Ona video zinazopatikana

Kuko Siku Mateso Itaisha?

Kuko Siku Mateso Itaisha?

Unawaza . . .

  • ndiyo?

  • hapana?

  • ao pengine?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” ​—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Utaamini kabisa kama haiko Mungu njo mwenye anatuleteaka mateso.​—Yakobo 1:13.

Utapata kitulizo wakati unajua kama Mungu anajisikia mubaya wakati tunateseka.​—Zekaria 2:8.

Utakuwa na tumaini kama mateso yote itaisha.​—Zaburi 37:9-11.

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Mungu anachukia wakati watu wanateseka na kutendewa mubaya. Waza namna Yehova Mungu alijisikia wakati watu wake walitendewa mubaya sana zamani. Biblia inasema kama alihuzunika juu “walikuwa wanawatendea mubaya.”​—Waamuzi 2:18, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

    Mungu anachukia sana wale wenye wanatesa wengine. Kwa mufano, Biblia inasema kama anachukia “mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa.”​—Mezali 6:16, 17.

  • Mungu anahangaikia kila mutu. Kila mutu anajua “pigo lake [ao, mateso yake] mwenyewe na maumivu yake mwenyewe,” lakini Yehova naye anaijua!​—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

    Hivi karibuni, Yehova atatumia Ufalme wake ili kumaliza mateso ya kila mutu. (Matayo 6:9, 10) Mbele wakati huo ufike, anafariji kwa upendo watu wenye wanamutafuta kwa moyo wote.​—Matendo 17:27; 2 Wakorinto 1:3, 4.

FIKIRIA ULIZO HILI

Juu ya nini Mungu anaacha watu wateseke?

Biblia inajibu ulizo hilo mu WAROMA 5:12 na 2 PETRO 3:9.