Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea

Walijitoa kwa Kujipendea

KATI ya Mashahidi wenye kutumika kwa bidii katika inchi kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme, kuna dada wengi wenye hawajaolewa. Wamoja kati yao wametumika katika inchi zingine kwa miaka mingi. Miaka mingi yenye imepita, ni nini iliwasaidia wahamie katika inchi zingine? Kutumika katika inchi zingine kumewafundisha mambo gani? Wamepata baraka gani? Tulizungumuza na dada fulani kati ya dada hao wenye uzoefu. Ikiwa uko dada mwenye hajaolewa na mwenye anapenda kabisa kufanya kazi hiyo yenye kuleta furaha sana, tuko hakika kama maelezo yao yatakuletea faida. Kwa kweli, watumishi wote wa Mungu wanaweza kupata faida kwa kuchunguza mufano wao.

KUPIGANISHA MASHAKA

Anita

Unajiuliza ikiwa uko kabisa na uwezo wa kufanya kazi ya upainia katika inchi ingine hata kama haujaolewa? Anita, mwenye kuwa sasa na miaka 75, alikuwa na mashaka sana juu ya uwezo wake. Alikomalia katika Uingereza kwenye alianza kufanya kazi ya upainia wakati alikuwa na miaka 18. Anasema hivi: “Nilifurahia kufundisha watu juu ya Yehova, lakini nilikuwa sijafikiria hata kidogo kutumikia katika inchi ingine. Nilikuwa sijajifunza hata kidogo luga ya kigeni na nilikuwa hakika kama siwezi kujua hata luga moja. Kwa hiyo, wakati nilipata mualiko wa kusoma Masomo ya Gileadi, nilishituka sana. Nilishangaa kuona kuwa mutu wa bure-bure kama miye angeweza kupata mualiko kama huo. Lakini nilifikiri hivi, ‘ikiwa Yehova anaona kuwa nitaweza kusoma masomo hayo, nitajikaza.’ Kumepita zaidi ya miaka 50. Tangu wakati huo, nimekuwa katika kazi ya umisionere katika Japani.” Anita anaongeza hivi: “Wakati fulani, ninaangalia dada vijana na macho yenye kungaa kwa furaha na ninawaambia, ‘Beba sakoshi yako na unifuate katika kazi ya muzuri zaidi ya wakati wote!’ Ninafurahi kusema kama wengi wamefanya hivyo.”

KUWA NA UJASIRI

Dada wengi wenye wametumikia katika inchi zingine walikuwa na mashaka mwanzoni juu ya kuhamia katika inchi ingine. Namna gani walipata ujasiri wa kufanya hivyo?

Maureen

Maureen, mwenye kuwa sasa na miaka 64, anasema hivi: “Wakati nilikuwa ninakomaa, nilipenda sana kuwa na maisha yenye kusudi, maisha ya kusaidia wengine.” Wakati alikuwa na miaka 20, alihamia Quebec, Kanada, kwenye kulikuwa lazima kubwa ya mapainia. Anasema tena hivi: “Kisha nilipata mualiko wa kusoma Masomo ya Gileadi, lakini niliogopa kuenda nafasi kwenye sijue bila kuwa na marafiki wangu. Pia, nilikuwa na wasiwasi juu ya kuacha mama yangu mwenye alipaswa kuhangaikia baba yangu mwenye alikuwa mugonjwa. Kwa siku nyingi, nilimulilia Yehova usiku katika sala juu ya mambo hayo. Wakati nilizungumuza na wazazi wangu juu ya mahangaiko yangu, walinitia moyo nikubali mualiko huo. Pia, niliona namna ndugu na dada katika kutaniko letu walikuwa wanasaidia wazazi wangu kwa upendo. Kuona namna Yehova alihangaikia wazazi wangu kulinisaidia nikuwe na tumaini kuwa angenihangaikia pia. Kwa hiyo, nilikuwa tayari kuenda!” Kuanzia mwaka wa 1979, Maureen alifanya kazi ya umisionere kwa miaka zaidi ya 30 katika Afrika ya Mangaribi. Leo, Maureen anachunga mama yake katika Kanada, na anaendelea kuwa painia wa pekee. Wakati anakumbuka miaka yenye alitumika katika inchi zingine, anasema hivi: “Sikuzote Yehova alinipatia mambo yenye nilikuwa nayo lazima na kwa wakati wenye kufaa.”

Wendy

Wendy, mwenye kuwa sasa na miaka 65, alizaliwa Australia kwenye alianza kufanya kazi ya upainia wakati alikuwa na miaka 14. Anakumbuka hivi: “Nilikuwa mwenye haya sana na ilikuwa vigumu kwangu kuzungumuza na watu wenye sijue. Lakini kazi ya upainia ilinifundisha kuzungumuza na watu wa namna zote, kwa hiyo sikuendelea kuogopa tena. Kisha, nilitambua kama sikukuwa tena na tatizo la kuogopa. Kazi ya upainia ilikuwa inanifundisha kumutegemea Yehova, na nilianza kufurahia kutumikia katika inchi ingine. Pia, dada mumoja mwenye alikuwa amefanya kazi ya umisionere katika Japani kwa zaidi ya miaka 30, alinialika niende kuhubiri kwa miezi tatu katika Japani. Kutumika pamoja naye kulinichochea zaidi nihamie katika inchi ingine.” Katika mwaka wa 1986, Wendy alihamia Vanuatu, kisiwa chenye kuwa kwenye kilometre 1770 mashariki mwa Australia.

