Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

panitan/stock.adobe.com

KAMPANYE YA UKUMBUSHO

Yesu Atamaliza Umaskini

Yesu Atamaliza Umaskini

 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama anapenda watu sana na alihangaikia sana maskini na wagonjwa. (Matayo 9:36) Yesu alitoa hata uzima wake juu ya wengine. (Matayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni, Yesu ataonyesha tena kama anapenda watu sana, atatumia mamlaka yake akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu juu ya kumaliza umaskini mu dunia yote.

 Ona vile Biblia inaonyesha mambo yenye Yesu atafanya:

  •   “Acha atetee watu wa hali ya chini katika taifa, acha aokoe wana wa maskini.” (Zb. 72:4).

 Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alishatufanyia na mambo yenye atatufanyia? Mu andiko ya Luka 22:19, Yesu aliambia wanafunzi wake wakumbuke kifo yake. Njo maana kila mwaka, ku tarehe yenye Yesu alikufa, Mashahidi wa Yehova wanakutanaka juu ya kukumbuka kifo yake. Tunakukaribisha na weye ukuye kufanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu pamoya na siye Siku ya Yenga, tarehe 24, Mwezi wa 3, 2024.

Ona Fasi Kwenye Ukumbusho Utafanyika