Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Siko Tena Mutu wa Jeuri”

“Siko Tena Mutu wa Jeuri”
  • Alizaliwa: 1973

  • Inchi: Uganda

  • Alikuwa: Mulevi na mutu wa jeuri

MAISHA YANGU YA ZAMANI

 Nilizaliwa Uganda katika wilaya ya Gomba. Watu wengi mu ile wilaya walikuwa maskini sana. Mu muji wetu hatukukuwa na umeme, kwa hiyo, usiku tulikuwa natumia tala ya pétrole.

 Wazazi wangu wenye walikuwa walimaji walitoka Rwanda na wakahamia Uganda. Walikuwa wanalima café na bitika, na kisha walikuwa wanatengeneza pombe ya bitika yenye inajulikana sana na yenye iliitwa waragi. Tena wazazi wangu walikuwa wanafuga kuku, mbuzi, nguruwe na ngombe. Desturi yetu na namna nilikomala ilinifundisha kama bibi anapaswa kutii bwana yake saa yoyote na hapaswe hata kidogo kuleta mawazo yake.

 Wakati nilikuwa na miaka 23, nilihamia Rwanda, na kule nilizoea kuenda mu nganda pamoya na marafiki wa miaka yangu. Nilikuwa nazoea kuenda sana mu nganda moya hivi mupaka mukubwa wa ile nganda akanipatia karte yenye iliniruhusu niingie mule bila kulipa. Nilifurahia kuangalia filme zenya zilikuwa naonyesha mambo ya kupigana na mambo ya kuuana. Watu wenye nilikuwa naishi nao na mambo yenye nilikuwa najifurahisha nayo ilinichochea nikuwe mutu mwenye jeuri na mulevi kabisa.

 Mu 2000, nilianza kuishi na mwanamuke moya kijana mwenye aliitwa Skolastique Kabagwira, na tukazala watoto watatu. Vile nilijifunzaka wakati nilikuwa kijana, nilitazamia bibi yangu akuwe ananipigia magoti saa yenye anapenda kunisalimia ao wakati anapenda kuniomba kitu fulani. Tena nilijua kama kila kitu yenye familia yetu ilikuwa nayo ilikuwa yangu na ningeitumia vile miye napenda. Mara mingi nilikuwa natoka ku nyumba usiku na kurudia saa tatu ya asubui na niko mulevi. Wakati nilikuwa napika hodi ku mulango na Skolastique anakawia kufungula nilikuwa namupiga.

 Ile wakati nilikuwa nasimamia kompanyi fulani na nilikuwa napata mushahara wa muzuri. Skolastique alijaribu kunisaidia ili nijiunge na kanisa yake ya Wapentekoste, pengine aliwaza kama ile njo ingenibadilisha. Sikupenda kuenda ku kanisa yake. Lakini nilianza njo kupenda mwanamuke mwingine. Juu ya tabia yangu ya mubaya na juu nilikuwa mutu mwenye jeuri, Skolastique alikamata watoto wetu watatu na akahamia kwa wazazi wake.

 Rafiki yetu moya wa zamani aliongea na miye juu ya namna yangu ya kuishi. Alinitia moyo nirudishane na Skolastique. Aliniambia kama watoto wangu hawastahili kabisa kuishi mbali na baba yao. Kwa hiyo mu 2005, niliacha kunywa pombe, na niliachana na ule mwanamuke mwingine na nikarudishana na Skolastique. Mu 2006 tulioana. Lakini, hata vile nilikuwa tu ningali mutu wa jeuri na niliendelea kumutendea bibi yangu mubaya.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

