Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Namna gani watu wa zamani walikuwa najua mwanzo wa mwaka na wa mwezi?

MU INCHI ya Ahadi, mwaka wa Waebrania ulikuwa naanza na kipindi ya kulima na kupanda, na ile ilikuwa mu Mwezi wa 9 na Mwezi wa 10 kulingana na kalendari yetu ya leo.

Juu ya kujua kama mwezi uko na siku ngapi, watu walifuata muzunguko wa mbalamwezi, wenye unafanyaka siku 29 ao 30. Na juu ya kujua kama mwaka uko na siku ngapi, waliangalia vipindi vya hali ya hewa. Lakini, mwaka wenye ulihesabiwa kwa kufuata mizunguko ya mbalamwezi ni mufupi kuliko mwaka wenye ulihesabiwa kwa kuangalia vipindi vya hali ya hewa. Kwa hiyo, walikuwa na lazima ya njia yenye ingewasaidia kufanya zile njia mbili za kuhesabu wakati zipatane. Walifanya vile kwa kuongeza siku fulani ao kwa kuongeza mwezi mwingine, pengine ku mwanzo wa mwaka wenye kufuata. Ile ilisaidia kalendari yao ipatane na wakati ya kupanda na kuvuna.

Lakini, mu wakati ya Musa, Mungu alisema kama mwezi wa kwanza wa mwaka wa Waisraeli ungekuwa Abibu, ao Nisani, wenye leo uko kati ya Mwezi wa 3 na Mwezi wa 4. (Kut. 12:2; 13:4) Mu mwezi wa Nisani, Waisraeli walifanya sikukuu, na mu ile sikukuu, walipaswa kumutolea Yehova mazao ya kwanza ya shayiri.​—Kut. 23:15, 16.

Mu kitabu yake The History of the Jewish People in the Age of Jesus Christ, (175 B.C.–A.D. 135), Emil Schürer, mutu mwenye elimu, anasema hivi: “Ilikuwa mwepesi kujua wakati yenye iliomba kuongeza mwezi moya mu kalendari. Pasaka, yenye ilipaswa kufanywa wakati mbalamwezi yote inakuwa kiviringo, mu mwezi wa Nisani (Nisani 14), kila mara ilipaswa kufanywa kisha siku yenye muchana na usiku vilikuwa na urefu moya, mu kipindi ya mvua ya kwanza . . . Kwa hiyo, kama Pasaka ingefanywa mbele ya ile siku, Wayahudi waliongeza mwezi moya [mwezi wa 13] mbele ya Nisani.”

Mashahidi wa Yehova wanatumiaka ile njia ili kujua tarehe ya Ukumbusho, yenye inaangukaka mu kipindi ya mvua ya kwanza, na yenye inalingana na Nisani 14 mu kalendari ya Kiebrania. Makutaniko ya mu dunia yote inajulishwaka ile tarehe mbele ya wakati. *

Lakini Waebrania walijua namna gani wakati mwezi moya ungemalizika na wakati mwezi mupya ungeanza? Leo ni mwepesi. Unaweza tu kuangalia ku kalendari yako ya karatasi ao kalendari yenye iko mu chombo yako ya kielektroniki. Lakini, zamani haikukuwa mwepesi.

Wakati ya Garika, mwezi ulikuwa na siku 30. (Mwa. 7:11, 24; 8:3, 4) Miaka fulani kisha Garika, mwezi wa Waebrania haukukuwa na siku 30. Kwa Waebrania, mwezi ulianza wakati tu mbalamwezi ilianza kuonekana. Ilianza kuonekana siku ya 29 ao 30 kisha mwezi wenye ulitangulia kuanza.

Wakati fulani, Daudi na Yonatani walizungumuzia mwanzo wa mwezi, kwa kusema: “Kesho ni mwezi [mbalamwezi] mupya.” (1 Sa. 20:5, 18) Kwa hiyo, inaonekana ile wakati, miezi ilikuwa nahesabiwa mbele ya wakati. Lakini namna gani Mwisraeli angejua ni wakati gani mwezi ulianza? Mishna, kitabu yenye kuzungumuzia sheria na desturi za Wayahudi, inatoa habari fulani. Inaonyesha kama kisha Wayahudi kutoka mu uhamisho wa Babiloni, Sanhedrini (tribinali kubwa ya Wayahudi) ilikuwa nasaidia watu kujua ni wakati gani mwezi ulianza. Mu miezi saba yenye sikukuu zilikuwa nafanywa, Sanhedrini ilikuwa nakutana siku ya 30 ya mwezi. Waamuzi wa Sanhedrini walikuwa na daraka ya kuamua ni wakati gani njo mwezi wenye kufuata ungeanza. Nini njo iliwasaidia kuamua?

Wanaume waliwekwa kwenye vilima kuzunguka Yerusamu na walikuwa naangalia juu ili kuona ni wakati gani mbalamwezi ingetokea. Na bila kukawia, walijulisha Sanhedrini. Wakati Sanhedrini ilipata ushuhuda wa kutosha wenye kuonyesha kama mbalamwezi imetokea kabisa, ilijulisha watu kama mwezi mupya umeanza. Lakini tuseme nini kama mawingu ao kunguku ingezuia wale wanaume kuona kuwa mbalamwezi imetokea? Kama ni vile, Sanhedrini iliamua kama mwezi wenye walikuwa ndani uko na siku 30, na kwa hiyo mwezi mupya ungeanza siku ya kufuata.

Mishna inaonyesha kama, juu ya kutangaza kama mwezi mupya umeanza, watu waliwasha moto ku Mulima wa Mizeituni, karibu na Yerusalemu. Mu maeneo ingine ya Israeli, moto uliwashwa juu ya kueneza habari. Mu miaka yenye ilifuata, wajumbe walitumwa juu ya kueneza habari. Kwa hiyo, mu Yerusalemu na mu maeneo ingine, watu walijua kama mwezi mupya umeanza. Wote wangeweza sasa kufanya sikukuu tarehe ileile.

Muchoro wenye kuwa hapa chini unaweza kukusaidia kuelewa miezi, sikukuu, na vipindi vya kalendari ya Kiebrania.

^ Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi 2, 1990, uku. 15.