Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kuzeeka Muzuri

Namna ya Kuzeeka Muzuri

UNAJISIKIA namna gani wakati unawaza juu ya uzee? Wakati watu wengi wanawaza juu ya uzee, wanahangaika sana, wanakuwa na wasiwasi, na hata wanaogopa sana. Hiyo ni kwa sababu watu wanaona kuwa uzee unaleta mambo mabaya, kama vile kufanya mwili uonekane wenye kuzeeka, kukosa nguvu, kusahau-sahau, na kuwa na magonjwa ya muda murefu.

Hata hivyo, watu wanazeeka kwa njia tofauti kabisa. Kwa kadiri fulani, watu wamoja wanaendelea kuwa na afya ya muzuri ya mwili na ya akili katika miaka yao ya uzee. Maendeleo yenye imefanyika katika matunzo imesaidia wengine kutunza ao kupunguza maumivu ya magonjwa fulani ya muda murefu. Katika inchi fulani, hilo linafanya watu wengi waishi miaka mingi na kuwa na afya ya muzuri.

Watu wengi wanapenda kuzeeka muzuri, hata kama wanapambana na matatizo ya uzee ao hapana. Namna gani mutu anaweza kuzeeka muzuri? Kwa kiasi fulani, hilo linategemea namna tunaona uzee. Pia litawezekana ikiwa tuko tayari na tuko na uwezo wa kujipatanisha na hali ya uzee. Fikiria mashauri haya yenye Biblia inatutolea ili kutusaidia katika mambo hayo.

UKUWE MWENYE KIASI: “Wenye kiasi wana hekima.” (Methali 11:2) Katika andiko hilo, maneno “wenye kiasi” yanaweza kumaanisha watu wenye kuzeeka ambao wanatambua kama kuna mambo hawawezi tena kutimiza, na hawakatae hali yao. Charles, mwenye miaka 93, anayeishi Brazili, anaonyesha mawazo ya kweli wakati anasema hivi: “Ikiwa unaishi miaka mingi, utazeeka tu. Haiwezekane kuwa tena kijana.”

Lakini kuwa mwenye kiasi haimaanishe kuwa na mawazo mabaya juu ya uzee. Kwa mufano, haimaanishe kama unapaswa kusema: “Nimezeeka, na sina tena uwezo wa kufanya jambo lolote.” Mawazo kama hayo yanaweza kufanya mutu akose furaha. Andiko la Methali 24:10 linasema hivi: “Je, umejionyesha kuwa umevunjika moyo siku ya taabu? Nguvu zako zitakuwa chache.” Kuliko kuwa na mawazo hayo, mutu mwenye kiasi anaonyesha hekima na anajikaza kufanya mambo yenye anaweza kutimiza.

Corrado, mwenye miaka 77, anayeishi Italia, anasema hivi kwa hekima: “Wakati unapanda na motokari kwenye kilima, unabadilisha mwendo lakini unaepuka kuzimisha motokari.” Kwa kweli, mutu anapaswa kubadilisha mambo fulani wakati amezeeka. Corrado na bibi yake wanaonyesha kiasi katika kazi za nyumbani. Wanajikaza kuwa na programu yenye kiasi ili mangaribi wasijisikie wenye kuchoka sana. Marian mwenye miaka 81, anayeishi Brazili, iko pia na mawazo ya muzuri juu ya uzee. Anasema hivi: “Nimejifunza kujiwekea mipaka. Wakati ninatumika, ninapumuzika mara kwa mara ikiwa ni lazima. Ninakaa ao ninalala ili kusoma ao kusikiliza muziki. Nimejifunza kutambua na kuheshimia mipaka yangu.”