Wendy angali huko Vanuatu, sasa anatumikia kwenye biro moja ya kutafsiri. Anasema hivi: “Kuona namna vikundi na makutaniko yanaendelea kuanzishwa katika maeneo ya mbali kunaniletea furaha sana. Kusaidia kidogo katika kazi ya Yehova katika visiwa hivyo ni pendeleo kubwa sana.”

Kumiko (katikati)

Kumiko, mwenye kuwa sasa na miaka 65, alikuwa painia wa kawaida katika Japani wakati painia mwenzake alimuomba wahamie Nepali. Kumiko anasema hivi: “Painia huyo aliendelea kuniomba tena na tena tuhamie huko, lakini niliendelea kukataa. Nilikuwa na wasiwasi juu ya kujifunza luga ingine na kufanya mabadiliko ili kuzoea eneo la mupya. Ilikuwa pia vigumu kupata feza zenye zingenisaidia kuhamia katika inchi ingine. Wakati nilikuwa ninajikaza kukamata maamuzi, nilifanya aksidenti na pikipiki (moto) na nilipelekwa katika hospitali. Wakati nilikuwa huko, nilifikiri hivi: ‘Ni nani mwenye anajua mambo yenye yanaweza kunifikia kisha hapa? Ninaweza kupatwa na ugonjwa mubaya sana na kupoteza nafasi yangu ya kufanya kazi ya upainia katika inchi ingine. Sababu gani siwezi kutumika katika inchi ingine hata kwa mwaka moja tu?’ Nilisali sana kwa Yehova ili anisaidie kutenda.” Kisha kutoka katika hospitali, Kumiko alitembelea inchi ya Nepali, na kisha yeye na painia mwenzake walihamia katika inchi hiyo.

Wakati anakumbuka miaka kumi yenye ametumika katika Nepali, Kumiko anasema hivi: “Mambo yenye yalikuwa yananihangaisha yalipita mbele yangu kama vile Bahari Nyekundu. Ninafurahi sana kwa sababu nilianza kutumika mahali kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Mara nyingi, wakati ninazungumuzia ujumbe wa Biblia kwenye nyumba ya familia fulani, majirani tano ao sita wanakuja kusikiliza. Hata watoto wadogo wananiomba kwa heshima niwapatie trakte zenye kuzungumuzia Biblia. Ni furaha kubwa kuhubiri katika eneo kwenye watu wako tayari kukubali ujumbe wa Ufalme.”

KUPIGANISHA MAGUMU

Kwa kweli, dada wenye bidii wenye tumezungumuzia walipambana na magumu. Namna gani walipiganisha magumu hayo?

Diane

Diane, mwenye kutoka Kanada, anasema hivi: “Mwanzoni niliona kuwa ni vigumu kuishi mbali sana na familia yangu.” Sasa iko na miaka 62, na alifanya kazi ya umisionere kwa miaka 20 katika Ivory Coast (sasa Côte d’Ivoire). “Nilimuomba Yehova anisaidie nipende watu katika mugawo wangu. Mwalimu moja wa Gileadi, Ndugu Jack Redford, alituambia kama mwanzoni tunaweza kuhuzunishwa, hata kujisikia mubaya sana kwa sababu ya hali wa watu katika mugawo wetu, zaidi sana wakati tutajionea sisi wenyewe namna watu ni masikini sana. Lakini alisema hivi: ‘Musiangalie umasikini. Muangalie watu, kwenye nyuso na macho yao. Muangalie namna wanatenda wakati wanasikia kweli za Biblia.’ Nilifanya hivyo, na ilikuwa baraka! Wakati nilikuwa ninahubiria watu ujumbe wa Ufalme wenye kufariji, niliona namna macho yao yalikuwa yanaangaa kwa furaha!” Ni jambo gani lingine lilimusaidia Diane azoee kutumika katika inchi ingine? Anasema hivi: “Nilikaribia sana wanafunzi wangu wa Biblia na nilifurahi sana kuwaona wanakuwa watumishi waaminifu wa Yehova. Mugawo wangu ulikuwa kama vile nyumbani kwetu. Kama vile Yesu aliahidi, nilipata mama na baba, ndugu na dada wa kiroho.”—Mk. 10:29, 30.

