Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
Dunia hii . . .
-
itabakia hivi?
-
itaharibika sana?
-
ao itakuwa muzuri?
ONA JIBU LA BIBLIA
“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.
UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?
Utakuwa na kazi ya muzuri na yenye kufurahisha.—Isaya 65:21-23.
Hautagonjwaka tena na hautateseka hata kidogo.—Isaya 25:8; 33:24.
Utakuwa na maisha yenye furaha na ya milele pamoja na watu wa familia yako na marafiki wako.—Zaburi 37:11, 29.
TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?
Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:
-
Mungu iko na uwezo wa kutimiza ahadi (malako) zake. Mu Biblia, Yehova Mungu tu njo mwenye anaitwa “Mweza-Yote,” juu iko na nguvu zenye hazina mipaka. (Ufunuo 15:3) Kwa hiyo, iko na nguvu kabisa ya kutimiza ahadi yake ya kufanya maisha ikuwe muzuri sana mu dunia. Biblia inasema kama, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.”—Matayo 19:26.
-
Mungu anapenda sana kutimiza ahadi zake. Kwa mufano, Yehova anapenda kabisa kufufua watu wenye wamekufa.—Yobu 14:14, 15.
Pia, Biblia inaonyesha kama Yesu, Mwana wa Mungu, aliponyesha wagonjwa. Juu ya nini aliponyesha wagonjwa? Juu alipenda kufanya vile. (Marko 1:40, 41) Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. Kama Baba yake, Yesu alipenda kusaidia watu wenye walikuwa na lazima ya musaada.—Yohana 14:9.
Kwa hiyo, tunaweza kuamini kabisa kama Yehova na Yesu wanataka kutusaidia tukuwe na maisha yenye furaha wakati wenye kuja!—Zaburi 72:12-14; 145:16; 2 Petro 3:9.
FIKIRIA ULIZO HILI
Mungu atafanya nini ili maisha ikuwe muzuri ku dunia?
Biblia inajibu ulizo hilo mu MATAYO 6:9, 10 na DANIELI 2:44.