 Mu 2008, Shahidi moya wa Yehova mwenye kuitwa Joël alitutembelea na nilisikiliza ujumbe wake. Kwa miezi mingi yeye na Shahidi mwingine mwenye anaitwa Bonaventure, walinitembelea kwa ukawaida na tulikuwa na mazungumuzo mingi sana nao juu ya Biblia. Niliuliza maulizo mingi, zaidi sana ile yenye inahusu kitabu ya Ufunuo. Kwa kweli, nilikuwa napenda kuonyesha kama Mashahidi wa Yehova wako mu makosa. Kwa mufano, niliwauliza nini njo ilifanya waseme kama “kundi kubwa la watu” wenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 7:9 wangeishi hapa ku dunia, sababu ile mustari inasema kama kundi kubwa ya watu walikuwa “wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme [cha Mungu] na mbele ya Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo. Joël alinijibia maulizo yangu kwa uvumilivu. Kwa mufano, alinionyesha Isaya 66:1, yenye inaonyesha kama Mungu anaita dunia kuwa ‘kiti cha miguu yake.’ Kwa hiyo, kundi kubwa ya watu wanasimama mbele ya kiti ya Ufalme ya Mungu na wako hapa ku dunia. Na nilisoma Zaburi 37:29, yenye kusema kama wenye haki wataishi hapa ku dunia milele.

 Nilifikia kukubali funzo ya Biblia. Kwa hiyo, Bonaventure alijifunza Biblia na miye pamoya na Skolastique. Kadiri tulikuwa tunajifunza Biblia ile ilinichochea kufanya mabadiliko fulani mu maisha yangu. Nilijifunza kutendea bibi yangu kwa heshima. Sikupenda tena aanze kunipikia magoti saa yenye alikuwa anapenda kunisalimia ao kuniomba kitu fulani, na niliacha kusema kama kila kitu yenye familia yetu ilikuwa nayo ilikuwa yangu. Niliacha pia kuangalia filme za jeuri. Haikukuwa mwepesi kufanya ile mabadiliko na iliniomba nionyeshe sifa ya kujizuia na ya unyenyekevu.

Biblia imenisaidia kuwa bwana muzuri zaidi

 Miaka kidogo mbele ya pale, nilitumaka Christian, mutoto wetu mukubwa aende aishi pamoya na watu wa familia yetu Uganda. Lakini, kisha kusoma Kumbukumbu la Torati 6:4-7, nilifikia kuelewa kama miye na bibi yangu tuko na daraka kutoka kwa Mungu ya kuhangaikia watoto wetu na ile daraka inatia ndani kuwafundisha kanuni ya Yehova. Tulifurahi sana wakati mutoto wetu alirudia ku nyumba, na yeye pia!

FAIDA YENYE NIMEPATA

 Nimejifunza kama Yehova ni Mungu mwenye rehema na niko hakika kama amenisamehe juu ya matendo yote ya mubaya yenye nilifanyaka zamani. Niko mwenye furaha kuona vile Skolastique alijiunga na miye ili kujifunza Biblia. Tulitoa maisha yetu kwa Yehova na tulibatizwa pamoya tarehe 4 Mwezi wa 12, 2010. Kwa sasa tunatumainiana na tunafurahia kutumikisha kanuni za Biblia mu familia yetu. Bibi yangu iko na furaha sana juu narudiaka mara moya ku nyumba kisha kutoka ku kazi. Tena, iko mwenye furaha sana juu niko namutendea kwa heshima na adabu, nimeamua kuacha pombe na siko tena mutu mwenye jeuri. Mu 2015, niliwekwa kuwa muzee juu ya kufanya kazi ya uchungaji mu kutaniko. Kati ya watoto wetu tano, watatu walishabatizwa.

 Wakati nilianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova sikukuwa nakubali mambo yenye walikuwa nanifundisha bila kuuliza maulizo. Lakini, nilishangazwa sana kuona vile walitumia Biblia ili kujibia maulizo yangu. Skolastique na miye tulifikia kuelewa kama wale wenye kusema kuwa wanamutumikia Mungu wa kweli wanapaswa kuishi kulingana na kanuni zake hapana kufanya mambo yenye wanajipendea. Namushukuru zaidi Yehova juu amenivuta kwake na juu niko mu sehemu ya familia yake ya kiroho. Wakati nakumbuka maisha yangu ya zamani, naamini kama kwa musaada wa Mungu mutu yeyote mwenye kuwa na moyo wa muzuri anaweza kufanya mabadiliko yenye inaombwa ili kumupendeza.