Anne, mwenye kuwa sasa na miaka 46 anatumikia Asia katika inchi fulani ambamo kazi yetu inakatazwa. Anasema hivi: “Kwa miaka mingi wakati nilikuwa ninatumikia katika maeneo mbalimbali katika inchi ya kigeni, niliishi pamoja na dada wenye walikomaa katika hali mbalimbali na wenye tabia zenye zilikuwa tofauti sana na zangu. Wakati fulani, hilo lilikuwa linafanya tukose kuelewana na tukwazane. Wakati hilo lilitokea, nilijikaza kukaribia sana dada wenye tuliishi pamoja nao, ili kuelewa muzuri zaidi desturi zao. Pia, nilifanya yangu yote ili kuwaonyesha upendo na kuwa mwenye usawaziko. Ninafurahi kwa sababu kufanya hivyo kulikuwa na matokeo ya muzuri na kumefanya nikuwe na marafiki wa sana na wenye wamenisaidia kuvumilia magumu katika mugawo wangu.”

Ute

Katika mwaka wa 1993, Ute, wa inchi ya Ujerumani, mwenye kuwa sasa na miaka 53, alipewa mugawo wa kuwa misionere katika Madagascar. Anasema hivi: “Mwanzoni, nilijikaza sana kujifunza luga ya eneo hilo, kuzoea baridi, na kupambana na malaria, amibe, na nyoka zenye kuwa katika tumbo. Lakini, nilisaidiwa sana. Dada wa eneo hilo, watoto wao, na wanafunzi wangu wa Biblia walinisaidia kwa uvumilivu ili nijue luga. Misionere mwenzangu alinihangaikia kwa upendo wakati nilikuwa mugonjwa. Lakini zaidi ya yote, Yehova alinisaidia. Nilimutupia kwa ukawaida mahangaiko yangu katika sala. Kisha, wakati fulani nilingojea kwa uvumilivu kwa siku nyingi ao kwa miezi mingi ili sala zangu zijibiwe. Yehova alimaliza kila tatizo.” Sasa, Ute ametumika katika Madagascar kwa miaka 23.

MAISHA YENYE BARAKA NYINGI

Kama vile wahubiri wengine wenye kutumika mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, dada wenye hawajaolewa wenye wanatumika katika inchi zingine, mara nyingi wanasema kuwa kufanya hivyo, kumewaletea baraka nyingi sana katika maisha yao. Ni baraka gani fulani zenye wamepata?

Heidi

Heidi, wa inchi ya Ujerumani, mwenye kuwa sasa na miaka 73, amefanya kazi ya umisionere katika Ivory Coast (sasa Côte d’Ivoire) kuanzia mwaka wa 1968. Anasema hivi: “Furaha kubwa zaidi yenye nimepata, ni kuona watoto wangu wa kiroho ‘wanatembea katika kweli.’ Watu fulani wenye nilijifunza nao Biblia zamani, leo ni mapainia na wazee wa kutaniko. Wengi kati yao wananiita Mama ao Tate (Nkambo). Mumoja kati ya wazee hao na bibi yake na watoto, wananiona kama mutu wa familia yao. Kwa hiyo, Yehova amenipatia mutoto mwanaume, mukwe wangu mwanamuke, na wajukuu (wankana) watatu.”—3 Yoh.4

Karen (katikati)

Karen, wa inchi ya Kanada, mwenye kuwa sasa na miaka 72, alitumika kwa miaka zaidi ya 20 katika Afrika ya Mangaribi. Anasema hivi: “Maisha ya umisionere yalinifundisha kuwa mutu mwenye kujitoa sana, mwenye upendo, na mwenye uvumilivu. Pia, kuwa pamoja na wafanya-kazi wenzangu wenye kutoka katika inchi mbalimbali kulifanya nipanuke. Nilijifunza kama kuko njia mbalimbali za kufanya mambo. Leo, ni baraka kubwa sana kuwa na marafiki wapendwa katika dunia yote! Hata kama migawo na maisha yetu yamebadilika, urafiki wetu unaendelea.”

Margaret, wa inchi ya Uingereza, mwenye kuwa sasa na miaka 79, alifanya kazi ya umisionere katika inchi ya Laos. Anasema hivi: “Kutumika katika inchi ingine kulinisaidia nijionee namna Yehova anakaribisha watu wa rangi zote za ngozi na wa hali mbalimbali ya maisha katika tengenezo lake. Hilo, lilitia kabisa nguvu imani yangu. Linanihakikishia kabisa kuwa Yehova anaendelea kuongoza tengenezo lake na kama makusudi yake yatatimia.”

Kwa kweli, dada wenye hawajaolewa wenye wanatumika katika inchi zingine, wamefanya mengi sana katika kazi ya kuhubiri. Wanastahili kupongezwa kwa furaha. (Amu. 11:40) Zaidi ya hilo, hesabu yao inaendelea kuongezeka. (Zab. 68:11) Unaweza kubadilisha mambo fulani katika maisha yako na kufuata mufano wa dada wenye bidii wenye tumezungumuzia katika habari hii? Ikiwa unaweza kufanya hivyo, kwa kweli ‘utaonja na kuona kuwa Yehova ni mwema.’—Zab. 34:8.