Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Watafsiri Wawili Wenye Walirudisha Jina ya Mungu mu Agano Jipya

Watafsiri Wawili Wenye Walirudisha Jina ya Mungu mu Agano Jipya

 Sala ya Baba Yetu, yenye Yesu alifundishaka wanafunzi wake, ni moya kati ya sala zenye watu wengi wanatiaka mu akili. Ile sala inapatikana mu sehemu yenye watu wanazoe kuita Agano Jipya. Inaanza hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe [ao litukuzwe].” (Matayo 6:9) Lakini, Mu Biblia ya Kiingereza, jina ya Mungu, yenye inatafsiriwa mu Kiingereza “Jehovah” (Yehova) ao wakati fulani “Yahweh,” haipatikane sana mu tafsiri za Kiingereza za Agano Jipya. Mu zile tafsiri muko njo majina ya miungu ya uongo, sawa vile Zeu, Herme, na Artemi. Je, hawakupaswa pia kutaya jina ya Mungu wa kweli na mwenye ni Mutungaji wa Biblia?​—Matendo 14:12; 19:35; 2 Timoteo 3:16.

Vile Agano Jipya inataya miungu mingi ya uongo, hauone kama ingekuwa muzuri pia itaye jina ya Mungu wa kweli?

 Lancelot Shadwell na Frederick Parker, watafsiri wangereza wa Biblia, waliwaza kama jina ya Mungu ilipaswa kurudishwa mu Agano Jipya. Juu ya nini tunasema “kurudishwa”? Juu walifikia kujua kama, ku mwanzo, jina ya Mungu ilikuwa ndani, lakini kisha iliondolewa. Nini njo iliwasaidia wajue vile?

 Shadwell na Parker walijua kama maandishi ya sehemu yenye watu wanazoea kuita Agano la Kale iliandikwaka zaidi sana mu Kiebrania, na mulikuwa jina ya pekee ya Mungu mara mingi sana. Kwa hiyo, walijiuliza ni juu ya nini maandishi ya Agano Jipya yenye walikuwa nayo ile wakati ilikuwa na jina ya Mungu mu kifupi. a Tena, Shadwell aliona kama fasi kwenye maandishi ya Agano Jipya ilitumia maneno ya Agano la Kale, sawa vile “malaika wa Yehova, watu wenye walifanya kopi ya Agano Jipya mu Kigiriki, walitia maneno sawa vile Kyʹri·os, yenye inamaanisha “Bwana” pa nafasi ya jina ya Mungu.”​—2 Wafalme 1:3, 15; Matendo 12:23.

Jina ya Mungu mu Kiebrania

 Mbele hata Shadwell na Parker watoe tafsiri zao za Kiingereza, watafsiri wengine walikuwa walisharudisha jina ya Mungu mu tafsiri zao za Kiingereza za Agano Jipya, lakini hawakuirudisha fasi mingi. b Mbele ya 1863, wakati Parker alitoa Tafsiri ya Agano Jipya ya Neno kwa Neno (A Literal Translation of the New Testament), hakuna hata mutafsiri Muingereza mwenye alirudisha jina ya Mungu fasi mingi mu Agano Jipya yenye ilitolewa. Lancelot Shadwell na Frederick Parker walikuwa nani?

Lancelot Shadwell

 Lancelot Shadwell alizaliwa mu 1808 na alikufa mu 1861. Alikuwa mwanasheria na alikuwa mutoto wa Sir Lancelot Shadwell, mwenye alikuwa musaidizi wa gavana wa mu Uingereza. Alikuwa mu Kanisa ya Anglikana. Hata kama aliamini Utatu, alionyesha kama aliheshimia jina ya Mungu kwa kusema kama ilikuwa “jina tukufu ya YEHOVA.” Mu tafsiri yake, ni kusema, mu Injili ya Matayo na Marko, alitumia jina “Yehova” mara 28 mu maandishi yenyewe, na mara 465 mu maelezo ingine.

 Pengine Shadwell alijua jina ya Mungu wakati aliiona mu maandishi ya kwanza-kwanza ya Kiebrania ya Agano la Kale. Alisema kama wale wenye walitia neno Kyʹri·os pa nafasi ya jina ya Mungu mu tafsiri ya Kigiriki ya Agano la Kale hawakukuwa “watafsiri wanyoofu.”

