Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Vitu vya zamani vinaunga mukono habari za Biblia?

Mufalme Sargoni wa pili wa ashuru, anayetajwa katika isaya 20:1

Habari yenye ilichapishwa katika gazeti moja ilisema kama leo vitu vya zamani vyenye vimepatikana, vinahakikisha kuwa “karibu watu 50” wenye wanatajwa katika Maandiko ya Kiebrania waliishi kabisa (Biblical Archaeology Review). Kati ya watu hao kuna wafalme 14 wa Yuda na Israeli; wale wenye kujulikana sana kama vile Daudi na Hezekia, na wale wasiojulikana sana kama vile Menahemu na Peka. Habari hiyo inataja pia Mafarao 5 na wafalme 19 wa Ashuru, Babiloni, Moabu, Perse, na Siria. Lakini kuna watu wengine wenye hawakuwa watawala, wenye wanatajwa pia katika Biblia na katika vitu vyenye vilivumbuliwa. Kwa mufano kuna watu wenye hawakujulikana sana kama vile makuhani wakubwa, muandishi mumoja, na watu wengine wenye mamlaka fulani.

Habari hiyo inasema tena kama “watu wengi wenye elimu wanakubaliana” kuwa watu hao wote wenye kutajwa waliishi kabisa. Bila shaka Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanazungumuzia watu wengine wengi wenye wanatajwa pia katika historia, na vitu vyenye vilivumbuliwa vinaonyesha wengi kati yao na kuhakikisha kuwa waliishi kabisa. Kati ya watu hao kuna Herode, Pontio Pilato, Tiberio, Kayafa, na Sergio Paulo.

Tangu wakati gani simba hawako tena katika maeneo yenye kuzungumuziwa katika Biblia?

Muchoro kwenye ukuta wa Babiloni ya zamani

Leo simba hawako katika mapori ya maeneo yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Lakini inaonekana kuwa waandikaji wa Biblia waliwajua sana kwa sababu maandiko ya Biblia yanataja wanyama hao karibu mara 150. Maandiko mengi kati ya hayo yanazungumuzia simba kwa njia ya mufano; lakini maandiko fulani yanazungumuzia simba wa kwelikweli. Kwa mufano Biblia inasema kama Samsoni, ­Daudi, na Benaya waliua simba. (Waamuzi 14:5, 6; 1 Samweli 17:34, 35; 2 Samweli 23:20) Watu wengine waliuawa na simba.—1 Wafalme 13:24; 2 Wafalme 17:25.

Zamani, simba wa Asia (Panthera leo persica) walipatikana katika Asia ndogo, Ugiriki, Palestina, Siria, Mesopotamia, na kaskazini-mangaribi mwa India. Simba alikuwa munyama mwenye kuogopwa na kuheshimiwa, na mara nyingi watu wa inchi fulani za Asia walikuwa wanatengeneza michoro na sanamu za simba. Njia yenye kuingia katika muji wa Babiloni ilikuwa yenye kupambwa na michoro ya simba yenye kupendeza sana.

Inasemekana kuwa wapiganaji wa dini walikuwa wanawinda simba katika inchi ya Palestina karibu na mwaka wa 1200. Inawezekana simba waliisha kabisa katika eneo hilo muda mufupi kisha mwaka wa 1300. Hata hivyo, simba walikuwa wangali katika Mesopotamia na Siria kufikia mwaka wa 1900 hivi, na katika Iran na Iraq kufikia mwaka wa 1950 hivi.