Hamia kwenye habari

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa Kati ya Watu wa Rangi Tofauti?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa Kati ya Watu wa Rangi Tofauti?

Biblia inajibu

 Mungu anakubali ndoa kati ya mwanaume na mwanamke wa rangi tofauti kwa sababu rangi zote ni sawa machoni pake. Biblia inasema: “Mungu hana ubaguzi . . . , katika kila taifa.”—Matendo 10:34, 35, Tafsiri ya Ulimwengu mpya.

 Fikiria kanuni nyingine za Biblia zinazohusiana na usawa wa kijamii na ndoa.

Watu wa rangi zote walitoka katika chanzo kimoja

 Wanadamu wote wametoka kwa mwanaume wa kwanza, Adamu, na mke wake, Hawa, ambaye Biblia inamwita “mama ya kila mtu anayeishi.” (Mwanzo 3:20) Kwa sababu hiyo, Biblia inasema hivi kumhusu Mungu: “Alifanya kutoka kwa mtu mmoja kila taifa la watu.” (Matendo 17:26) Licha ya rangi tofauti, wanadamu wote ni sehemu ya familia moja tu. Lakini, namna gani ikiwa kuna ubaguzi wa rangi au tofauti kubwa za kijamii katika eneo unaloishi?

Watu wenye hekima “hushauriana”

 Ingawa Mungu anaikubali kabisa ndoa kati ya watu wa rangi tofauti, si watu wote wanaokubaliana na maoni yake. (Isaya 55:8, 9) Ikiwa unafikiria kufunga ndoa na mtu wa rangi tofauti na yako, wewe pamoja na yule utakayefunga naye ndoa mnapaswa kuzungumzia mambo yafuatayo:

  •   Mtashughulikiaje mikazo ambayo huenda mkakabili kutoka katika jamii au familia yenu?

  •   Mtawasaidiaje watoto wenu ili waweza kukabiliana na ubaguzi?

 ‘Kushauriana’ kwa njia hiyo kunaweza kuwasaidia mfanikiwe katika ndoa.—Methali 13:10; 21:5.