Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika New York

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika New York

NDUGU Cesar na dada Rocio bibi yake, walikuwa na maisha mazuri katika jimbo la Californie kumepita miaka fulani. Katika jimbo hilo, ndugu Cesar alitumika katika kazi ya kutia joto, hewa na baridi katika nyumba. Kazi hiyo ilikuwa inamuchukua wakati mwingi sana. Lakini dada Rocio alikuwa na kazi yenye haikumuomba wakati mwingi katika biro ya munganga mumoja. Walikuwa na nyumba yao wenyewe na hawakuwa na watoto. Hata hivyo, kulitokea jambo fulani lenye lilibadilisha maisha yao. Ni jambo gani lilitokea?

Katika Mwezi wa 10, 2009, biro ya tawi ya États-Unis ilituma barua kwa makutaniko yote ya États-Unis. Barua hiyo iliomba wale wote wenye wanajua ufundi fulani wajitolee kwa muda fulani ili kusaidia kupanua majengo ya Beteli ya Wallkill, New York. Barua hiyo ilialika hata wale wenye walikuwa wamevukisha miaka yenye inaombwa ili kutumikia kwenye Beteli. Ndugu Cesar na dada Rocio wanasema hivi: “Kwa sababu ya miaka yetu, tuliona kwamba hiyo ni nafasi ya pekee sana katika maisha ya kutumikia kwenye Beteli. Tulisema kwamba hatuwezi kupoteza pendeleo hilo.” Kwa hiyo, ndugu Cesar na dada Rocio wakajaza ombi.

Wajitoleaji fulani wenye kutumikia Warwick

Lakini ndugu Cesar na dada Rocio walifanya zaidi ya mwaka moja bila kualikwa kwenye Beteli. Hata hivyo, walijikaza kufanya maisha yao kuwa mepesi ili waweze kufikia muradi wao. “Mahali tulikuwa tunawekea motokari tulipageuza kuwa chumba kimoja ili tuweze kupangisha nyumba yetu kwa mutu mwengine. Kisha tukaacha nyumba yetu ya metre za muraba 200 (ao 200 mètres carrés) yenye tulipenda sana na yenye tulijenga kumepita miaka fulani, na tukahamia katika chumba cha metre za muraba 25. Ndugu Cesar anasema hivi: “Kufanya mabadiliko hayo kulitufanya tukuwe tayari kutumikia kwenye Beteli ikiwa tungealikwa.” Ni nini ilitokea kisha hapo? Dada Rocio anasema hivi: “Mwezi moja kisha kuhamia katika chumba hicho, tulipokea mwaliko wa kuenda kutumikia kwa muda fulani kwenye Beteli ya Wallkill kama wafanyakazi wa kujitolea. Tulielewa kwamba kwa kufanya maisha yetu ikuwe mepesi, tulimupatia Yehova nafasi ya kutubariki.”

Jason, Cesar, na William

WANABARIKIWA KWA SABABU YA ROHO YAO YA KUJITOA

Kama vile ndugu Cesar na dada Rocio walifanya, ndugu na dada wengi walijitoa sana ili kuenda kusaidia katika kazi ya ujenzi yenye inafanyika katika New York. Wamoja kati yao wanasaidia kupanua Beteli ya Wallkill, na wengine wengi wako na pendeleo la kusaidia kujenga makao makubwa ya duniani pote ya Warwick. * Bibi na bwana wengi wameacha nyumba zao nzuri, kazi nzuri, na hata wanyama wao ili kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova. Yehova alibariki roho hiyo ya kujitoa? Bila shaka, alifanya hivyo!

Way

Tuchukue mufano wa ndugu Way ambaye alijua mambo ya umeme (courant), na dada Debra, ambao walikuwa wanaishi katika jimbo la Kansas. Walikuwa na miaka karibu 60 na waliuzisha nyumba na vitu vyao vingi, kisha wakaenda kwenye Beteli ya Wallkill ili kutumika kama Wanabeteli wanaoishi inje ya Beteli. * Hilo liliwaomba kufanya mabadiliko katika maisha yao, lakini wanajisikia kwamba wamebarikiwa sana. Kuhusu mugawo wenye alipewa, dada Debra anasema hivi: “Wakati fulani ninajisikia kwamba niko pamoja na wale wenye kuonyeshwa kwenye picha katika vichapo vyetu na ambao wanajenga nyumba katika Paradiso!”

Ndugu Melvin na dada Sharon, bibi yake, wa Caroline du Sud waliuzisha nyumba na vitu vyao ili waweze kusaidia katika kazi ya ujenzi ya Warwick. Hata kama haikuwa mwepesi kufanya hivyo, wanaona kwamba ni pendeleo kufanya kazi hiyo ya lazima sana. Wanasema hivi: “Ni furaha kubwa sana kujua kwamba kazi yenye tunafanya italetea faida ndugu na dada wa duniani pote.”

