoze watu kwenda mahali nilipokuambia. Tazama! Malaika wangu atakutangulia,+ na siku ya kuwaadhibu itakapofika, nitawaadhibu kwa sababu ya dhambi yao.” 35  Ndipo Yehova akaanza kuwaletea watu pigo kwa sababu walikuwa wametengeneza sanamu ya ndama, sanamu ambayo Haruni alitengeneza.

Maelezo ya Chini

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Au “wamejichafua.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Tnn., “wana shingo ngumu.”
Tnn., “akautuliza uso wa.”
Au “ughairi kuhusu.”
Tnn., “mbegu.”
Au “kughairi kuhusu.”
Au “tendo la kishujaa.”
Tnn., “Ujazeni mkono wenu.”