Ukuwe mwenye kiasi

UHANGAIKIE SURA YAKO: ‘Wanawake wajipambe kwa mavazi [nguo] yenye mupangilio muzuri, pamoja na kiasi na utimamu wa akili.’ (1 Timotheo 2:9) Maneno ‘mavazi yenye mupangilio muzuri’ yanaonyesha kama mutu anapaswa kuchagua muzuri na kuwa na mipaka. Barbara, mwanamuke mwenye miaka 74, anayeishi Kanada, anasema hivi: “Ninajikaza kuonekana muzuri na musafi. Sipendi kuonekana kuwa wa zamani na kusema kila mara ‘nimezeeka na sihangaikie namna ninaonekana.’” Fern, mwanamuke mwenye miaka 91, anayeishi Brazili, anasema hivi: “Kisha muda fulani ninanunua nguo za mupya ili nijisikie kuwa mwenye kupendeza.” Tuseme nini juu ya wanaume wenye kuzeeka? Antônio, mwenye miaka 73, anayeishi Brazili, anasema hivi: “Ninafanya yangu yote ili nionekane mwenye kupendeza. Ninavaa nguo zenye kuwa safi na mupya.” Na juu ya usafi wake anasema: “Kila siku ninanawa mwili wote na kukata ndevu.”

Hata hivyo, ni lazima uepuke kuhangaikia sana sura yako, kwa sababu hilo linaweza kukufanya ukose “utimamu wa akili.” Bok-im, mwanamuke mwenye miaka 69 anayeishi Korea ya Kusini, iko na mawazo ya muzuri juu ya nguo. Anasema hivi: “Ninaelewa kabisa kama haiko muzuri nivae tena nguo fulani zenye nilikuwa ninavaa wakati nilikuwa kijana.”

Ukuwe na mawazo ya muzuri

UKUWE NA MAWAZO YA MUZURI: ‘Siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya, lakini mutu aliye muchangamufu moyoni anakuwa na karamu sikuzote.’ (Methali 15:15) Wakati unazeeka, unaweza kuwa na mawazo mabaya kama unakumbuka nguvu yenye ulikuwa nayo wakati ulikuwa kijana, na mambo mengi yenye ulikuwa na uwezo wa kufanya. Hilo linaeleweka. Hata hivyo, ujikaze ili mawazo hayo mabaya yasikutawale. Ukiendelea kuwaza kila mara mambo ya zamani, unaweza kukosa furaha na kushindwa kufanya mambo yenye ungali na uwezo wa kufanya. Joseph, mwenye miaka 79, anayeishi Kanada, iko na mawazo ya muzuri. Anasema hivi: “Ninafurahia kufanya mambo yenye ninaweza kufanya kuliko kuhuzunika kwa sababu ya mambo yenye nilikuwa ninafanya zamani, lakini leo siwezi tena kuyafanya.”

Pia kusoma na kujifunza vinaweza kukusaidia kuwa na mawazo ya muzuri na kujua mambo mapya. Kwa hiyo, utafute nafasi za kusoma na kujifunza mambo mapya. Ernesto, mwenye miaka 74, anayeishi Ufilipino, anazoea kuenda mahali pa kuwekea vitabu ili kutafuta vitabu vyenye kumupendeza. Anasema hivi: “Ninafurahia kusoma habari mbalimbali; ni kama vile ninasafiri kupitia usomaji.” Lennart, mwenye miaka 75, anayeishi Suède, aliamua kufanya jambo ngumu sana, ni kusema, kujifunza luga mupya.

Usikuwe muchoyo

USIKUWE MUCHOYO: ‘Mukuwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi.’ (Luka 6:38) Uzoee kutumia wakati na vitu vyako pamoja na wengine. Hilo litakufanya ujisikie kuwa umetimiza jambo fulani la maana na utakuwa na furaha. Hosa, mwenye miaka 85, anayeishi Brazili, anajikaza kusaidia wengine hata kama hana uwezo mwingi wa kimwili. Anasema hivi: “Ninaita kwenye telefone marafiki wagonjwa ao wenye kuvunjika moyo na ninawaandikia barua. Wakati fulani, ninawatumia zawadi ndogo. Ninafurahia pia kupikia wagonjwa chakula.”

