Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 2:1-16

  • Paulo ahubiri huko Korintho (1-5)

  • Ubora wa hekima ya Mungu (6-10)

  • Tofauti kati ya mtu wa kiroho na mtu wa kimwili (11-16)

2  Kwa hiyo, nilipokuja kwenu, akina ndugu, sikuja na maneno mengi+ au hekima nikiwatangazia siri takatifu+ ya Mungu.  Kwa maana niliamua kutojua kitu chochote kati yenu isipokuwa Yesu Kristo, naye akiwa ameuawa kwenye mti.+  Nami nilikuja kwenu nikiwa dhaifu, mwenye woga na nikitetemeka sana;  na katika maneno yangu na mambo niliyohubiri sikutumia maneno ya kushawishi yenye hekima bali wonyesho wa roho na nguvu,+  ili imani yenu iwe, si katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.  Basi tunazungumza kuhusu hekima kati ya wale ambao ni wakomavu,+ lakini si hekima ya mfumo huu wa mambo* wala ile ya watawala wa mfumo huu wa mambo, ambao watapitilia mbali.+  Bali tunazungumza kuhusu hekima ya Mungu katika siri takatifu,+ hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiagiza awali kabla ya mifumo ya mambo kwa ajili ya utukufu wetu.  Hakuna mtawala hata mmoja wa mfumo huu wa mambo* aliyeijua hekima hii,+ kwa maana kama wangejua hawangemuua* Bwana mwenye utukufu.  Lakini kama ilivyoandikwa: “Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaompenda.”+ 10  Kwa maana Mungu ameyafunua kwetu+ kupitia roho yake,+ kwa maana roho huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito* ya Mungu.+ 11  Kwa maana ni nani kati ya wanadamu anayejua mambo ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ambaye ameyajua mambo ya Mungu, isipokuwa roho ya Mungu. 12  Basi, sisi hatukupokea roho ya ulimwengu, bali tulipokea roho inayotoka kwa Mungu,+ ili tuyajue mambo ambayo Mungu ametupatia kwa fadhili. 13  Mambo hayo tunayasema pia, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya binadamu,+ bali kwa yale yanayofundishwa kwa roho,+ tunapofafanua* mambo ya kiroho kwa maneno ya kiroho. 14  Lakini mtu wa kimwili hayakubali* mambo ya roho ya Mungu, kwa maana hayo ni upumbavu kwake; naye hawezi kuyajua, kwa sababu yanachunguzwa kiroho. 15  Hata hivyo, mtu wa kiroho huchunguza mambo yote,+ lakini yeye mwenyewe hachunguzwi na mwanadamu yeyote. 16  Kwa maana “ni nani ameijua akili ya Yehova,* ndipo amfundishe?”+ Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “hawangemtundika kwenye mti.”
Au “yenye kina.”
Au “tunapounganisha.”
Au “hayapokei.”