Ona video zinazopatikana

Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?

Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?

Dunia hii . . .

  • itabakia hivi?

  • itaharibika sana?

  • ao itakuwa muzuri?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”​—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utakuwa na kazi ya muzuri na yenye kufurahisha.​—Isaya 65:21-23.

Hautagonjwaka tena na hautateseka hata kidogo.​—Isaya 25:8; 33:24.

Utakuwa na maisha yenye furaha na ya milele pamoja na watu wa familia yako na marafiki wako.​—Zaburi 37:11, 29.

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Mungu iko na uwezo wa kutimiza ahadi (malako) zake. Mu Biblia, Yehova Mungu tu njo mwenye anaitwa “Mweza-Yote,” juu iko na nguvu zenye hazina mipaka. (Ufunuo 15:3) Kwa hiyo, iko na nguvu kabisa ya kutimiza ahadi yake ya kufanya maisha ikuwe muzuri sana mu dunia. Biblia inasema kama, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.”​—Matayo 19:26.

  • Mungu anapenda sana kutimiza ahadi zake. Kwa mufano, Yehova anapenda kabisa kufufua watu wenye wamekufa.​—Yobu 14:14, 15.

    Pia, Biblia inaonyesha kama Yesu, Mwana wa Mungu, aliponyesha wagonjwa. Juu ya nini aliponyesha wagonjwa? Juu alipenda kufanya vile. (Marko 1:40, 41) Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. Kama Baba yake, Yesu alipenda kusaidia watu wenye walikuwa na lazima ya musaada.​—Yohana 14:9.

    Kwa hiyo, tunaweza kuamini kabisa kama Yehova na Yesu wanataka kutusaidia tukuwe na maisha yenye furaha wakati wenye kuja!​—Zaburi 72:12-14; 145:16; 2 Petro 3:9.

FIKIRIA ULIZO HILI

Mungu atafanya nini ili maisha ikuwe muzuri ku dunia?

Biblia inajibu ulizo hilo mu MATAYO 6:9, 10 na DANIELI 2:44.