Kenneth

Ndugu Kenneth ambaye alikuwa mujenzi hapo zamani, na dada Maureen bibi yake, wana miaka 55 hivi. Walitoka Californie ili kuenda kusaidia katika kazi ya ujenzi ya Warwick. Ili waweze kuhama, walimuomba dada mumoja wa kutaniko achunge nyumba yao, na waliomba watu wa familia wamushugulikie baba yake na Kenneth mwenye kuzeeka. Je, wanasikitika kwa sababu wamejitolea ili kutumikia kwenye Beteli? Hapana! Ndugu Kenneth anasema hivi: “Tunapata faida nyingi sana. Tunapata pia magumu fulani, lakini tunaishi maisha yenye furaha, na tunatia wengine moyo wajitolee katika kazi hii.”

MAGUMU MBALIMBALI HAYAKUWAZUIA

Ndugu na dada wengi wenye wamejitolea, walipambana na magumu fulani. Kwa mufano, ndugu William na dada Sandra bibi yake, ambao wana miaka 60 hivi, walikuwa na maisha mazuri katika Pennsylvania. Walikuwa na kompanyi ya kutengeneza sehemu mbalimbali za mashine, na walikuwa na wafanyakazi 17. Walikuwa katika kutaniko moja tangu walikuwa watoto wadogo, na waliishi katika eneo moja na watu wengi wa jamaa yao. Kwa hiyo, wakati walipewa nafasi ya kutumikia kwenye Beteli ya Wallkill kama Wanabeteli wenye kuishi inje, walielewa kwamba walipaswa kuacha kila kitu chenye walikuwa wanapenda, na kuacha watu wenye walikuwa wanazoeana nao. Ndugu William anasema hivi: “Bila shaka, tatizo kubwa zaidi ilikuwa kuacha eneo letu lenye tulikuwa tunafurahia sana.” Lakini kisha kusali sana, ndugu huyo na bibi yake waliamua kuenda; na leo, hawaone kwamba walifanya uamuzi mubaya. Ndugu William anasema hivi: “Furaha yenye tunapata kwa kutumika moja kwa moja na familia ya Beteli, hatuwezi kuilinganisha na kitu kingine chochote. Mimi na Sandra tunapata furaha kubwa yenye tulikuwa hatujapataka!”

Bibi na bwana fulani wenye kutumikia Wallkill

Ndugu Ricky, musimamizi wa ujenzi katika Hawaii, alialikwa ili asaidie katika kazi ya ujenzi ya Warwick kama Mwanabeteli mwenye kuishi inje. Dada Kendra, bibi yake, alipenda Ricky akubali mualiko huo. Hata hivyo, jambo lenye liliwahangaisha sana ilikuwa kumushugulikia Jacob, mutoto wao wa miaka 11. Walijiuliza ikiwa ni jambo la hekima wote wahamie New York, na ikiwa mutoto wao ataweza kuzoea eneo hilo mupya.

Ndugu Ricky anasema hivi: “Jambo lingine lenye lilituhangaisha sana ilikuwa kupata kutaniko lenye kuwa na vijana ambao wako na hali nzuri ya kiroho. Tulipenda Jacob apate marafiki wengi wazuri.” Mwishowe, wakapata kutaniko lenye lilikuwa na watoto wachache sana, lakini lenye lilikuwa na Wanabeteli wengi. Ndugu Ricky anasema tena hivi: “Kisha kukusanyika kwa mara ya kwanza katika kutaniko hilo, nilimuuliza Jacob maoni yake kuhusu kutaniko hilo mupya, zaidi sana kwa sababu kutaniko hilo halikuwa na vijana wa miaka yake. Akaniambia: ‘Papa, usiogope. Vijana Wanabeteli ndio watakuwa marafiki wangu.’”

Jacob na wazazi wake wanafurahia kuwa pamoja na Wanabeteli katika kutaniko lao

Kama vile alisema, vijana Wanabeteli wamefanya urafiki pamoja na Jacob. Matokeo imekuwa nini? Ndugu Ricky anaeleza: “Usiku moja, nilipita pembeni ya chumba cha mutoto wangu, na nikaona kwamba alikuwa hajazima tala. Niliwaza nitamukuta iko anacheza michezo ya video, kumbe alikuwa anasoma Biblia! Nilimuuliza kama alikuwa anafanya nini, akaniambia: ‘Ninataka kuwa kijana Mwanabeteli; kwa hiyo, nitasoma Biblia yote katika mwaka moja.’” Bila shaka, ndugu Ricky pamoja na dada Kendra bibi yake, ni wenye furaha sana. Si kwa sababu tu ndugu Ricky anasaidia kujenga Beteli ya Warwick, lakini pia kwa sababu kuhamia katika New York kunasaidia mutoto wao akomae kiroho.—Met. 22:6.

