Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Je, Waroma waliruhusu mutu mwenye alitundikwa ku muti, sawa vile Yesu, azikwe mu kaburi?

WATU wengi wanajua kama Yesu alitundikwa ku muti kati ya watenda-mabaya wawili. (Mt. 27:35-38) Lakini, watu fulani wanaamini kama Biblia haiseme kweli wakati inasema kama mwili wa Yesu ulitayarishwa kwa ajili ya maziko na kisha ukatiwa mu kaburi.​—Mk. 15:42-46.

Wachunguzi fulani wa vitabu vya Injili hawako hakika kama mutu mwenye alitundikwa angeruhusiwa kuzikwa mu kaburi. Lakini, wale wachunguzi wanaamini kama mutu mwenye anatundikwa alikuwa anatendewa mu njia tofauti. Ariel Sabar, mutangazaji wa habari na mumoja wa waandikaji wa gazeti Smithsonian, anafasiria juu ya nini wachunguzi fulani wako na ile mawazo. Anasema hivi: “Kutundikwa ilikuwa malipizi ya watu wenye kuzarauliwa sana. Njo maana wachunguzi fulani walisema kama ni upumbavu kuwaza kuwa Waroma wangeruhusu watu wenye kutundikwa wazikwe kwa njia ya heshima vile.” Waroma walipenda kupatisha haya watu wenye walihukumiwa kutundikwa. Njo maana mara mingi walikuwa wanaacha miili ya wale watu ku muti juu ikuliwe na ndege na wanyama wa pori. Kisha, sehemu za miili yao zenye zilibakia zilitupwa pamoya mu kaburi.

Lakini, watu wenye kuchimbula vitu vya zamani wamevumbula jambo fulani tofauti kuhusu mabaki ya miili ya Wayahudi fulani wenye waliuawa. Mu 1968, walivumbula mabaki ya mifupa ya mwanaume fulani mwenye alitundikwa mu karne ya kwanza. Waliivumbula mu kaburi moya ya familia ya Wayahudi karibu na Yerusalemu. Ile mabaki ilikuwa mu sanduku ya mifupa. Kati ya ile mabaki, mulikuwa mufupa wa kisigino. Ule mufupa ulikuwa umepigiliwa ku ubao na musumari wa chuma wenye urefu wa santimetre 11.5. Sabar anasema hivi: “Ule mufupa wa kisigino wa mwanaume mwenye kuitwa Yehokanani ulitoa ushuhuda wenye kuonyesha kama Injili haidanganye wakati inasema kama Yesu alizikwa mu kaburi. Kwa hiyo, mufupa wa kisigino wa Yehokanani unaonyesha kama wakati ya Yesu kuko watu wenye walitundikwa na kisha Waroma waliruhusu wazikwe mu kaburi sawa vile Wayahudi walikuwa wanazika.”

Mufupa wa kisigino wa Yehokanani unatokeza mawazo yenye kutofautiana juu ya namna Yesu alitundikwa ku muti. Lakini mambo yenye tunajua kabisa ni kwamba watenda-mabaya fulani wenye walitundikwa walizikwa, miili yao haikutupwa tu mu kaburi. Kwa hiyo, Biblia haidanganye wakati inasema kama mwili wa Yesu ulizikwa mu kaburi. Ushuhuda unaonyesha kama mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli.

Na zaidi sana, Yehova alitabiri kama Yesu angezikwa mu kaburi ya mwanaume tajiri, na hakuna mwenye anaweza kuzuia maneno ya Mungu isitimie.​—Isa. 53:9; 55:11.