Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mazungumuzo ya mbele ya wakati na yenye kuwa wazi ni ya maana sana

Wakati Mupendwa Anakaribia Kufa Kwa Sababu ya Ugonjwa Fulani

Wakati Mupendwa Anakaribia Kufa Kwa Sababu ya Ugonjwa Fulani

DOREEN alivurugika sana wakati, Wesley, bwana yake, mwenye kuwa na miaka 54 tu alivumbuliwa na kivimba kwenye ubongo chenye kuwa hatari sana. * Wanganga walisema kama anabakia na miezi kidogo tu ya kuishi. Anakumbuka hivi: “Sikuamini mambo yenye walisema. Nilikuwa kama vile mwenye kufa kwa majuma mingi. Ilikuwa kama vile hali hiyo ilikuwa inapata mutu mwengine, hapana sisi. Sikuwazia kama hali hiyo ingetupata.”

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, hali hiyo yenye ilimufikia Doreen inapata watu wengi. Hali ya mutu mwenye anakaribia kufa kwa sababu ya ugonjwa fulani inaweza kumuletea huzuni mutu yeyote na wakati wowote. Jambo la kufurahisha ni kwamba watu wengi wako tayari kuchunga wapendwa wao wenye wanakaribia kufa kwa sababu ya ugonjwa fulani. Lakini kuchunga mutu mwenye kuwa mugonjwa haiko kazi mwepesi. Watu wa familia wanaweza kufanya nini ili kuchunga na kufariji wapendwa wao wenye wanakaribia kufa kwa sababu ya ugonjwa fulani? Namna gani watu wenye kuchunga mupendwa wao wanaweza kupambana na hisia zenye zinaweza kuwapata wakati wote wa ugonjwa huo? Ni nini inaweza kutazamiwa kadiri kifo kinakaribia? Hata hivyo, kwanza, tuone sababu gani kuchunga wapendwa wenye kukaribia kufa ni kazi yenye kuwa nguvu sana leo.

TATIZO LENYE KUHANGAISHA WATU LEO

Sayansi yenye kujifunza mambo ya matunzo imebadilisha namna ya kufa. Kumepita miaka mia moja hivi watu wengi walikuwa na tumaini la kuishi miaka kidogo, hata katika inchi zenye kuendelea. Watu wengi walikufa sana kwa sababu ya magonjwa ya kuambukiza na aksidenti. Watu wengi hawakuwa na uwezo wa kupata matunzo kwenye hospitali, kwa hiyo, walichungwa na watu wa familia zao na walikufa nyumbani.

Leo, maendeleo katika mambo ya matunzo yamewezesha wanganga kupiganisha magonjwa kabisa ili kurefusha uzima. Zamani magonjwa yenye yangeua mutu bila kukawia, leo yanaweza kufanya miaka mingi. Lakini, kurefusha uzima haiko kumaliza magonjwa. Mara nyingi, wagonjwa wanakuwa na uzaifu mukubwa wenye kufanya washindwe kujihangaikia wao wenyewe. Kuchunga watu kama hao kunakuwa vigumu zaidi na inaomba kujitoa kabisa.

Hilo linafanya watu wengi wanaanza kufa kwenye hospitali kuliko nyumbani. Watu wengi hawajue alama zenye kuonyesha kama mutu anaanza kufa, na watu kidogo tu ndio wameona na macho yao namna mutu anakufa. Kuogopa kifo kunaweza kuzuia ao hata kupunguza bidii ya mwenye kuhangaikia mutu wa familia mwenye kuwa mugonjwa. Ni nini inaweza kusaidia?

MUJITAYARISHE MBELE YA WAKATI

Kama vile habari ya Doreen inaonyesha, watu wengi wanavurugika sana wakati mupendwa wao anapatwa na ugonjwa wenye kuua. Hata kama unahangaika, unaogopa, na unahuzunika, ni nini inaweza kukusaidia kujitayarisha kwa ajili ya mambo yenye kuwa mbele? Mutumishi mumoja muaminifu wa Mungu alisali hivi: “Utuonyeshe jinsi ya kuzihesabu siku zetu hivi kwamba tupate kuuingiza moyo wa hekima.” (Zaburi 90:12) Ndiyo, umuombe Yehova Mungu kwa bidii akuonyeshe namna ya ‘kuhesabu siku zako’ kwa hekima ili utumie muzuri siku zenye kubakia ambazo utapitisha pamoja na mupendwa wako.

Hilo linaomba kujitayarisha muzuri. Kama mupendwa wako angali na uwezo wa kuzungumuza na kama anapenda kutoa mawazo yake, inaweza kuwa jambo la hekima kumuuliza nani mwenye anapaswa kukamata maamuzi pa nafasi yake wakati hatakuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote. Kuzungumuza waziwazi na mugonjwa ili kujua kama anaweza kupenda wamusaidie kupumua tena, kubakia kwenye hospitali, ao kupata matunzo fulani kunaweza kupunguza magumu ya kukosa kuelewana na kusaidia watu wa familia wasijihukumu wakati itawaomba kukamata maamuzi kwa ajili ya mugonjwa mwenye hana tena uwezo wa kufanya jambo lolote. Mazungumuzo ya mbele ya wakati na yenye kuwa wazi yanaweza kusaidia watu wa familia kukaza akili yao juu ya kuchunga mupendwa wao wakati wa magonjwa yake. Biblia inasema, ‘Mipango inavunjika mahali ambapo hapana mazungumuzo ya siri.’​—Methali 15:22.