HAWAOGOPE WAKATI UNAOKUJA

Luis na Dale

Mwishowe, kazi ya ujenzi ya Wallkill na Warwick itamalizika. Kwa hiyo, wale wote wenye wamealikwa ili kusaidia katika kazi hiyo wanaelewa kwamba kazi yao ni ya muda tu. Je, ndugu na dada hao wako na wasiwasi na kujiuliza wataenda wapi ao watafanya nini? Hapana! Wengi wanajisikia kama ndugu wawili na bibi zao, kutoka Florida na ambao wana miaka 50 hivi. Ndugu John, musimamizi wa ujenzi, na dada Carmen bibi yake, ambao walijitolea ili kusaidia katika kazi ya ujenzi ya Warwick, wanasema hivi: “Mupaka sasa tumejionea namna Yehova ametimiza mahitaji yetu ya lazima. Tuko hakika kwamba Yehova hakutufikisha hapa ili kutuachilia baadaye.” (Zab. 119:116) Ndugu Luis, ambaye anatengeneza vyombo vya kuzima moto, na dada Quenia bibi yake, wanatumikia kwenye Beteli ya Wallkill. Wanasema hivi: “Tumekwisha kujionea namna Yehova ametutimizia mahitaji yetu ya kimwili kwa ukarimu. Tuko hakika kwamba Yehova ataendelea kututimizia mahitaji yetu, hata kama hatujue atafanya hivyo namna gani, wakati gani, ao wapi.”—Zab. 34:10; 37:25.

‘BARAKA HATA KUSIKUWE NA UHITAJI TENA’

John na Melvin

Ndugu na dada wengi wenye wameenda kusaidia kufanya kazi ya ujenzi katika New York, walikuwa na sababu nyingi zenye zingewafanya wakose kujitolea. Hata hivyo, walimujaribu Yehova kama vile yeye mwenyewe anatuomba sisi wote: ‘Tafazali, munijaribu, . . . kama sitawafungulia ninyi malango ya mbinguni na kuwamwangia baraka hata kusikuwe na uhitaji tena.’—Mal. 3:10.

Wewe pia utamujaribu Yehova ili ujionee namna atakubariki? Kwa hiyo, usali na ufikirie namna unaweza kusaidia katika kazi nzuri sana za ujenzi mbalimbali wa kiteokrasi, iwe katika New York ao mahali pengine, na ujionee namna Yehova atakubariki.—Mk. 10:29, 30.

Gary

Ndugu Dale, ambaye ni fundi wa ujenzi, na dada Cathy bibi yake, kutoka Alabama, wanajitolea ili kusaidia katika kazi ya ujenzi ya Wallkill na wanatia wengine moyo kufanya hivyo. Wanasema hivi: “Ikiwa unapata ujasiri wa kutoka katika eneo lenye unapenda sana, utaona namna roho ya Yehova itakusaidia.” Inaomba ufanye nini ili kujitayarisha? Ndugu Dale anasema hivi: “Ufanye maisha yako yakuwe mepesi zaidi. Hautasikitika hata siku moja!” Ndugu Gary, kutoka Caroline du Nord, amesimamia kazi ya ujenzi kwa muda wa miaka 30. Yeye na dada Maureen bibi yake, wanasema kwamba kati ya baraka zenye wamepata kwa kutumikia Warwick ni “kujuana na kutumika pamoja na ndugu na dada wengi wenye sifa nzuri ambao wametumia maisha yao ili kumutumikia Yehova kwenye Beteli.” Ndugu Gary anasema tena hivi: “Ili uweze kutumikia kwenye Beteli, ni lazima ufanye maisha yako kuwa mepesi, na hiyo ndio namna nzuri zaidi ya kuishi katika ulimwengu huu.” Ndugu Jason, ambaye alikuwa fundi wa kutia umeme, na dada Jennifer bibi yake, kutoka Illinois, wanasema kwamba kazi ya ujenzi kwenye Beteli ya Wallkill inafanana sana na “mambo yenye watu watafanya katika dunia mupya.” Dada Jennifer anaongeza hivi: “Inafurahisha sana kujua kwamba Yehova anapendezwa na kila kitu chenye tunafanya, na hilo linatutayarisha kwa ajili ya wakati unaokuja wenye anatutayarishia. Yehova anafanya ubarikiwe sana.”

^ fu. 6 Ona Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2014, ukurasa wa 12-13.

^ fu. 7 Wanabeteli wanaoishi inje ya Beteli na ambao hawatumike kwa wakati wote, wanatumika siku moja ao zaidi katika juma kwenye Beteli. Wanajilipia garama za nyumba zao na wanashugulikia mahitaji yao mengine.