Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

Mawazo ya watu wengi

 Uongo: Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Noeli juu hawamuamini Yesu.

 Ukweli: Tuko Wakristo. Tunaamini kama wokovu unapatikana kupitia tu Yesu Kristo.—Matendo 4:12.

 Uongo: Munagawanya familia kwa kufundisha watu wasisherehekee Noeli.

 Ukweli: Tunahangaikia sana familia na tunatumia Biblia juu ya kuzisaidia zikuwe nguvu.

 Uongo: Munakosaka mambo ya muzuri ya mu “Noeli”, sawa vile kuonyesha ukarimu, kutakia watu amani mu dunia na kutendea watu mambo ya muzuri.

 Ukweli: Tunajikazaka kuwa wakarimu na wenye kufanya amani kila siku. (Mezali 11:25; Waroma 12:18) Kwa mufano, namna yetu ya kuongoza mikutano na kuhubiri inapatana na hii agizo ya Yesu: “Mulipokea bure, mutoe bure.” (Matayo 10:8) Zaidi ya ile, tunaelewa kama Ufalme wa Mungu tu njo utaleta amani ku dunia.​—Matayo 10:7.

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

  •   Yesu alitupatia amri ya kukumbuka kifo yake, hapana kuzaliwa kwake.​—Luka 22:19, 20.

  •   Mitume na wanafunzi wa kwanza wa Yesu, hawakukuwa nasherehekea Noeli. Kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema kama “watu walianza kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu mu 243 [K.K.Y.],” karne moya kisha mutume wa mwisho kufa.

  •   Hakuna ushuhuda wenye kuonyesha kama Yesu alizaliwa tarehe 25, Mwezi wa 12; tarehe yake ya kuzaliwa haiandikwe mu Biblia.

  •   Tunaamini kama Mungu hakubali Noeli juu inatokana na desturi za kipagani.​—2 Wakorinto 6:17.

Juu ya nini mutu akubali kuchukiwa juu tu ya kukatala kusherehekea Noeli?

 Watu wengi wanaendelea kusherehekea Noeli hata kama wanajua kwamba inatokana na desturi za kipagani na haitegemezwe na Biblia. Wale watu wanaweza kujiuliza: Juu ya nini wakristo wanakubali kuchukiwa juu tu ya kukatala kusherehekea Noeli?

 Biblia inatutia moyo tufikiri, tutumie ‘nguvu zetu za kufikiri’. (Waroma 12:1, 2) Inatufundisha kuisamini kweli. (Yohana 4:23, 24) Ni kweli tunahangaikiaka namna watu wanatuona, lakini tunajikaza kushikamana na kanuni za Biblia hata kama ile inaweza kufanya wengine watuchukie.

 Hata kama hatusherehekeake Noeli, tunaheshimia haki ya kila mutu ya kujiamulia ikiwa ataisherehekea ao hapana. Hatuzuie wengine kuisherehekea.