The Gospel according to Matthew rendered into English with notes, by L. Shadwell (1859), provided by the Bodleian Libraries. Licensed under CC BY-NC-SA 2.0 UK. Modified: Text highlighted

Matayo 1:20 mu tafsiri ya Shadwell

 Mu tafsiri yake, Shadwell alitumia mara ya kwanza jina “Yehova” mu Matayo 1:20. Maelezo yake ya ile andiko inasema hivi: “Neno [Kyʹri·os] mu hii andiko na mu maandiko ingine mingi yenye kuwa mu Agano Jipya inamaanisha YEHOVA, jina ya pekee ya Mungu; na ni jambo ya maana sana kurudisha ile neno mu tafsiri ya Kiingereza.” Alisema tena hivi: “Tunapaswa kufanya vile ili kumuheshimia Mungu. Yeye mwenyewe alijiita YEHOVA, na wakati tuko namuzungumuzia, ni muzuri zaidi kutumia jina yake.” Kisha alisema hivi: “Mu tafsiri yetu ya Biblia ya Version autorisée de la Bible, [ao Tafsiri ya King James], jina YEHOVA haipatikane mara mingi . . . Pa nafasi ya jina ya Mungu, tunakuta neno “The Lord” [“Bwana”].” Shadwell alisema hivi: “The Lord ao Bwana. . . ni jina ya cheo yenye haistahili hata kidogo” kutumiwa pa nafasi ya jina ya Mungu, na anaongezea kama, mu inchi yao, hata yeye watu wanamuitaka “The Lord” ao Bwana.

“[Mungu] mwenyewe alijiita YEHOVA, na wakati tuko namuzungumuzia, ni muzuri zaidi kutumia jina yake.”​—Lancelot Shadwell

 Shadwell alitoa tafsiri yake ya Matayo mu 1859 na mu 1861 alitoa tafsiri yenye kuchangwa ya Matayo na ya Marko. Pale njo kazi yake iliishia. Alikufa tarehe 11 Mwezi wa 1, 1861, wakati alikuwa na miaka 52. Lakini, bidii yake haikupita bure.

Frederick Parker

 Frederick Parker, mufanyabiashara mwenye alikuwa tajiri mu Londres, alizaliwa mu 1804 na alikufa mu 1888. Siku moya, alipata tafsiri ya injili ya Matayo, kisha alianza kutafsiri Agano Jipya wakati alikuwa na miaka 20 hivi. Tofauti na Shadwell, Parker hakuamini fundisho ya Utatu. Aliandika hivi: “[Itakuwa muzuri kama] Wakristo wote “wanakubali mambo ya kweli . . . na kumuabudu tu Mweza-Yote, Yehova.” Parker aliona pia kama maandishi ya Agano Jipya yenye inatumia neno Kyʹri·os juu ya kutafsiri Bwana Mungu na Bwana Yesu ilifanya ikuwe nguvu kuona tofauti kati ya wale watu wawili. Kwa hiyo, alifurahi kuona kama, mu hali fulani, Shadwell alitafsiri neno Kyʹri·os kuwa “Yehova.”

 Namna gani Parker alifikia kuelewa ile? Alijifunza Kigiriki na aliandika vitabu mbalimbali na trakte mu sarufi ya Kigiriki. Alifikia pia kuwa mushiriki wa the Anglo-Biblical Institute, yenye ilikuwa nafanya utafiti mu maandishi ya Biblia juu ya kutoa Biblia za muzuri zaidi mu Kiingereza. Mu 1842, Parker alianza kutoa sehemu fulani za maandishi ao vitabu vya Agano Jipya mu vipindi na mu sehemu mbalimbali. c

Tafsiri ya Agano Jipya ya Parker (Heinfetter)

Mambo Yenye Parker Alifanya ili Kurudisha Jina ya Mungu

 Kwa miaka fulani, Parker aliandika habari kuhusu hii maulizo: “Ni wakati gani neno Kyʹri·os inazungumuzia Bwana Yesu? Na ni wakati gani inazungumuzia Bwana Mungu? Juu ya nini neno Kyʹri·os inatumiwa mara mingi, kulingana na sarufi, ili kuzungumuzia jina na hapana cheo?”