NAMNA UNAWEZA KUSAIDIA

Mara nyingi, kazi kubwa ya mutu mwenye kuchunga mugonjwa ni kutoa faraja. Mutu mwenye anakaribia kufa iko na lazima ya kuhakikishiwa kama anapendwa na kama haiko peke yake. Namna gani unaweza kufanya hivyo? Umusomee ao umuimbie mugonjwa, kwa kuchagua vitabu na nyimbo zenye kujenga na zenye anapenda. Watu wengi wanafarijiwa wakati mutu wa familia yao anakamata mukono wao na kuongea nao kwa upole.

Kila mara, ni jambo lenye kufaa kumusaidia mugonjwa ajue ni nani wanakuja kumutembelea. Ripoti moja inasema hivi: “Inasemekana kwamba, kati ya uwezo wa kuona, kusikia, kunusa, kugusa, na kuonja, uwezo wa kusikia ndio wa mwisho kupotea. Hata kama mugonjwa anaweza kuonekana kuwa mwenye kusinzia, bado uwezo wake wa kusikia unaweza kuwa ungali wenye nguvu, kwa hiyo, usiseme jambo lenye haungemuambia kama angekuwa macho.”

Kama inawezekana, usali pamoja naye. Biblia inaonyesha kama wakati fulani, mutume Paulo pamoja na wenzake walipambana na magumu makali na hawakuwa hakika kama wangeendelea kuishi. Walitafuta musaada gani? Paulo alitia moyo rafiki zake hivi: ‘Ninyi pia munaweza kushiriki kusaidia kwa dua yenu kwa ajili yetu.’ (2 Wakorintho 1:8-11) Sala ya kutoka moyoni ni ya lazima sana wakati wa magumu makali na magonjwa hatari.

UKUBALI HALI HIYO

Mara nyingi, wazo la kifo cha mupendwa linahangaisha sana. Hilo halishangaze kwa sababu kifo haiko jambo la asili. Kifo hakikupangwa kuwa sehemu ya kawaida ya maisha yetu. (Waroma 5:12) Neno la Mungu linasema kwamba kifo ni “adui.” (1 Wakorintho 15:26) Kwa hiyo, kuepuka kuwaza kuhusu kifo cha mupendwa ni jambo la kawaida na lenye kueleweka.

Hata hivyo, kufikiria mbele ya wakati mambo yenye yanaweza kutokea kunaweza kusaidia watu wa familia kupunguza woga wao na kukazia uangalifu juu ya namna ya kushugulikia muzuri mambo hayo kadiri inawezekana. Alama fulani zenye zinaweza kutokea zinaonyeshwa katika sehemu “ Majuma ya Mwisho ya Maisha.” Ni kweli kwamba alama hizo zote hazitokee kwa kila mugonjwa wala kufuatana kabisa kama vile zinaonyeshwa katika sehemu hiyo. Lakini, wagonjwa wengi wanaonyesha alama fulani kati ya hizo.

Kisha kifo cha mupendwa, inaweza kuwa muzuri kuzungumuza na rafiki wa sana mwenye alitoa musaada wakati wenye ulipita. Familia na watu wenye walichunga mugonjwa wanaweza kuwa na lazima ya kuhakikishiwa kwamba magumu ya mupendwa wao yameisha na kwamba haendelei kuteseka tena. Kwa upendo, Muumbaji wa wanadamu anatuhakikishia kwamba “wafu, hawajui lolote kamwe.”​—Mhubiri 9:5.

MUCHUNGAJI MUKUBWA ZAIDI

Tunaweza kujifunza kukubali musaada wa mutu yeyote

Ni jambo la maana kumutegemea Mungu​—hapana tu wakati mupendwa anakaribia kufa lakini pia wakati wa huzuni yenye inatokea kisha kifo cha mupendwa. Mungu anaweza kuwasaidia kupitia maneno na matendo yenye kufariji ya watu wengine. Doreen anasema hivi: “Nilijifunza kukubali musaada wa mutu yeyote. Kwa kweli, tulipata musaada sana. Mimi na bwana yangu tulitambua waziwazi kwamba ni Yehova mwenye alikuwa anasema, ‘Niko karibu yenu ili kuwasaidia.’ Sitasahau jambo hilo hata siku moja.”

Bila shaka, Yehova Mungu ndiye Muchungaji mukubwa zaidi. Kwa kuwa yeye ni Muumbaji wetu, anaelewa huzuni na maumivu yetu. Iko na uwezo na anapenda kututolea musaada na kitia moyo ili tuweze kupambana na magumu yetu. Jambo la muzuri zaidi, ameahidi kwamba hivi karibuni ataondoa kifo milele na kufufua mamiliare ya watu wenye kuwa katika kumbukumbu lake. (Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:3, 4) Wakati huo, watu wote watakubaliana na maneno haya ya mutume Paulo: ‘Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi muchomo wako?’​—1 Wakorintho 15:55.

^ fu. 2 Majina yamebadilishwa.