Hamia kwenye habari

Je, Tuabudu Sanamu?

Je, Tuabudu Sanamu?

Jibu la Biblia

 La, hatupaswi. Kuhusu sheria ambayo Mungu alipatia taifa la Israeli, kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema hivi: “Kutokana na masimulizi mbalimbali ya Biblia ni wazi kwamba ibada ya kweli ya Mungu haikuhusisha sanamu.” Fikiria mistari hii ya Biblia:

  •   “Usijifanyie sanamu ya kuchongwa wala umbo lililo kama kitu chochote kilicho juu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho ndani ya maji chini ya dunia. Usiviinamie wala kushawishiwa kuvitumikia, kwa sababu mimi Yehova Mungu wako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili.” (Kutoka 20:​4, 5) Kwa kuwa Mungu anataka watu “wajitoe kikamili,” hafurahi kuona tukisifu au kuabudu sanamu, picha, au mifano.

  •   “Sitakubali sanamu zichukue sifa yangu.” (Isaya 42:8, Easy-to-Read Version) Mungu hukataa ibada anayopewa kupitia sanamu. Baadhi ya Waisraeli walipoanza kumwabudu kupitia sanamu ya ndama, Mungu alisema kwamba walifanya “dhambi nzito sana.”​—Kutoka 32:​7-9, Easy-to-Read Version.

  •   “Hatupaswi kuwazia kwamba Mungu ni kama dhahabu au fedha au jiwe, kama kitu kilichochongwa kwa ufundi na mtungo wa mwanadamu.” (Matendo 17:29) Tofauti na ibada ya kipagani, ambayo kwa kawaida huhusisha sanamu ‘zilizochongwa kwa ufundi na mtungo wa mwanadamu,’ Wakristo wanapaswa ‘kutembea kwa imani, si kwa kuona,’ kama Biblia inavyosema.​—2 Wakorintho 5:7.

  •   “Jilindeni na sanamu.” (1 Yohana 5:​21) Katika amri ambazo taifa la Israeli na Wakristo walipewa, Biblia inafunua kwamba mafundisho ya kwamba Mungu anakubali matumizi ya sanamu katika ibada ni ya uwongo.