 Wakati Parker aliona tafsiri ya Shadwell ya mu 1859 ya Matayo na maelezo yake kuhusu neno Kyʹri·os, alifikia kuwa hakika kama mu hali fulani, neno Kyʹri·os “ilipaswa kutafsiriwa Yehova.” Njo maana, alitafsiri tena tafsiri yake yote ya Agano Jipya na akatia ndani jina “Yehova” fasi yote kwenye aliwaza kama ilipaswa kuwa, ikitegemea hali na sarufi yenye ilikuwa mu maandishi ya Kigiriki. Kwa hiyo, tafsiri ya Neno kwa Neno ya Agano Jipya (A Literal Translation of the New Testament) yenye Parker alitoa mu 1863 illikuwa ndani jina ya Mungu mara 187 mu maandishi yenyewe. Inaonekana kama ile njo tafsiri ya kwanza ya Kiingereza yenye kutumia jina ya Mungu mu Maandiko yote ya Kigiriki ya Kikristo. d

Ukurasa wa kichwa wa tafsiri ya Agano Jipya ya Parker ya 1864

 Mu 1864, Parker alitoa pia kichapo fulani juu ya kulinganisha tafsiri yake ya Agano Jipya na Version Autorisée ya Kiingereza (A Collation of an English Version of the New Testament . . . With the Authorized English Version). Alichanga zile tafsiri mbili za Agano Jipya juu ya kuonyesha fasi kwenye tafsiri yake ilikuwa tofauti na ile tafsiri ingine. e

 Juu ya kuonyesha ulazima wa kurudisha jina ya Mungu, Parker alitia maandiko mingi mu Version autorisée, sawa vile Waroma 10:13, yenye inasema: “Kwa kuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokoka.” Parker aliuliza hivi: “[Nani] njo angewaza kama maandiko yenye kuwa mu Version autorisée ilizungumuzia Yehova na hapana Yesu Kristo Bwana wetu . . .”?

Waroma 10:13 mu tafsiri ya King James Version (yulu) na mu tafsiri ya Parker ya 1864

 Parker alitumia ratili mingi sana, yenye ilikuwa utajiri mukubwa ile wakati, juu ya kutoa na kueneza trakte, habari, na maandishi yake ingine. Kwa kweli, mu mwaka moya tu, alitumia ratili 800, zenye kwa sasa ni zaidi ya ratili 100 000 za Uingereza (132 000 dolare). Tena, alitumia kwa bure watu wenye alijuana nao na viongozi wa dini kopi mingi za vichapo vyake ili kujua mawazo yao.

 Watu wenye walisoma sana walizarau maandishi na tafsiri za Parker za Agano Jipya vyenye havikuchapishwa sana. Hawakusamini bidii ya Parker, Shadwell, na wengine ya kurudisha jina ya pekee ya Mungu mu Agano Jipya ya Kiingereza.

 Ona pia hii video ya dakika kumi: Kutembelea Jumba la Makumbusho Lenye kuwa Warwick: “Biblia na Jina la Mungu.”

a “Yah” ni kifupi ya jina “Yehova,” yenye iko mu Ufunuo 19:1, 3, 4, 6, inatumia neno “Hallelujah,” (Haleluya) yenye inamaanisha “Mumusifu Yah!”

b Shadwell hakutafsiri Agano Jipya yote. Kulikuwa watafsiri wengine, sawa vile Philip Doddridge, Edward Harwood, William Newcome, Edgar Taylor, na Gilbert Wakefield.

c Juu ya kuepuka kuchanga mambo yake ya maisha na utafiti wake wa Biblia, Parker alitumia jina Herman Heinfetter mu maandishi yake ya kidini na mu tafsiri zake za Biblia. Ile jina inapatikana mara mingi ku nyongeza za Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

d Mu 1864, Parker alitoa tafsiri ya Kiingereza ya Agano Jipya yenye kuwa na jina ya Mungu mara 186.

e Mbele Parker atoe tafsiri zake, tafsiri mingi za Kiebrania za Agano Jipya zilikuwa na jina ya Mungu mu maandiko mbalimbali. Tena, mu 1795, Johann Jakob Stolz alitoa tafsiri mu Kijerumani yenye kuwa na jina ya Mungu zaidi ya mara 90, kuanzia Matayo mupaka Yuda.