Wakati tunasaidia wengine, wao pia wanakuwa tayari kutusaidia. Jan, mwenye miaka 66, anayeishi Suède, anasema hivi: “Wakati unaonyesha wengine upendo, wao pia watakuonyesha upendo.” Mutu mwenye iko tayari kutoa, anatokeza hali ya muzuri yenye wengine wanafurahia.

UFANYE URAFIKI NA WENGINE: ‘Mutu anayejitenga na wengine anatafuta mapendezi yake mwenyewe; anashindana na hekima yote inayotumika.’ (Methali 18:1) Kuna wakati unaweza kupenda kuwa peke yako, lakini uepuke kujitenga na wengine. Innocent, mwenye miaka 72, anayeishi Nigeria, anafurahia kuwa pamoja na marafiki. Anasema hivi: “Ninafurahia kuwa pamoja na watu wa miaka tofauti-tofauti.” Börje, mwenye miaka 85, anayeishi Suède, anasema hivi: “Ninajikaza kuwa pamoja na vijana. Wakati ninaona nguvu yao, ninajisikia tena kuwa kijana katika moyo.” Fanya mupango wa kualika marafiki wakati fulani. Han-sik, mwenye miaka 72, anayeishi Korea ya Kusini, anasema hivi: “Mimi na bibi yangu tunafurahia kualika marafiki wa miaka tofauti-tofauti; wenye kuzeeka na vijana, ili kupitisha wakati pamoja ao kula chakula.”

Ufanye urafiki na wengine

Watu wenye urafiki wanazungumuza na wengine. Lakini, ili kuzungumuza muzuri inafaa pia kusikiliza wengine. Onyesha kama unapendezwa na wengine. Helena, mwenye miaka 71, anayeishi Mozambique, anasema hivi: “Ninafurahia kufanya urafiki na ninatendea wengine kwa heshima. Ninawasikiliza ili nijue mawazo yao na mambo wanapenda.” José, mwenye miaka 73, anayeishi Brazili, anasema hivi: “Watu wanafurahia kuwa pamoja na marafiki wenye kusikiliza muzuri, wenye kujitia pa nafasi yao na kuwahangaikia, wenye wanasema neno la kupongeza kwa wakati unaofaa na wenye kuchekesha.”

Wakati unaeleza mawazo yako, ujikaze ili maneno yako yakuwe “yenye kukolezwa chumvi.” (Wakolosai 4:6) Ukuwe mwenye kufikiria wengine na uwatie moyo.

UKUWE MWENYE SHUKRANI: ‘Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.’ (Wakolosai 3:15) Wakati wengine wanakusaidia, uonyeshe kama unafurahia namna wanakuhangaikia. Kuonyesha shukrani kunasaidia kufanya urafiki muzuri. Marie-Paule, mwenye miaka 74, anayeishi Kanada, anasema hivi: “Mimi na bwana yangu tulihamia katika nyumba ingine. Marafiki wengi walikuja kutusaidia. Tulikosa hata maneno ya kuwashukuru. Tulitumia kila mumoja wao barua ya shukrani, na tulialika wamoja kati yao kula chakula.” Jae-won, mwenye miaka 76, anayeishi Korea ya Kusini, anaonyesha shukrani kwa wale wenye wanamupeleka kwenye Jumba la Ufalme. Anasema hivi: “Mimi ni mwenye shukrani sana kwa musaada wote huo, na ninajikaza kutoa feza kidogo za kununua essence. Wakati fulani ninatayarisha zawadi ndogo na ninaandika barua za shukrani.”

Zaidi ya yote, onyesha shukrani kwa sababu ya uzima wako. Mufalme Sulemani mwenye hekima alitukumbusha hivi: ‘Imbwa aliye hai [muzima] ni afazali kuliko simba aliyekufa.’ (Mhubiri 9:4) Kwa kweli, mutu anaweza kuzeeka muzuri ikiwa iko na mawazo ya muzuri na iko tayari kujipatanisha na hali ya uzee.

Ukuwe mwenye shukranil