Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 16:1-24

  • Mchango kwa ajili ya Wakristo huko Yerusalemu (1-4)

  • Mipango ya safari za Paulo (5-9)

  • Mipango ya ziara za Timotheo na Apolo (10-12)

  • Himizo na salamu (13-24)

16  Basi kuhusu mchango kwa ajili ya watakatifu,+ fuateni mwongozo niliotoa kwa makutaniko ya Galatia.  Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu anapaswa kuweka kando kitu fulani kulingana na uwezo wake, ili michango isikusanywe nitakapofika.  Lakini nitakapofika huko, nitawatuma watu mtakaopendekeza katika barua zenu,+ wapeleke zawadi yenu ya fadhili Yerusalemu.  Hata hivyo, ikiwa itafaa mimi niende huko pia, wataenda pamoja nami.  Lakini nitakuja kwenu baada ya kupitia Makedonia, kwa maana nitapitia huko Makedonia;+  na labda nitakaa kwa muda au hata nitakaa nanyi kipindi chote cha majira ya baridi, ili mnisindikize umbali fulani kule nitakapoenda.  Kwa maana sitaki kuwaona ninyi sasa ninapopita, kwa kuwa natumaini kukaa pamoja nanyi muda fulani,+ Yehova* akiruhusu.  Lakini nitakaa Efeso+ mpaka Sherehe ya Pentekoste,  kwa sababu nimefunguliwa mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji,+ lakini kuna wapinzani wengi. 10  Sasa Timotheo+ akifika, hakikisheni kwamba haogopi chochote akiwa kati yenu, kwa maana anafanya kazi ya Yehova,*+ kama mimi. 11  Kwa hiyo, mtu yeyote asimdharau. Msindikizeni kwa amani ili aje kwangu, kwa maana ninamsubiri nikiwa pamoja na akina ndugu. 12  Basi kumhusu Apolo+ ndugu yetu, nilimhimiza sana aje kwenu pamoja na akina ndugu. Hakukusudia kuja sasa, lakini atakuja atakapopata nafasi. 13  Kaeni macho,+ simameni imara katika imani,+ endeleeni kuwa kama wanaume,*+ iweni na nguvu.+ 14  Mambo yote mnayofanya yafanyeni kwa upendo.+ 15  Sasa ninawahimiza, akina ndugu: Mnajua kwamba nyumba ya Stefana ndiyo matunda ya kwanza ya Akaya na kwamba walijitoa kuwahudumia watakatifu. 16  Endeleeni kujitiisha kwa watu wa aina hiyo na kwa wale wote wanaoshirikiana na kufanya kazi kwa bidii.+ 17  Lakini ninashangilia kuwapo kwa Stefana+ na Fortunato na Akaiko, kwa sababu wamejazia kutokuwapo kwenu hapa. 18  Kwa maana wameiburudisha roho yangu na yenu. Kwa hiyo, watambueni watu wa namna hiyo. 19  Makutaniko ya Asia yanawatumia salamu zao. Akila na Priska pamoja na kutaniko lililo katika nyumba yao+ wanawasalimu kwa moyo mkunjufu katika Bwana. 20  Ndugu wote wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu. 21  Hii ni salamu yangu, Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. 22  Ikiwa yeyote hampendi Bwana, mtu huyo na alaaniwe. Njoo, Ee Bwana wetu! 23  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu. 24  Upendo wangu na uwe pamoja nanyi nyote katika muungano na Kristo Yesu.

Maelezo ya Chini

Au “kuwa jasiri.”